Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 19:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Usimlaghai mwenzako+ wala kumnyang’anya vitu vyake.+ Usikae na mshahara wa kibarua usiku kucha mpaka asubuhi.+

  • Kumbukumbu la Torati 24:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 “Usimlaghai kibarua mwenye uhitaji na maskini, awe ni mmoja wa ndugu zako au ni mkaaji mgeni katika nchi yenu, ndani ya majiji* yenu.+ 15 Unapaswa kumpa mshahara wake siku hiyohiyo,+ kabla ya jua kutua, kwa sababu ana uhitaji na uhai wake unategemea* mshahara wake. Usipofanya hivyo, atamlilia Yehova, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.+

  • Yeremia 22:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Ole wake anayejenga nyumba yake bila uadilifu

      Na vyumba vyake vya juu bila haki,

      Anayemfanya mwanadamu mwenzake amtumikie bure,

      Na ambaye anakataa kumlipa malipo yake;+

  • Malaki 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Nitawakaribia ili niwahukumu, nami nitakuwa shahidi asiyesita* dhidi ya walozi,+ dhidi ya wazinzi, dhidi ya watu wanaotoa viapo vya uwongo,+ dhidi ya wale wanaomlaghai kibarua,+ mjane, na yatima,*+ na dhidi ya wale wanaokataa kumsaidia* mgeni.+ Watu hao hawaniogopi,” asema Yehova wa majeshi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki