Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/90 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 3
  • JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 10
  • JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 17
  • JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 24
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 9/90 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 3

Wimbo 154

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Je! Wewe Umejipatia Vifaa kwa Ajili ya Shamba? Toa muhtasari wa vifaa muhimu kwa ajili ya mkoba wa utumishi wa shambani, kutia na Biblia, Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, kile kijitabu Good News for All Nations, trakti, kalamu, toleo la wakati huu na magazeti, kikaratasi cha maandishi ya nyumba kwa nyumba, na kadhalika. Kuwa tumejitayarisha kiakili hututaka tupitie mambo yatakayokaziwa katika fasihi. Pia, sali upate roho takatifu na msaada katika kuwapata watu wa mfano wa kondoo.—Flp. 4:6, 7.

Dak. 20: “Mheshimu Muumba wa Vitu Vyote.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Katika kuzungumza fungu la 3 na 4, mhubiri mwenye mafanikio atoe wonyesho wa Kichwa cha Mazungumzo na kutoa toleo. Onyesha mipango hususa ikifanywa ya ziara ya kurudia.

Dak. 15: Mzee azungumza na vijana kadhaa walio vielelezo vizuri. Zungumzeni mambo makuu kutoka kitabu Young People Ask, sura ya 17 au gSW 11/85, kur. 16-8, “Je! Niache Shule?” Kazia uhitaji wa wazazi kuongoza vijana wachague masomo yanayowasaidia kupata stadi zenye mafaa, na zenye kutumika zitakazowasaidia kujenga wakati ujao pamoja na tengenezo la Mungu na kufuatia masilahi ya Ufalme.

Wimbo 225 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 10

Wimbo 71

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe mipango ya utumishi wa shambani, uwatie moyo wategemeze kutoa ushahidi jioni.

Dak. 15: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Magazeti.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Katika kuzungumza fungu la 8, toa wonyesho wa jinsi mpango unavyoweza kufanywa wa kumpelekea magazeti kwa ukawaida mtu anayeonyesha kupendezwa halisi, ukikazia makala moja yenye upendezi wa kwenu katika gazeti.

Dak. 15: “Je! Wewe Ungali Mtumwa wa Mapokeo Yasiyo ya Kikristo?” Maziko na Makesha. Hotuba ikitolewa na mzee pamoja na ushirika wa wasikilizaji. Zungumza mafungu 44 hadi 55 katika makala mfululizo zilizochapwa kwenye Huduma ya Ufalme Yetu katika 1975 juu ya mapokeo. Tumia maswali yaliyochapwa kukazia mambo makuu.

Dak. 10: “Twawathamini Wenye Umri Mkubwa!” Hotuba ikitolewa na mzee, ikitegemea habari katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Februari 1, 1986, kurasa 28-9 au Mnara wa Mlinzi wa Juni 1, 1987, “Wakristo wa Kweli Wanaheshimu Watu Wenye Umri Mkubwa!” kurasa 4-7. Habari itumiwe ihusu kwenu. Waweza kueleza hasa juu ya kufanya kazi pamoja nao shambani, na kutumia mwendo wa polepole kuwafaa. Waweza kusaidiwa kununua vitu dukani, kufanya miadi na daktari, na kadhalika, nasi kunufaishwa na hekima na ujuzi wao.—Ayu. 15:10; Mit. 16:31; 1 Tim. 5:1, 2.

Wimbo 116 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 17

Wimbo 160

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu na kutoa shukrani zozote kutoka kwa Sosaiti kwa ajili ya upaji uliotolewa. Toa pongezi kwa kundi kwa ajili ya kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote. (Mit. 3:9) Sanduku la Swali. Hotuba ikitolewa na mzee.

Dak. 18: “Uwe Chonjo Kuanza Mafunzo ya Biblia.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Toa habari juu ya hesabu ya mafunzo ya Biblia yanayoongozwa na kundi. Katika fungu la 5, onyesha jinsi funzo linavyoweza kuanzishwa katika ziara ya kwanza. Anza wonyesho mwenye nyumba akionyeshwa kupendezwa kidogo katika mageuzi lakini akubali kwa furaha trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani. Mhubiri azungumzie fungu moja au mawili katika trakti na kufanya mwadi hususa wa kurudi. Halafu, toa wonyesho wa njia ya moja kwa moja, ukitumia mojapo tangulizi katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 10 chini ya “Funzo la Biblia Nyumbani.” Eleza jinsi kutoa ushahidi jioni hutoa fursa kubwa zaidi za kuanza mafunzo na familia nzima-nzima, kwa kuwa kwa ukawaida waume wamo nyumbani wakati huo.

Dak. 15: “Unapofundisha, Fikia Moyo.” Hotuba ikizungumzia mambo makuu manne katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1985, kurasa 16-21. Wasaidie wasikilizaji wathamini uhitaji wa kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo. Pia, eleza wakati wa kuacha kuongoza mafunzo yasiyo na mazao.

Wimbo 121 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 24

Wimbo 69

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia moyo utendaji wa magazeti Jumamosi. Maonyesho mawili mafupi. Moja ambapo kupendezwa kwaonyeshwa, na mwingine ambapo mwenye nyumba haonyeshi kupendezwa na magazeti lakini akubali kusoma trakti. Ambapo kupendezwa kwaonyeshwa, mhubiri aweza kumwelekeza mtu huyo kwenye taarifa juu ya kazi ya elimu ya Biblia ya ulimwenguni pote kwenye ukurasa wa pili wa Mnara wa Mlinzi au ukurasa wa 4 wa Amkeni! Au aweza kutaarifu kifupi kwamba jambo analofanya ni sehemu ya kazi ya elimu ya Biblia ya ulimwenguni pote inayotegemezwa na upaji wa hiari. Huenda mazungumzo yakafungua njia ya kumtolea mwenye nyumba funzo la Biblia nyumbani la bure.

Dak. 20: “Kuwathamini Mapainia Wetu.” Mwangalizi wa utumishi azungumza habari hiyo pamoja na mapainia wawili au watatu juu ya jinsi wamewatia wengine moyo, nao waeleze ni nini hasa kimewatia moyo kundini mwao. Pongeza kundi kwa kuwategemeza mapainia.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Au mwangalizi msimamizi azungumzie “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1984, kurasa 23-4, “Tunaweza kuwasaidiaje wale walio katika kundi letu ambao mtu wa ukoo wao ametengwa na ushirika?”

Wimbo 62 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki