Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 31
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Mambo ya Nyakati—Yaliyomo

      • Hezekia aung’oa uasi imani (1)

      • Makuhani na Walawi wategemezwa ifaavyo (2-21)

2 Mambo ya Nyakati 31:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Kut 23:24
  • +Kum 7:5; 2Fa 18:1, 4; 2Nya 14:2, 3; 34:1, 3
  • +Kum 12:2
  • +2Nya 23:16, 17
  • +2Nya 30:1, 18

2 Mambo ya Nyakati 31:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kambi.”

Marejeo

  • +1Nya 24:1
  • +1Nya 23:6
  • +2Nya 8:14
  • +1Nya 23:13, 27-30

2 Mambo ya Nyakati 31:3

Marejeo

  • +2Nya 30:24
  • +Kut 29:39
  • +Hes 28:9
  • +Hes 10:10
  • +Kum 16:16

2 Mambo ya Nyakati 31:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wajitoe kikamili kwa.”

Marejeo

  • +Hes 18:21; Ne 10:38, 39

2 Mambo ya Nyakati 31:5

Marejeo

  • +Hes 18:12
  • +Kut 22:29; 23:19; Ne 10:37
  • +Met 3:9

2 Mambo ya Nyakati 31:6

Marejeo

  • +Law 27:30; Kum 14:28

2 Mambo ya Nyakati 31:7

Marejeo

  • +Law 23:16
  • +Law 23:24

2 Mambo ya Nyakati 31:10

Marejeo

  • +Hes 18:8
  • +Mal 3:10

2 Mambo ya Nyakati 31:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “vyumba vya kulia chakula.”

Marejeo

  • +Ne 10:38, 39; 12:44

2 Mambo ya Nyakati 31:12

Marejeo

  • +Law 27:30; Kum 14:28

2 Mambo ya Nyakati 31:14

Marejeo

  • +1Nya 26:17, 19
  • +Kum 12:5, 6; 16:10
  • +Hes 18:8
  • +Law 2:10; 7:1

2 Mambo ya Nyakati 31:15

Marejeo

  • +Yos 21:19
  • +1Nya 24:1

2 Mambo ya Nyakati 31:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Marejeo

  • +1Nya 24:4
  • +Hes 4:2, 3; 8:24; 1Nya 23:24
  • +1Nya 23:6

2 Mambo ya Nyakati 31:19

Marejeo

  • +Law 25:33, 34; Hes 35:2; Yos 21:13

2 Mambo ya Nyakati 31:21

Marejeo

  • +2Nya 29:35

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Nya. 31:1Kut 23:24
2 Nya. 31:1Kum 7:5; 2Fa 18:1, 4; 2Nya 14:2, 3; 34:1, 3
2 Nya. 31:1Kum 12:2
2 Nya. 31:12Nya 23:16, 17
2 Nya. 31:12Nya 30:1, 18
2 Nya. 31:21Nya 24:1
2 Nya. 31:21Nya 23:6
2 Nya. 31:22Nya 8:14
2 Nya. 31:21Nya 23:13, 27-30
2 Nya. 31:32Nya 30:24
2 Nya. 31:3Kut 29:39
2 Nya. 31:3Hes 28:9
2 Nya. 31:3Hes 10:10
2 Nya. 31:3Kum 16:16
2 Nya. 31:4Hes 18:21; Ne 10:38, 39
2 Nya. 31:5Hes 18:12
2 Nya. 31:5Kut 22:29; 23:19; Ne 10:37
2 Nya. 31:5Met 3:9
2 Nya. 31:6Law 27:30; Kum 14:28
2 Nya. 31:7Law 23:16
2 Nya. 31:7Law 23:24
2 Nya. 31:10Hes 18:8
2 Nya. 31:10Mal 3:10
2 Nya. 31:11Ne 10:38, 39; 12:44
2 Nya. 31:12Law 27:30; Kum 14:28
2 Nya. 31:141Nya 26:17, 19
2 Nya. 31:14Kum 12:5, 6; 16:10
2 Nya. 31:14Hes 18:8
2 Nya. 31:14Law 2:10; 7:1
2 Nya. 31:15Yos 21:19
2 Nya. 31:151Nya 24:1
2 Nya. 31:171Nya 24:4
2 Nya. 31:17Hes 4:2, 3; 8:24; 1Nya 23:24
2 Nya. 31:171Nya 23:6
2 Nya. 31:19Law 25:33, 34; Hes 35:2; Yos 21:13
2 Nya. 31:212Nya 29:35
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Mambo ya Nyakati 31:1-21

Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati

31 Mara tu walipomaliza kufanya mambo hayo yote, Waisraeli wote waliokuwepo wakaenda katika majiji ya Yuda, nao wakazivunjavunja nguzo takatifu,+ wakaikatakata miti mitakatifu,*+ na kubomoa mahali pa juu+ na madhabahu+ katika nchi yote ya Yuda na Benjamini, na pia kule Efraimu na Manase,+ mpaka walipoviharibu kabisa vitu hivyo, kisha Waisraeli wote wakarudi katika majiji yao, kila mmoja kwenye miliki yake.

2 Kisha Hezekia akawaweka makuhani katika vikundi vyao+ na Walawi katika vikundi vyao,+ kila kuhani na Mlawi katika utumishi wake,+ kwa ajili ya dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, ili wahudumu na kushukuru na kusifu katika malango ya nyua* za Yehova.+ 3 Baadhi ya mali za mfalme mwenyewe zilitolewa kwa ajili ya dhabihu za kuteketezwa,+ kutia ndani dhabihu zilizotolewa asubuhi na jioni,+ na pia dhabihu za kuteketezwa kwa ajili ya Sabato,+ miezi mipya,+ na sherehe mbalimbali,+ kulingana na mambo yaliyoandikwa katika Sheria ya Yehova.

4 Isitoshe, aliwaamuru watu walioishi Yerusalemu watoe fungu ambalo makuhani na Walawi walistahili kupokea,+ ili waishike kabisa* sheria ya Yehova. 5 Mara tu agizo hilo lilipotolewa, Waisraeli walitoa kwa wingi mazao ya kwanza ya nafaka, divai mpya, mafuta,+ na asali, na mazao yote ya shambani;+ walileta kwa wingi sehemu ya kumi ya kila kitu.+ 6 Na watu wa Israeli na wa Yuda waliokuwa wakiishi katika majiji ya Yuda walileta pia sehemu ya kumi ya ng’ombe na kondoo na sehemu ya kumi ya vitu vitakatifu+ vilivyotakaswa kwa ajili ya Yehova Mungu wao. Walivileta na kuvipanga katika marundo mengi. 7 Katika mwezi wa tatu,+ walianza kuvipanga katika marundo vitu walivyotoa michango; na katika mwezi wa saba+ wakamaliza. 8 Hezekia na wakuu walipokuja na kuona marundo hayo, walimsifu Yehova na kuwabariki watu wake Waisraeli.

9 Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu marundo hayo, 10 ndipo Azaria mkuu wa makuhani wa nyumba ya Sadoki akamwambia: “Tangu watu walipoanza kuleta michango ndani ya nyumba ya Yehova,+ wamekuwa wakila na kushiba na bado kiasi kikubwa kimebaki, kwa maana Yehova amewabariki watu wake, na kiasi hiki kikubwa sana kimebaki.”+

11 Ndipo Hezekia akawaambia watayarishe vyumba vya kuhifadhia vitu hivyo*+ katika nyumba ya Yehova, basi wakavitayarisha. 12 Waliendelea kuleta kwa uaminifu michango, sehemu za kumi,+ na vitu vitakatifu; na Mlawi aliyeitwa Konania aliwekwa kuwa msimamizi wa vitu hivyo vyote, na Shimei ndugu yake alikuwa wa pili. 13 Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yerimothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi, na Benaya walikuwa maofisa waliomsaidia Konania na Shimei ndugu yake, kama Mfalme Hezekia alivyoagiza, na Azaria alikuwa msimamizi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 14 Na Kore mwana wa Imna, Mlawi aliyekuwa mlinzi wa malango upande wa mashariki,+ alisimamia matoleo ya hiari+ ya Mungu wa kweli, naye aligawa mchango uliotolewa kwa Yehova+ na pia vitu vitakatifu kabisa.+ 15 Na Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria, na Shekania walikuwa chini ya usimamizi wake katika majiji ya makuhani,+ katika wadhifa wao wa kuaminiwa, ili wawagawie ndugu zao kwa usawa katika vikundi,+ wakubwa kwa wadogo. 16 Hilo halikutia ndani mchango waliogawiwa wanaume wenye umri wa miaka mitatu na zaidi walioandikishwa kwenye orodha ya koo, ambao walikuja kila siku kutumikia katika nyumba ya Yehova na kutimiza majukumu ya vikundi vyao.

17 Makuhani waliandikishwa katika orodha ya koo kulingana na ukoo wao,*+ kama walivyoandikishwa Walawi waliokuwa na umri wa miaka 20 na zaidi,+ kulingana na majukumu ya vikundi vyao.+ 18 Walioandikishwa katika orodha ya koo walitia ndani watoto wao wote, wake zao, wana wao, na mabinti wao, kutaniko lote—kwa maana walidumisha utakaso wao kwa ajili ya mambo matakatifu kwa sababu ya wadhifa wao wa kuaminiwa— 19 na pia wazao wa Haruni, makuhani walioishi katika mashamba yenye malisho ambayo yalizunguka majiji yao.+ Katika majiji yote, wanaume walikuwa wamechaguliwa na kutajwa majina ili wampe mafungu kila mwanamume kuhani na kila mtu aliyeandikishwa katika orodha ya koo za Walawi.

20 Hezekia alifanya hayo katika nchi yote ya Yuda, naye aliendelea kutenda mema na yaliyo sawa na ya uaminifu mbele za Yehova Mungu wake. 21 Na kila kazi aliyofanya ili kumtafuta Mungu wake, iwe ni kuhusiana na utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli+ au kuhusiana na Sheria na amri, aliifanya kwa moyo wote, naye alifanikiwa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki