Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 13
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Wafalme—Yaliyomo

      • Yehoahazi, mfalme wa Israeli (1-9)

      • Yehoashi, mfalme wa Israeli (10-13)

      • Elisha apima bidii ya Yehoashi (14-19)

      • Kifo cha Elisha; mifupa yake yamfufua mtu (20, 21)

      • Unabii wa mwisho wa Elisha watimizwa (22-25)

2 Wafalme 13:1

Marejeo

  • +2Fa 11:2, 21
  • +2Fa 8:26; 9:27
  • +2Fa 10:30, 35

2 Wafalme 13:2

Marejeo

  • +1Fa 12:28-30; 13:33; 14:16

2 Wafalme 13:3

Marejeo

  • +Ebr 12:29
  • +Law 26:14, 17
  • +1Fa 19:17; 2Fa 8:12
  • +2Fa 13:24

2 Wafalme 13:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “akautuliza uso wa Yehova.”

Marejeo

  • +Kut 3:7; Amu 10:16; 2Fa 14:26, 27

2 Wafalme 13:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, kwa amani na usalama.

Marejeo

  • +Ne 9:27

2 Wafalme 13:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Aliendelea kutembea katika.”

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +2Fa 10:29; 17:21
  • +Kum 7:5; 1Fa 14:15; 16:33

2 Wafalme 13:7

Marejeo

  • +2Fa 8:12; 10:32
  • +Amo 1:3

2 Wafalme 13:9

Marejeo

  • +2Fa 10:35

2 Wafalme 13:10

Marejeo

  • +2Fa 14:1

2 Wafalme 13:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Alitembea katika.”

Marejeo

  • +2Fa 10:29

2 Wafalme 13:12

Marejeo

  • +2Fa 14:8, 13

2 Wafalme 13:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Yeroboamu wa Pili.

Marejeo

  • +2Fa 14:28
  • +2Fa 10:35; 13:9

2 Wafalme 13:14

Marejeo

  • +1Fa 19:16
  • +2Fa 2:11, 12

2 Wafalme 13:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wokovu.”

  • *

    Au “wokovu.”

  • *

    Au “Utaishinda.”

Marejeo

  • +1Sa 29:1; 1Fa 20:26

2 Wafalme 13:19

Marejeo

  • +2Fa 13:25

2 Wafalme 13:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mwaka unapoingia,” inawezekana ni wakati wa masika.

Marejeo

  • +2Fa 1:1; 24:2

2 Wafalme 13:21

Marejeo

  • +Yoh 11:44; Ebr 11:35

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi (Funzo),

    12/2017, uku. 5

    The Watchtower,

    8/1/2005, uku. 11

    11/15/1991, uku. 5

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 8/1 11

2 Wafalme 13:22

Marejeo

  • +1Fa 19:15
  • +2Fa 8:12; 10:32

2 Wafalme 13:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kutoka kwenye uwepo wake.”

Marejeo

  • +2Fa 14:26, 27
  • +Mwa 13:14-16
  • +Mwa 26:3
  • +Mwa 28:13; Zb 105:8; Mik 7:20

2 Wafalme 13:25

Marejeo

  • +2Fa 13:19

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Fal. 13:12Fa 11:2, 21
2 Fal. 13:12Fa 8:26; 9:27
2 Fal. 13:12Fa 10:30, 35
2 Fal. 13:21Fa 12:28-30; 13:33; 14:16
2 Fal. 13:3Ebr 12:29
2 Fal. 13:3Law 26:14, 17
2 Fal. 13:31Fa 19:17; 2Fa 8:12
2 Fal. 13:32Fa 13:24
2 Fal. 13:4Kut 3:7; Amu 10:16; 2Fa 14:26, 27
2 Fal. 13:5Ne 9:27
2 Fal. 13:62Fa 10:29; 17:21
2 Fal. 13:6Kum 7:5; 1Fa 14:15; 16:33
2 Fal. 13:72Fa 8:12; 10:32
2 Fal. 13:7Amo 1:3
2 Fal. 13:92Fa 10:35
2 Fal. 13:102Fa 14:1
2 Fal. 13:112Fa 10:29
2 Fal. 13:122Fa 14:8, 13
2 Fal. 13:132Fa 14:28
2 Fal. 13:132Fa 10:35; 13:9
2 Fal. 13:141Fa 19:16
2 Fal. 13:142Fa 2:11, 12
2 Fal. 13:171Sa 29:1; 1Fa 20:26
2 Fal. 13:192Fa 13:25
2 Fal. 13:202Fa 1:1; 24:2
2 Fal. 13:21Yoh 11:44; Ebr 11:35
2 Fal. 13:221Fa 19:15
2 Fal. 13:222Fa 8:12; 10:32
2 Fal. 13:232Fa 14:26, 27
2 Fal. 13:23Mwa 13:14-16
2 Fal. 13:23Mwa 26:3
2 Fal. 13:23Mwa 28:13; Zb 105:8; Mik 7:20
2 Fal. 13:252Fa 13:19
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Wafalme 13:1-25

Kitabu cha Pili cha Wafalme

13 Katika mwaka wa 23 wa utawala wa Yehoashi+ mwana wa Ahazia+ mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu+ akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 17. 2 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, na kuendelea kutenda dhambi ya Yeroboamu mwana wa Nebati aliyosababisha Waisraeli kutenda.+ Hakugeuka na kuiacha. 3 Kwa hiyo hasira ya Yehova+ ikawaka dhidi ya Waisraeli,+ akawatia mikononi mwa Mfalme Hazaeli+ wa Siria na mikononi mwa Ben-hadadi+ mwana wa Hazaeli siku zao zote.

4 Baada ya muda Yehoahazi akamsihi Yehova amwonyeshe kibali,* naye Yehova akamsikiliza, kwa maana alikuwa ameona jinsi mfalme wa Siria alivyowakandamiza Waisraeli.+ 5 Basi Yehova akawapa Waisraeli mwokozi+ ili awaokoe kutoka mikononi mwa Wasiria, na Waisraeli wakakaa katika nyumba zao kama awali.* 6 (Hata hivyo, hawakuacha dhambi ya nyumba ya Yeroboamu aliyosababisha Waisraeli kutenda.+ Waliendelea kutenda* dhambi hiyo, na mti mtakatifu*+ ukaendelea kusimama huko Samaria.) 7 Yehoahazi akabaki tu na jeshi lenye wapanda farasi 50, magari 10 ya vita, na wanajeshi 10,000 wanaotembea kwa miguu kwa sababu mfalme wa Siria alikuwa amewaangamiza,+ aliwakanyaga-kanyaga kama mavumbi wakati wa kupura.+

8 Na mambo mengine katika historia ya Yehoahazi, mambo yote aliyofanya na ukuu wake, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 9 Kisha Yehoahazi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake huko Samaria;+ na Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.

10 Katika mwaka wa 37 wa utawala wa Mfalme Yehoashi wa Yuda, Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 16. 11 Akaendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, hakuacha kutenda dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati alizosababisha Waisraeli kutenda.+ Aliendelea kutenda* dhambi hizo.

12 Na mambo mengine katika historia ya Yehoashi, mambo yote aliyofanya na ukuu wake na jinsi alivyopigana na Mfalme Amazia wa Yuda,+ je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 13 Kisha Yehoashi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake, na Yeroboamu*+ akaketi kwenye kiti chake cha ufalme. Naye Yehoashi akazikwa huko Samaria pamoja na wafalme wa Israeli.+

14 Sasa Elisha+ alipougua ugonjwa ambao hatimaye ulisababisha kifo chake, Yehoashi mfalme wa Israeli alishuka kwenda kwake na kumlilia akisema: “Baba yangu, baba yangu! Gari la vita la Israeli na wapanda farasi wake!”+ 15 Ndipo Elisha akamwambia: “Chukua upinde na mishale.” Basi akachukua upinde na mishale. 16 Kisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Shika upinde wako.” Basi akashika upinde wake, halafu Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme. 17 Kisha akasema: “Fungua dirisha la upande wa mashariki.” Basi akalifungua. Elisha akasema: “Piga mshale!” Basi akapiga mshale. Sasa akasema: “Mshale wa ushindi* wa Yehova, mshale wa ushindi* dhidi ya Siria! Utapiga* Siria huko Afeki+ mpaka uiangamize kabisa.”

18 Akaendelea kusema: “Chukua mishale,” naye akaichukua. Kisha Elisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Piga ardhi.” Basi akapiga ardhi mara tatu halafu akaacha. 19 Ndipo yule mtu wa Mungu wa kweli akamkasirikia sana na kumwambia: “Ulipaswa kuipiga ardhi mara tano au mara sita! Kama ungefanya hivyo, ungeipiga Siria mpaka uiangamize, lakini sasa utaipiga Siria mara tatu tu.”+

20 Baada ya hayo, Elisha akafa na kuzikwa. Kulikuwa na makundi ya wavamizi+ ya Wamoabu yaliyokuwa yakija nchini mwanzoni mwa mwaka.* 21 Wanaume fulani walipokuwa wakimzika mtu, waliona kundi la wavamizi, kwa hiyo wakamtupa mara moja mtu huyo ndani ya kaburi la Elisha na kukimbia. Mtu huyo alipogusa mifupa ya Elisha, akafufuka+ na kusimama.

22 Sasa Mfalme Hazaeli+ wa Siria aliwakandamiza Waisraeli+ sikuzote za utawala wa Yehoahazi. 23 Hata hivyo, Yehova akawaonyesha kibali na rehema+ na kuwajali kwa sababu ya agano lake na Abrahamu,+ Isaka,+ na Yakobo.+ Hakutaka kuwaangamiza, naye hajawatupa mbali kutoka mbele zake* mpaka leo. 24 Mfalme Hazaeli wa Siria alipokufa, Ben-hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake. 25 Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akayachukua tena majiji ambayo Ben-hadadi mwana wa Hazaeli alikuwa ameyachukua vitani kutoka kwa Yehoahazi baba yake. Yehoashi alimshinda Ben-hadadi mara tatu,+ naye akayakomboa majiji ya Israeli.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki