Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Septemba 7
  • Juma Linaloanza Septemba 14
  • Juma Linaloanza Septemba 21
  • Juma Linaloanza Septemba 28
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 9/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba

Juma Linaloanza Septemba 7

Wimbo 28

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Pitia sanduku lenye kichwa “Dokezo.”

Dak. 15: “Twaweza Kufanya Kazi Kubwa Zaidi.” Maswali na majibu. Tia moyo wote waweke miradi ifaayo ya mwaka mpya wa utumishi na wafanye bidii kuifikia.—Ona Huduma Yetu, ukurasa wa 116-118.

Dak. 20: “Mapainia Wasaidia Wengine.” Mzee aeleza kwamba kuongezea mazoezi yatolewayo katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, mipango imefanywa ili mapainia wasaidie wengine kibinafsi katika huduma. Atokeza swali linalotegemea makala na kukaribisha wasikilizaji watoe maelezo, hasa mapainia na wahubiri ambao wamehusishwa katika programu hiyo. Fikiria jinsi ya kupata matokeo bora kutokana nayo. Mapainia wanaweza kusimulia jinsi ambavyo wamefurahia na kunufaika katika kushiriki kuwasaidia wengine. Wahubiri ambao wamesaidiwa wanaweza kueleza jinsi wanavyothamini uandalizi huu wenye upendo na kutaja mambo yaliyowasaidia wafikie mafanikio makubwa na shangwe katika huduma.

Wimbo 172 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 14

Wimbo 160

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Mungu Anataka Tufanye Nini? Hotuba. Tutaanza kusoma broshua hii juma lifuatalo kwenye funzo la kitabu. Tia moyo wote wajitayarishe mapema na kuhudhuria kila pindi ili kuifahamu broshua hiyo na kujifunza jinsi ya kuitumia kuwafundisha wengine. Soma fungu chini ya “Jinsi ya Kutumia Broshua Hii.” Tumia habari iliyo katika Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1997, ukurasa wa 16-17, kukazia umaana wa kufundisha kwa maswali, maandiko, na vielezi vilivyo katika broshua. Viongozi wa funzo la kitabu wapaswa kuwekea kielelezo wale wanaoongoza mafunzo ya Biblia nyumbani, kwa kutosema mambo mengi mno na kutoleta mambo ya ziada.—Ona Huduma ya Ufalme Yetu, Juni 1996, ukurasa wa 3, fungu la 5.

Dak. 20: Tulifanyaje Mwaka Jana? Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wapitia ripoti ya utumishi ya kutaniko na hudhurio la mkutano la mwaka uliopita. Wanaeleza mambo yenye kutia moyo ya ripoti hiyo na kukazia sehemu ambazo maendeleo yaweza kufanywa. Je, wahubiri wote walishiriki katika utumishi mwezi wa Agosti? Eleza ni miradi gani ambayo wazee watakazia miezi inayokuja, kutia ndani kusaidia wote wawe wahubiri wa kawaida. Shiriki mambo yanayojenga kutoka ripoti iliyopita ya mwangalizi wa mzunguko.

Wimbo 144 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 21

Wimbo 122

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Pata Kuwajua Ndugu Zako.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo yaliyo kwenye Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1988, ukurasa wa 10-11. Tia moyo wote wachukue hatua ya kufahamiana vizuri.

Wimbo 34 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 28

Wimbo 17

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Septemba. Tia moyo wote wafanye mipango ya kuhubiri zaidi nyumba hadi nyumba katika Oktoba ili kuongeza uangushaji wa magazeti. Rejezea Huduma ya Ufalme Yetu, Oktoba 1996 ukurasa wa 8, ili kupata madokezo ya jinsi ya kutayarisha utoaji mbalimbali. Toa wonyesho wa toleo ukitumia magazeti ya karibuni. Chukua magazeti kwa ajili ya utendaji wa mwisho-juma.

Dak. 20: “Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi wa Utumishi.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi. Baada ya kupitia wajibu wake, aeleza njia hususa ambazo kutaniko laweza kushirikiana ili kuongeza fursa na matokeo ya huduma kwenu.

Dak. 13: Ni Nini Huhitajiwa Ili Kuwa Mhubiri Mzuri wa Kutaniko? Hotuba, na wasikilizaji wakishiriki kwa kiasi fulani. Si lazima mtu awe na uwezo bora zaidi au vipaji; badala yake, inatakikana zaidi kwamba wote wawe na mtazamo wa hiari unaoonyesha upendo, unyenyekevu, bidii, na uthamini. Alika wasikilizaji waeleze kwa nini mambo yafuatayo ni yenye kutamanika: (1) roho ya uchangamfu, (2) kuhudhuria na kushiriki kwa ukawaida katika mikutano, (3) utayari wa kukubali na kutimiza migawo, (4) kushirikiana na wazee na mipango inayofanywa kwa ajili ya kutaniko, (5) kupendezwa kwa unyofu kusaidia wengine, na (6) kushiriki kwa ukawaida katika utumishi wa shambani na kuripoti bila kukawia kila mwezi.

Wimbo 25 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki