Mikutano ya Utumishi kwa Novemba
Juma Linaloanza Novemba 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 20: “Tumia Lile Neno la Kweli kwa Ustadi.” Kushughulikia makala kwa maswali na majibu. Kazia uhitaji wa kutumia Biblia kwenye milango. Baada ya kuzungumzia fungu la 5, toa onyesho moja kati ya maonyesho yaliyodokezwa katika fungu hilo. Eleza kwamba nyakati nyingine wahubiri waweza kutoa tu kitabu God’s Word kwa watu wanaoonekana kuwa hawataki Biblia nyingine. Hakikisheni kuwa na toleo la Kiswahili la broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya!”
Dak. 15: “New World Translation—Ya Utaalamu na Yenye Kufuatia Haki.” Mazungumzo ya makala ya Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 1991. Kazia mambo yanayoweza kuwa na mafaa katika kutoa Biblia katika utumishi.
Wimbo 23 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 11
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Tia moyo kufanya upainia msaidizi katika Desemba.
Dak. 22: “Kutoa Habari Njema—Kutoa Mafunzo ya Biblia Nyumbani.” Kuishughulikia kwa maswali na majibu. Mhubiri mwenye ujuzi atoe onyesho la jinsi funzo la Biblia laweza kuanzishwa pamoja na mtu ambaye ameonyesha kupendezwa na Biblia iliyotolewa. Pia, onyesha jinsi ya kutumia trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani ili kuanzisha funzo. Watie moyo akina ndugu kufuatia upendezi wowote ulioonyeshwa, iwe vichapo vimeangushwa au la.
Dak. 15: “Je! Wewe Ungali Mtumwa wa Mapokeo Yasiyo ya Kikristo?—Ndoa, Mahari na Uzazi.” Hotuba ikitolewa na mzee kukiwa na ushiriki fulani wa wasikilizaji ikitegemea mafungu 22-29 ya mfululizo wa Huduma ya Ufalme Yetu uliochapishwa katika 1975 kuhusu Mapokeo. Tumia maswali yaliyochapishwa ili kukazia mambo makuu.
Wimbo 167 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu, ripoti ya hesabu, na shukrani za Sosaiti kwa upaji. Shukuru akina ndugu kwa ushiriki wao wa kutoa. Kumbusha akina ndugu kuleta Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1991 kwenye mkutano wa wiki ijayo.
Dak. 20: “Mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi—Sehemu ya 5.” Mazungumzo ya maswali na majibu yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Uliza maelezo ya jinsi wengine wamefaidika na uandalizi huu, au hoji mmoja au wawili ambao wamesaidiwa na ziara ya mwangalizi wa utumishi.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu au “Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti.” Hotuba. Elekeza kwenye mambo yaliyoonwa katika makala hiyo ya Mnara wa Mlinzi ukionyesha matokeo yenye nguvu ambayo Biblia inapata maishani mwa watu. Waweza kutia ndani ripoti zilizo katika Aprili 1, 1991, na Agosti 1, 1991.
Wimbo 75 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Watie moyo wote kushiriki katika utumishi wa shambani mwisho wa juma hili. Kazia makala katika magazeti ya karibuni ambayo yanaweza kutumiwa katika kazi ya magazeti Jumamosi hii.
Dak. 20: “Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Huduma ya Shambani—Sehemu ya 5.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya makala inayomalizia mfululizo wa makala. Watie moyo wote kwa uchangamfu kuhakikisha wanafuata madokezo yaliyotolewa. Kadiri wakati uruhusuvyo, tia ndani mahoji ya mhubiri mwenye bidii au painia ambaye aweza kusimulia faida za kibinafsi anazofurahia kutokana na kushiriki kikamili katika huduma.
Dak. 15: Kutoa magazeti. Pitia makala “Kwa Magazeti” chini ya Kutoa Habari Njema katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1991. Tumia maswali na majibu. Kazia mambo makuu katika mafungu 3, 4, na 5. Halafu uwe na maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri yakionyesha jinsi ya kukazia jambo moja katika utangulizi, likitegemezwa na makala moja katika gazeti moja hilo. Katika kumalizia, toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Tia moyo kutumia kanuni hizo katika kazi ya kawaida ya magazeti.
Wimbo 205 na sala ya kumalizia.