-
Danieli 7:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 “Nikaendelea kuangalia katika maono ya usiku, na tazama! mtu fulani kama mwana wa binadamu+ alikuwa akija na mawingu ya mbinguni; naye akaja mbele za Mzee wa Siku,+ nao wakamleta karibu Naye. 14 Naye akapewa utawala,+ heshima,+ na ufalme, ili watu wa makabila, mataifa, na lugha zote wamtumikie.+ Utawala wake ni utawala wa milele ambao hautapitilia mbali, na ufalme wake hautaangamizwa.+
-
-
Mathayo 6:9-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
“‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako+ na litakaswe.*+ 10 Ufalme wako+ na uje. Mapenzi yako+ na yatendeke duniani+ kama ilivyo mbinguni. 11 Utupatie leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii;+ 12 na utusamehe madeni yetu, kama vile tunavyowasamehe wadeni wetu.+ 13 Na usituingize katika majaribu,+ bali utukomboe* kutoka kwa yule mwovu.’+
-