Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni
Juma Linaloanza Juni 1
Dak. 5: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 13: Sanduku la Swali. Ipitiwe kwa maswali na majibu. Kazia kuwa wenye usawaziko kwa jambo hilo na si kuwatolea imla wengine kuchukua msimamo fulani.
Dak. 12: “Uhitaji wa Ainabinadamu wa Kutafuta-Tafuta Mungu.” Maswali na majibu. Tia moyo kuwe na bidii katika kazi yetu shambani mwezi huu. Onyesha jinsi kichapo hicho kinavyoweza kusaidia watu wa dini mbalimbali katika eneo lenu.
Dak. 15: “Kutoa Utangulizi wa Kitabu Mankind’s Search for God.” Zungumzia na utoe wonyesho wa baadhi ya madokezo katika makala. Katika wonyesho mmoja onyesha jinsi ya kutumia mfikio wa moja kwa moja ili kuanzisha mafunzo. Pia, onyesha jinsi zile njia kumi za kutambulisha dini ya kweli katika ukurasa 377 zinavyoweza kutumiwa kwa njia yenye matokeo.
Wimbo 225 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 8
Dak. 10: Matangazo. Tayarisha kimbele kuwa na mapainia wawili wa kawaida au wasaidizi watoe maelezo juu ya matangulizi ambayo wameona kuwa yenye matokeo wanapohubiri katika eneo la kwenu.
Dak. 20: “Uwe na Roho ya Kujidhabihu!” Hotuba juu ya makala katika Mnara wa Mlinzi la Februari 1, 1992, kurasa 25-8. Kazia kwamba kuwa na roho ya kujidhabihu si jambo la kujichagulia bali ni takwa la Kikristo. Sisi hatupati hasara kwa kudhabihu vitu vya kimwili na tafrija ili kufuatilia faida za Ufalme kwanza.
Dak. 15: “Kuchukua Furushi Letu Wenyewe la Daraka.” Mzee azungumzia makala pamoja na kikundi cha familia. Akumbuka jinsi kundi lilivyofurahia na kunufaika na programu ya kusanyiko la mzunguko lililopita na atia moyo kutazamia mbele kwenye programu mpya ya kusanyiko la mzunguko. Auliza vichwa vya familia miongoni mwa wasikilizaji jinsi programu ya 1991 ilivyosaidia jamaa zao. Awatia moyo wote kufanya mipango hususa ili kuhudhuria na kunufaika na programu iliyopangwa kwa ajili ya mwaka wa utumishi wa 1992. Ikiwa tarehe ya kusanyiko litakalofuata yajulikana, hiyo yaweza kutangazwa.
Wimbo 61 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 15
Dak. 10: Matangazo. Taja mambo makuu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Februari. Onyesha sehemu ambayo kundi lenu lilikuwa nayo katika ripoti ya utumishi wa shambani ya Februari. Toa ripoti ya hesabu. Pongeza kundi kwa kazi iliyofanywa katika utumishi wa shambani na kwa utegemezo walo wa kifedha wenye ukarimu.
Dak. 20: Kupangia Kampeni Yetu ya 18 ya Makedonia. Mwangalizi wa utumishi apaswa aeleze waziwazi mipango ya kuhubiri sehemu za maeneo ya kundi zisizofanyiwa kazi mara nyingi na mipango kwa ajili ya kampeni ya maeneo yasiyogawiwa mtu. Makundi mengi yatapokea migawo hususa ya “Makedonia.” Tumieni vizuri siku za soko na mwe na ugavi wa kutosha wa fasihi, hasa broshua katika lugha mbalimbali. Kila kundi linatiwa moyo kusonga mbele zaidi katika sehemu za mbali. Tia moyo kila mmoja awe na ushiriki kamili wa kufikia sehemu ambazo ushahidi hautolewi kwa ukawaida.
Dak. 15: Mazungumzo na maonyesho juu ya mazungumzo ya Biblia na utoaji wa kitabu Mankind’s Search for God, kwa kutumia Isaya 55:6, 7 na Matendo 17:26, 27. Onyesha jinsi wapya na wachanga wanavyoweza kutumia utoaji uliosahilishwa, kwa kutumia tu Isaya 55:6, 7.
Wimbo 154 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 22
Dak. 5: Matangazo. Habari za Kitheokrasi. Katika kupitia habari, linganisha ripoti ya sasa na habari juu ya tawi hilo katika mwaka wa utumishi wa 1986, kama inavyopatikana katika ripoti ya mwaka wa utumishi katika Kitabu-Mwaka cha 1987.
Dak. 20: “Kupainia—Wonyesho wa Upendo.” Maswali na majibu. Baada ya kuzungumzia mafungu 3 na 4, wahoji mapainia wa kawaida watatu (au wahubiri wanaofanya upainia msaidizi kwa ukawaida au mara kwa mara), kutia ndani, ikiwezekana, painia wa kawaida mmoja mchanga aliyepainia punde tu baada ya kumaliza shule. Uliza jinsi walivyopanga mambo yao ili waweze kupainia, ni nini kilichowasukuma wafanye hivyo, ni dhabihu gani za kimwili walizolazimika kufanya, na ni baraka zipi ambazo wamepokea wakitumikia wakiwa mapainia wa kawaida.
Dak. 20: “Kurudi Tukiwa na Kusudi la Kuanzisha Funzo la Biblia.” Mazungumzo na maonyesho. Toa wonyesho wa madokezo ya mazungumzo ya Biblia katika fungu la 3. Tumia mafungu 17-20 kwenye kurasa 372-5 za kitabu Mankind’s Search for God kuwa msingi wa kuanzisha funzo la Biblia.
Wimbo 135 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 29
Dak. 10: Matangazo. Fanya maonyesho mawili mafupi yakionyesha jinsi ya kutoa magazeti katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak. 15: “Mwandamano wa Kimitume.” Mwangalizi wa utumishi aandamana na painia kufanya ziara ya kurudia ya mtu aliyezusha swali: “Je! papa si mwandamizi wa mtume Petro?” Tegemeza mazungumzo juu ya kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 224 hadi 226.
Dak. 20: Mahitaji ya kwenu. Mnaweza kupitia mambo yaliyotolewa kwenye kusanyiko la mzunguko lililopita au kwenye programu ya siku ya kusanyiko la pekee yanayoweza kutumiwa kwenu.
Wimbo 167 na sala ya kumalizia.