8 kwa kuwa wakati fulani mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru+ kuhusiana na Bwana.+ Endeleeni kutembea kama watoto wa nuru, 9 kwa maana tunda la nuru lina kila namna ya wema na uadilifu na kweli.+
9 Lakini ninyi ni “jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu,+ na watu walio mali ya pekee,+ ili mtangaze kotekote sifa bora”*+ za Yule aliyewaita kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.+
12 Dumisheni mwenendo wenu ukiwa mzuri kati ya mataifa,+ ili wanapowashutumu kuwa watenda dhambi, washuhudie kwa macho yao matendo yenu mazuri+ na hivyo wamtukuze Mungu katika siku ya ukaguzi wake.