Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 14
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Wafalme—Yaliyomo

      • Amazia, mfalme wa Yuda (1-6)

      • Apigana vita na Waedomu na Waisraeli (7-14)

      • Kifo cha Yehoashi wa Israeli (15, 16)

      • Kifo cha Amazia (17-22)

      • Yeroboamu wa Pili, mfalme wa Israeli (23-29)

2 Wafalme 14:1

Marejeo

  • +2Fa 13:10

2 Wafalme 14:2

Marejeo

  • +2Nya 25:1-4

2 Wafalme 14:3

Marejeo

  • +1Fa 15:5
  • +2Nya 24:2

2 Wafalme 14:4

Marejeo

  • +1Fa 15:14
  • +2Fa 12:1, 3

2 Wafalme 14:5

Marejeo

  • +2Fa 12:20; 2Nya 24:25

2 Wafalme 14:6

Marejeo

  • +Kum 24:16

2 Wafalme 14:7

Marejeo

  • +2Fa 8:20
  • +2Sa 8:13; 1Nya 18:12
  • +2Nya 25:11, 12

2 Wafalme 14:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “tukutane uso kwa uso.”

Marejeo

  • +2Nya 25:17-19

2 Wafalme 14:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba lako la mfalme.”

Marejeo

  • +2Fa 14:7

2 Wafalme 14:11

Marejeo

  • +2Nya 25:15, 16
  • +Yos 15:10, 12; 21:8, 16
  • +2Nya 25:20-24

2 Wafalme 14:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “katika hema lake.”

2 Wafalme 14:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Karibu mita 178 (futi 584). Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Ne 8:16; 12:38, 39
  • +Yer 31:38; Zek 14:10

2 Wafalme 14:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba la mfalme.”

2 Wafalme 14:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Yeroboamu wa Pili.

Marejeo

  • +2Fa 10:35; 13:9
  • +Ho. 1:1; Amo 1:1; 7:10

2 Wafalme 14:17

Marejeo

  • +2Fa 14:1
  • +2Fa 13:10
  • +2Nya 25:25-28

2 Wafalme 14:19

Marejeo

  • +2Fa 12:20

2 Wafalme 14:20

Marejeo

  • +1Fa 2:10

2 Wafalme 14:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Yehova Amesaidia.” Anaitwa Uzia katika 2Fa 15:13; 2Nya 26:1-23; Isa 6:1; na Zek 14:5.

Marejeo

  • +Mt 1:8
  • +2Fa 15:1, 2
  • +2Nya 26:1

2 Wafalme 14:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Amazia baba yake.

Marejeo

  • +Kum 2:8; 1Fa 9:26; 2Fa 16:6
  • +2Nya 26:2

2 Wafalme 14:23

Marejeo

  • +Ho. 1:1; Amo 1:1

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    “Kila Andiko,” uku. 153

2 Wafalme 14:24

Marejeo

  • +1Fa 12:28-30; 13:34; Zb 106:20

2 Wafalme 14:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “njia ya kuingia Hamathi.”

  • *

    Yaani, Bahari ya Chumvi.

Marejeo

  • +Hes 13:21; 34:2, 7, 8
  • +Kum 3:16, 17
  • +Yon 1:1; Mt 12:39
  • +Yos 19:10, 13

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Igeni, kur. 108-109

    Mnara wa Mlinzi,

    1/1/2009, uku. 25

    “Kila Andiko,” uku. 153

  • Fahirishi ya Machapisho

    w09 1/1 25

2 Wafalme 14:26

Marejeo

  • +Kut 3:7; Amu 10:16; Zb 106:43, 44

2 Wafalme 14:27

Marejeo

  • +Yer 31:20
  • +2Fa 13:4, 5

2 Wafalme 14:28

Marejeo

  • +2Sa 8:6
  • +2Nya 8:3

2 Wafalme 14:29

Marejeo

  • +2Fa 15:8

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Fal. 14:12Fa 13:10
2 Fal. 14:22Nya 25:1-4
2 Fal. 14:31Fa 15:5
2 Fal. 14:32Nya 24:2
2 Fal. 14:41Fa 15:14
2 Fal. 14:42Fa 12:1, 3
2 Fal. 14:52Fa 12:20; 2Nya 24:25
2 Fal. 14:6Kum 24:16
2 Fal. 14:72Fa 8:20
2 Fal. 14:72Sa 8:13; 1Nya 18:12
2 Fal. 14:72Nya 25:11, 12
2 Fal. 14:82Nya 25:17-19
2 Fal. 14:102Fa 14:7
2 Fal. 14:112Nya 25:15, 16
2 Fal. 14:11Yos 15:10, 12; 21:8, 16
2 Fal. 14:112Nya 25:20-24
2 Fal. 14:13Ne 8:16; 12:38, 39
2 Fal. 14:13Yer 31:38; Zek 14:10
2 Fal. 14:162Fa 10:35; 13:9
2 Fal. 14:16Ho. 1:1; Amo 1:1; 7:10
2 Fal. 14:172Fa 14:1
2 Fal. 14:172Fa 13:10
2 Fal. 14:172Nya 25:25-28
2 Fal. 14:192Fa 12:20
2 Fal. 14:201Fa 2:10
2 Fal. 14:21Mt 1:8
2 Fal. 14:212Fa 15:1, 2
2 Fal. 14:212Nya 26:1
2 Fal. 14:22Kum 2:8; 1Fa 9:26; 2Fa 16:6
2 Fal. 14:222Nya 26:2
2 Fal. 14:23Ho. 1:1; Amo 1:1
2 Fal. 14:241Fa 12:28-30; 13:34; Zb 106:20
2 Fal. 14:25Hes 13:21; 34:2, 7, 8
2 Fal. 14:25Kum 3:16, 17
2 Fal. 14:25Yon 1:1; Mt 12:39
2 Fal. 14:25Yos 19:10, 13
2 Fal. 14:26Kut 3:7; Amu 10:16; Zb 106:43, 44
2 Fal. 14:27Yer 31:20
2 Fal. 14:272Fa 13:4, 5
2 Fal. 14:282Sa 8:6
2 Fal. 14:282Nya 8:3
2 Fal. 14:292Fa 15:8
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Wafalme 14:1-29

Kitabu cha Pili cha Wafalme

14 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Mfalme Yehoashi wa Yuda akawa mfalme. 2 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 29 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Yehoadini wa Yerusalemu.+ 3 Aliendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, lakini si kama Daudi+ babu yake. Alifanya mambo yote kama Yehoashi baba yake.+ 4 Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa,+ na watu bado walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu.+ 5 Mara tu ufalme ulipoimarika kabisa mikononi mwake, aliwaua watumishi wake waliomuua mfalme, baba yake.+ 6 Lakini hakuwaua wana wa wauaji hao, kulingana na amri hii ya Yehova iliyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa: “Akina baba hawapaswi kuuawa kwa sababu ya wana wao, na wana hawapaswi kuuawa kwa sababu ya baba zao; lakini kila mtu anapaswa kuuawa kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe.”+ 7 Akawaua Waedomu+ katika Bonde la Chumvi,+ wanaume 10,000, akaliteka jiji la Sela katika vita hivyo,+ na tangu wakati huo jiji hilo likaitwa Yoktheeli.

8 Kisha Amazia akawatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli, akisema: “Njoo, tupambane vitani.”*+⁠ 9 Mfalme Yehoashi wa Israeli akatuma ujumbe huu kwa Mfalme Amazia wa Yuda: “Gugu lenye miiba kule Lebanoni lilituma ujumbe huu kwa mwerezi huko Lebanoni, ‘Mpe mwanangu binti yako awe mke wake.’ Hata hivyo, mnyama wa mwituni wa Lebanoni akapita karibu na kulikanyaga-kanyaga gugu hilo lenye miiba. 10 Ni kweli kwamba uliwaangamiza Waedomu,+ kwa hiyo moyo wako umekuwa na kiburi. Furahia utukufu wako, lakini kaa katika nyumba yako mwenyewe.* Kwa nini utafute msiba kisha uanguke, na kuwaangusha pia watu wa Yuda?” 11 Lakini Amazia hakusikiliza.+

Basi Mfalme Yehoashi wa Israeli akapanda kwenda huko, naye akapambana vitani na Mfalme Amazia wa Yuda huko Beth-shemeshi,+ jiji la Yuda.+ 12 Watu wa Yuda wakashindwa na Waisraeli, kwa hiyo kila mmoja akakimbilia nyumbani kwake.* 13 Mfalme Yehoashi wa Israeli akamkamata Mfalme Amazia wa Yuda, mwana wa Yehoashi mwana wa Ahazia, huko Beth-shemeshi. Kisha wakaja Yerusalemu, naye akabomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu+ mpaka Lango la Pembeni,+ urefu wa mikono 400.* 14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vitu vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mfalme,* na pia akachukua mateka. Kisha akarudi Samaria.

15 Na mambo mengine katika historia ya Yehoashi, mambo aliyofanya na ukuu wake na jinsi alivyopigana na Mfalme Amazia wa Yuda, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 16 Kisha Yehoashi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake huko Samaria+ pamoja na wafalme wa Israeli; na Yeroboamu mwana wake*+ akawa mfalme baada yake.

17 Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda aliendelea kuishi kwa miaka 15 baada ya kifo cha Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.+ 18 Na mambo mengine katika historia ya Amazia, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 19 Baadaye njama ikapangwa dhidi yake+ huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatie huko Lakishi, nao wakamuua huko. 20 Kwa hiyo wakambeba juu ya farasi, naye akazikwa Yerusalemu pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ 21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria,*+ aliyekuwa na umri wa miaka 16,+ wakamweka kuwa mfalme baada ya Amazia baba yake.+ 22 Alijenga upya jiji la Elathi+ na kulirudisha kwa Yuda baada ya mfalme* kuzikwa pamoja na mababu zake.+

23 Katika mwaka wa 15 wa utawala wa Amazia mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu+ mwana wa Mfalme Yehoashi wa Israeli akawa mfalme huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 41. 24 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova. Hakuacha dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Waisraeli kutenda.+ 25 Alirudisha mpaka wa Israeli kuanzia Lebo-hamathi*+ hadi kwenye Bahari ya Araba,*+ kulingana na neno ambalo Yehova Mungu wa Israeli alisema kupitia Yona+ mtumishi wake, mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-heferi.+ 26 Kwa maana Yehova alikuwa ameyaona mateso makali sana ya Waisraeli.+ Hakukuwa na yeyote aliyebaki wa kuwasaidia Waisraeli, hata watu wasio na uwezo au walio dhaifu hawakuwepo. 27 Lakini Yehova alikuwa ameahidi kwamba hatafutilia mbali jina la Israeli kutoka chini ya mbingu.+ Kwa hiyo akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.+

28 Na mambo mengine katika historia ya Yeroboamu, mambo yote aliyofanya na ukuu wake, jinsi alivyopigana na jinsi alivyorudisha jiji la Damasko+ na Hamathi+ ili yamilikiwe tena na Yuda nchini Israeli, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 29 Kisha Yeroboamu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake, pamoja na wafalme wa Israeli; na Zekaria+ mwanawe akawa mfalme baada yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki