-
Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya WakristoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 21
Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo
Njozi ya 5—Ufunuo 8:1–9:21
Habari: Kuvumishwa kwa sita kati ya zile tarumbeta saba
Wakati wa utimizo: Kutoka kuketishwa kwa Kristo Yesu katika kiti cha ufalme katika 1914 hadi dhiki kubwa
1. Kunakuwa nini wakati Mwana-Kondoo anapofungua kifungo cha saba?
“PEPO nne” zimezuiwa mpaka 144,000 wa Israeli wa kiroho wawe wametiwa muhuri na ule “umati mkubwa” uwe umekubaliwa kwa ajili ya kuokoka. (Ufunuo 7:1, 9, NW) Hata hivyo, kabla hiyo dhoruba yenye tufani haijafyatukia dunia, hukumu mbaya za Yehova dhidi ya ulimwengu wa Shetani lazima pia zijulishwe! Mwana-Kondoo aendeleapo kufungua kifungo cha saba na cha mwisho kabisa, lazima Yohana awe anatazama kwa makini aone ni kitu gani kitakunjulika. Sasa yeye anashiriki pamoja na sisi ono lake: “Na wakati yeye [Mwana-Kondoo] alipofungua kifungo cha saba, kukawa kimya katika mbingu kwa muda wapata nusu saa. Na mimi nikaona malaika saba ambao husimama mbele za Mungu, na tarumbeta saba wakapewa wao.”—Ufunuo 8:1, 2, NW.
Wakati wa Sala ya Bidii
2. Kunatukia nini wakati wa nusu saa ya kimya katika mbingu?
2 Hiki ni kimya chenye kutokeza sana! Nusu saa yaweza kuonekana kuwa wakati mrefu unapongojea jambo fulani liwe. Sasa, hata korasi daima ya kimbingu yenye sifa haisikiki tena. (Ufunuo 4:8) Kwa nini? Yohana anaona sababu katika njozi: “Na malaika mwingine akawasili na akasimama kwenye madhabahu, akiwa na chombo cha dhahabu cha uvumba; na kiasi kikubwa cha uvumba akapewa yeye akitoe pamoja na sala za watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu ambayo ilikuwa mbele ya kiti cha ufalme. Na moshi wa uvumba ukapaa kutoka mkono wa malaika pamoja na sala za watakatifu mbele za Mungu.”—Ufunuo 8:3, 4, NW.
3. (a) Kuchomwa kwa uvumba hutukumbusha juu ya nini? (b) Ni nini kusudi la nusu saa ya kimya katika mbingu?
3 Hii inatukumbusha kwamba chini ya mfumo wa mambo wa Kiyahudi, uvumba ulichomwa kila siku kwenye tabenakulo na, katika miaka ya baadaye, kwenye hekalu katika Yerusalemu. (Kutoka 30:1-8) Wakati wa kuchoma uvumba hivyo, Waisraeli wasio wa kikuhani walingojea nje ya eneo takatifu, wakisali—pasipo shaka kwa kimya katika mioyo yao—kwa Mmoja ambaye kwake moshi wa uvumba ulikuwa ukipaa. (Luka 1:10) Yohana sasa anaona kitu fulani kama hicho kikitukia katika mbingu. Uvumba unaotolewa na malaika unashirikishwa na “sala za watakatifu.” Kwa kweli, katika njozi ya mapema zaidi, uvumba unasemwa kuwa ukiwakilisha sala hizo. (Ufunuo 5:8; Zaburi 141:1, 2) Kwa wazi, basi, kimya cha ufananisho katika mbingu ni kuruhusu “sala za wale watakatifu” walio duniani zisikike.
4, 5. Ni matukio gani ya kihistoria yanayotusaidia kujua kipindi cha wakati kinacholingana na nusu saa ya ufananisho yenye kimya?
4 Je! sisi tunaweza kujua wakati hili linapokuwa? Ndiyo, tunaweza, kwa kuchunguza muktadha pamoja na matukio ya kihistoria ya mapema katika “siku ya Bwana.” (Ufunuo 1:10, NW) Wakati wa 1918 na 1919, matukio duniani yalipatana katika njia yenye kutokeza sana na mandhari-mfululizo inayoelezwa kwenye Ufunuo 8:1-4. Kwa miaka 40 kabla ya 1914, Wanafunzi wa Biblia—kama walivyokuwa wakiitwa Mashahidi wa Yehova wakati huo—walikuwa wakitangaza kwa ujasiri kwamba “majira ya Mataifa” yangekwisha wakati huo. Yale matukio yenye kujaa taabu ya 1914 yaliwathibitisha kuwa sahihi. (Luka 21:24; Mathayo 24:3, 7, 8) Lakini wengi wao waliitikadi pia kwamba katika 1914 wao wangechukuliwa kutoka dunia hii wapelekwe kwenye urithi wao wa kimbingu. Hilo halikuwa hivyo. Badala ya hivyo, wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu, walivumilia wakati wa mnyanyaso mkali. Katika Oktoba 31, 1916, Charles T. Russell, msimamizi wa kwanza wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, akafa. Kisha, katika Julai 4, 1918, msimamizi mpya, Joseph F. Rutherford, na wawakilishi wengine saba wa Sosaiti wakasafirishwa kupelekwa kwenye gereza katika Atlanta, Georgia, wakihukumiwa kimakosa miaka mirefu katika jela.
5 Wakristo wenye mioyo myeupe wa jamii ya Yohana walitatizika. Mungu alitaka wao wafanye nini kufuata hapo? Ni lini wangechukuliwa juu mbinguni? Makala moja iliyokuwa na kichwa “Mavuno Yamekwisha—Ni Nini Kitafuata?” Ilitokea katika toleo la Mei 1, 1919, la Mnara wa Mlinzi. Hiyo ilionyesha hali hii ya kutokuwa na hakika na ikatia moyo waaminifu waendelee kuvumilia, ikiongeza: “Sisi tunaitikadi ni usemi wa kweli sasa kwamba mavuno ya jamii ya ufalme ni uhakika uliokamilishwa, kwamba wote hao wamekwisha tiwa muhuri na kwamba mlango umefungwa.” Katika pindi hii ngumu, sala za bidii za jamii ya Yohana zilikuwa zikipaa, kana kwamba katika moshi wa kiasi kikubwa cha uvumba. Na sala zao zilikuwa zikisikiwa!
Kuvurumisha Moto Kwenye Dunia
6. Kunakuwa na nini baada ya hicho kimya katika mbingu, na ni katika kuitikia nini?
6 Yohana anatuambia: “Lakini mara hiyo malaika akachukua chombo cha uvumba, na kukijaza baadhi ya moto wa madhabahu na kuuvurumisha kwenye dunia. Na ngurumo zikatukia na sauti na meme na tetemeko la dunia.” (Ufunuo 8:5, NW) Baada ya kimya, kuna utendaji wa ghafula wenye kutazamisha! Kwa wazi huo ni katika kuitikia “sala za watakatifu,” kwa kuwa huo unaanzishwa na moto uliochukuliwa kutoka madhabahu ya uvumba. Huko nyuma katika 1513 K.W.K. kwenye Mlima Sinai, ngurumo na meme, kelele kubwa, moto, na kutetemeka kwa mlima viliashiria kugeuzwa kwa uangalifu wa Yehova kuelekea watu wake. (Kutoka 19:16-20) Madhihirisho kama hayo yanayoripotiwa na Yohana hali kadhalika huonyesha uangalifu wa Yehova ukitolewa kwa watumishi wake duniani. Lakini anachoona Yohana kinatolewa kwa ishara. (Ufunuo 1:1, NW) Kwa hiyo moto, ngurumo, sauti, meme, na tetemeko la dunia vya ufananisho vitafasiriwaje leo?
7. (a) Ni moto gani wa ufananisho ambao Yesu aliwasha duniani wakati wa huduma yake? (b) Ndugu za kiroho za Yesu waliwashaje moto katika Jumuiya ya Wakristo?
7 Pindi moja, Yesu aliambia wanafunzi wake: “Mimi nilikuja kuanzisha moto juu ya dunia.” (Luka 12:49, NW) Kwa kweli, yeye aliwasha moto. Kwa kuhubiri kwake kwa bidii, Yesu alifanya Ufalme wa Mungu uwe ndio suala kubwa mbele ya watu wa Kiyahudi, na huo ulitokeza ubishani mkubwa kotekote katika taifa hilo. (Mathayo 4:17, 25; 10:5-7, 17, 18) Katika 1919 ndugu za kiroho za Yesu waliokuwako duniani, kile kikosi kidogo cha Wakristo wapakwa-mafuta ambao walikuwa wameokoka siku zenye kujaribu za Vita ya Ulimwengu 1, waliwasha moto kama huo katika Jumuiya ya Wakristo. Katika Septemba wa mwaka huo, roho ya Yehova ilionekana wazi kwa njia yenye kutokeza sana wakati Mashahidi wake washikamanifu walipokusanyika katika Sida Pointi, Ohaiyo, U.S.A. kutoka karibu na mbali. Joseph F. Rutherford, aliyekuwa ameachiliwa hivi majuzi kutoka jela na ambaye karibuni angeondolewa kabisa mashtaka yote, alihutubia mkusanyiko huo kwa ujasiri, akisema: “Kwa kutii amri ya Bwana-Mkubwa wetu, na tukitambua pendeleo na wajibu wetu wa kufanya vita dhidi ya ngome za kosa ambazo zimeshika watu katika utumwa kwa muda mrefu sana, shughuli yetu ilikuwa na ni kutangaza ufalme mtukufu unaokuja wa Mesiya.” Hilo ndilo suala kuu—Ufalme wa Mungu!
8, 9. (a) J. F. Rutherford alielezaje habari ya mwelekeo na tamaa ya watu wa Mungu wakati wa miaka migumu ya vita? (b) Ilikuwaje kwamba moto ulivurumishwa kwenye dunia? (c) Ngurumo, sauti, meme, na tetemeko la dunia vimetukiaje?
8 Akirejezea magumu ya karibuni ya watu wa Mungu, mhutubu huyo alisema: “Shambulio la adui lilikuwa lisilo na sikitikio sana hivi kwamba wengi wa kundi lenye kupendwa la Bwana waliduwaa wakasimama tuli kwa mshangao, wakisali na kungojea Bwana aonyeshe penzi lake. . . . Lakini ijapokuwa kivunja-moyo cha kitambo, kulikuwako tamaa yenye kuwaka ya kutangaza ujumbe wa ufalme.”—Ona toleo la Septemba 15, 1919 la The Watch Tower ukurasa 280.
9 Katika 1919 tamaa hiyo ilitoshelezwa. Hiki kikundi kidogo lakini chenye kutenda cha Wakristo kiliwashwa moto, kusema kiroho, waanze kampeni ya kuhubiri ulimwenguni pote. (Linga 1 Wathesalonike 5:19.) Moto ulivurumishwa duniani katika njia ya kwamba Ufalme wa Mungu ukawa ndilo suala lenye kuwaka, na ndivyo unaendelea kuwa! Sauti zenye nguvu zilichukua mahali pa kimya, zikivumisha ujumbe wa Ufalme kwa uwazi. Maonyo ya dhoruba yenye kunguruma kutoka Biblia yalitoa sauti. Kama mimeto ya umeme, miale miangavu ya ukweli iliangaza kutoka Neno la Yehova la kiunabii, na tetemeko la dunia lenye nguvu likaanza kutikisa milki ya kidini mpaka misingi yayo. Jamii ya Yohana iliona kwamba kulikuwako kazi ya kufanywa. Na kufikia leo hii, kazi hiyo huendelea kupanuka kwa njia tukufu kotekote katika dunia inayokaliwa!—Warumi 10:18.
Kujitayarishia Mipigo ya Tarumbeta
10. Malaika saba wanajitarisha kufanya nini, na kwa nini?
10 Yohana anaendelea kusema: “Na malaika saba waliokuwa na tarumbeta saba wakajitayarisha kuzipuliza.” (Ufunuo 8:6, NW) Kupulizwa kwa tarumbeta hizo kunamaanisha nini? Katika siku za Israeli, mipigo ya tarumbeta ilitumiwa kuashiria siku za maana au matukio yanayostahili kuangaliwa. (Walawi 23:24; 2 Wafalme 11:14) Hali kadhalika, mipigo ya tarumbeta ambayo Yohana atasikia itavuta uangalifu kuelekea matukio ya umaana wa uhai na kifo.
11. Ni kazi gani ya matayarisho duniani iliyokuwa ikifanywa na ile jamii ya Yohana tangu 1919 mpaka 1922?
11 Malaika walipojitayarisha kupuliza tarumbeta hizo, bila shaka wao walikuwa wakitoa mwelekezo kwa kazi ya matayarisho duniani. Tangu 1919 mpaka 1922, jamii ya Yohana iliyotiwa uhai mpya ilikuwa na shughuli katika kupanga tena kitengenezo huduma ya peupe na kujenga vifaa vya kutangazia. Katika 1919 lile gazeti The Golden Age, linalojulikana leo kuwa Amkeni!, lilikuwa limetokezwa likiwa “Jarida la Uhakika, Tumaini, na Usadikisho”—kifaa kama tarumbeta ambacho kingetimiza daraka kubwa katika kufunua wazi kujiingiza kwa dini bandia katika siasa.
12. Ni nini kinachotolewa habari na kila mmojapo mipigo ya tarumbeta, ikitukumbusha nini katika siku ya Musa?
12 Kama tutakavyoona, kila mmojapo wa mipigo ya tarumbeta hutoa habari ya mandhari moja yenye kutokeza ambayo katika hiyo tauni za kuogopesha sana huathiri visehemu vya dunia. Baadhi ya hizo hutukumbusha sisi zile tauni ambazo Yehova alipeleka kuadhibu Misri katika siku ya Musa. (Kutoka 7:19–12:32) Hizo zilikuwa maonyesho ya hukumu za Yehova juu ya taifa hilo, nazo zilifungulia njia watu wa Mungu waponyoke kutoka utumwa. Tauni anazoona Yohana zinatimiza jambo fulani kama hilo. Hata hivyo, si tauni halisi. Ni ishara ambazo hufananisha hukumu za uadilifu za Yehova.—Ufunuo 1:1, NW.
Kutambulisha “Theluthi”
13. Kunakuwa nini wakati tarumbeta nne za kwanza zinapopulizwa, na hii inazusha swali gani?
13 Kama tutakavyoona, wakati tarumbeta nne za kwanza zinapopulizwa, tauni zinapiga “theluthi moja” ya dunia, ya bahari, ya mito, na vibubujiko vya maji, na ya machimbuko ya dunia ya nuru. (Ufunuo 8:7-12, NW) Theluthi moja ni sehemu kubwa ya kitu lakini si chote kwa ujumla. (Linga Isaya 19:24; Ezekieli 5:2; Zekaria 13:8, 9.) Hivyo ni “theluthi” gani ingekuwa yenye kustahili zaidi sana tauni hizi? Sehemu iliyo kubwa zaidi ya aina ya binadamu imepofushwa na kufisidiwa na Shetani na mbegu yake. (Mwanzo 3:15; 2 Wakorintho 4:4, NW) Hali ni kama ilivyoelezwa na Daudi: “Wao wote wamekengeuka, wao wote kwa kufanana ni wafisadi; hakuna mmoja ambaye anafanya mema, hakuna hata mmoja.” (Zaburi 14:3, NW) Ndiyo, aina ya binadamu kwa ujumla imo katika hatari ya kupokea hukumu mbaya. Lakini kisehemu chayo hasa ni chenye hatia. Sehemu moja—“theluthi moja”—ilipaswa kujua vizuri zaidi! Hiyo ni “theluthi” gani?
14. Ni nini ile “theluthi” inayopokea jumbe zenye kusumbua kutoka kwa Yehova?
14 Ni Jumuiya ya Wakristo! Katika miaka ya 1920 milki yayo ilitia ndani yapata theluthi moja ya aina ya binadamu. Dini yayo ni tunda la uasi-imani (ukengeufu) mkubwa kutoka Ukristo wa kweli—uasi-imani ambao Yesu na wanafunzi wake walitabiri. (Mathayo 13:24-30; Matendo 20:29, 30; 2 Wathesalonike 2:3; 2 Petro 2:1-3) Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo hudai kuwa katika hekalu la Mungu na wamejionyesha kuwa walimu wa Ukristo. Lakini mafundisho yao ya kidini yako mbali sana na ukweli wa Biblia, na kwa kuendelea wameliletea jina la Mungu sifa mbaya. Ikiwakilishwa kwa kufaa na “theluthi” ya ufananisho, Jumuiya ya Wakristo inapokea ujumbe wenye nguvu, wenye kusumbua kutoka kwa Yehova. “Theluthi” hiyo ya aina ya binadamu haistahili hata kidogo upendeleo wa kimungu!
15. (a) Je! kila mmojapo mipigo ya tarumbeta unahusu mwaka mmoja hasa? Eleza. (b) Ni sauti ya nani ambayo imeongezwa kwa ile ya jamii ya Yohana katika kupiga mbiu ya hukumu za Yehova?
15 Kwa kupatana na kuwa kwamba kuna mfululizo wa mipigo ya tarumbeta, maazimio maalumu yalitolewa kwenye mikusanyiko saba kuanzia 1922 mpaka 1928. Lakini kupigwa kwa tarumbeta hakukuhusu miaka hiyo tu. Kufichua kwa nguvu njia mbovu za Jumuiya ya Wakristo kumekuwa kwenye kuendelea, kwenye kusonga mbele, muda wote wa “ile siku ya Bwana.” Hukumu za Yehova lazima zipigiwe mbiu katika ulimwengu wote mzima, mataifa yote, ijapokuwa chuki na minyanyaso ya kimataifa. Hapo ndipo tu ule mwisho wa mfumo wa Shetani huja. (Marko 13:10, 13) Kwa furaha, “umati mkubwa” umeongeza sasa sauti yao kwenye ile ya jamii ya Yohana katika kufanya matamko hayo yenye mngurumo ya umaana wa ulimwenguni pote.
Theluthi Moja ya Dunia Yateketezwa
16. Ni nini kinachofuata wakati malaika wa kwanza anapopuliza tarumbeta yake?
16 Akitoa ripoti ya hao malaika, Yohana aandika: “Na wa kwanza akapuliza tarumbeta yake. Na kukatukia mvua-mawe na moto uliotangamana na damu, nayo ikavurumishwa kwenye dunia; na theluthi moja ya dunia ikateketezwa, na theluthi moja ya miti ikateketezwa, na mimea yote ya chanikiwiti ikateketezwa.” (Ufunuo 8:7, NW) Hii inalingana na ile tauni ya saba juu ya Misri, lakini inamaanisha nini kwa nyakati zetu?—Kutoka 9:24.
17. (a) Ni nini kinachowakilishwa na neno “dunia” kwenye Ufunuo 8:7, NW? (b) Theluthi ya dunia ya Jumuiya ya Wakristo inateketezwaje?
17 Katika Biblia, neno “dunia” mara nyingi hurejezea aina ya binadamu. (Mwanzo 11:1; Zaburi 96:1, NW) Kwa kuwa tauni ya pili iko juu ya bahari, ambayo pia inahusiana na aina ya binadamu, “dunia” lazima irejezee ile jamii ya kibinadamu iliyo imara zaidi ambayo Shetani amejenga na ambayo inakaribia kuharibiwa. (2 Petro 3:7; Ufunuo 21:1, NW) Mandhari-mfululizo ya tauni inafunua kwamba “theluthi” ya dunia ya Jumuiya ya Wakristo imeunguzwa na joto lenye kuchoma la kutokuwa na kibali cha Yehova. Wale walio mashuhuri wayo—wanaosimama kama miti katikati yayo—‘wanateketezwa’ na kule kupigwa mbiu ya hukumu mbaya ya Yehova. Mamia ya mamilioni ya wanakanisa wayo, ikiwa wao wataendelea kuunga mkono dini ya Jumuiya ya Wakristo, wanakuwa kama mabapa ya nyasi yaliyounguzwa moto, wamenyauka kiroho katika macho ya Yehova.—Linga Zaburi 37:1, 2.a
18. Ujumbe wa hukumu ya Yehova ulipigiwaje mbiu kwenye mkusanyiko wa 1922 katika Sida Pointi, Ohaiyo?
18 Ujumbe huu wa hukumu unapelekwaje? Kwa kawaida, si kupitia vyombo vya habari, ambavyo ni sehemu ya ulimwengu na mara nyingi husuta “mtumwa” wa Mungu. (Mathayo 24:45) Ulipelekwa kwa njia yenye kujulikana kwenye mkutano wa pili wenye kufanyiza historia wa watu wa Mungu katika Sida Pointi, Ohaiyo, Septemba 10, 1922. Kwa umoja na kwa idili hawa walikubali azimio lililokuwa na kichwa “Sai kwa Waongoza Ulimwengu.” Katika semi zilizo wazi, lilijulisha “dunia” ya ufananisho ya ki-siku-hizi, kama ifuatavyo: “Kwa hiyo sisi tunayaomba mataifa ya dunia, watawala na viongozi wayo, na viongozi wa kidini wote wa migawanyiko yote ya makanisa ya dunia, wafuasi wayo na wafungamani, biashara kubwa-kubwa na wanasiasa wakubwa-wakubwa, watokeze ushahidi katika kuthibitisha msimamo waliouchukua kwamba wao wanaweza kusimamisha amani na ufanisi duniani na kuleta furaha kwa watu; na wakishindwa katika hili, sisi tunawaomba wategee sikio ushahidi ambao sisi tunatoa tukiwa mashahidi kwa ajili ya Bwana, na kisha acheni wao waseme kama ushahidi wetu ni wa kweli au sivyo.”
19. Ni ushahidi gani ambao watu wa Mungu walipelekea Jumuiya ya Wakristo kuhusu Ufalme wa Mungu?
19 Mashahidi hawa walitoa ushahidi gani? Huu: “Sisi tunashikilia na twajulisha kwamba ufalme wa Mesiya ndio ponyo kamili kwa taabu zote za aina ya binadamu nao utaleta amani duniani na nia njema kwa watu, ile tamaa ya mataifa yote; kwamba wale wanaojitoa kwa moyo wa kupenda kwa utawala wake wa uadilifu [ambao] sasa umeanza watabarikiwa kwa amani ya kudumu, uhai, uhuru na furaha isiyokwisha.” Katika nyakati hizi zenye ufisadi, wakati serikali zilizofanywa na binadamu, hasa katika Jumuiya ya Wakristo, zinashindwa kabisa kutatua magumu ya siku hizi, dai hilo la ithibati lenye kupigiwa tarumbeta lina mlio ulio na kani kubwa hata zaidi ya ulivyokuwa katika 1922. Jinsi ilivyo kweli kwamba Ufalme wa Mungu ulio mikononi mwa Kristo wake mwenye kushinda ndio tumaini moja tu na la pekee la aina ya binadamu!
20. (a) Ni kwa njia gani jumbe za hukumu katika 1922 na baada ya hapo zimepigiwa tarumbeta na kundi la Wakristo wapakwa-mafuta? (b) Tokeo lilikuwa nini kwa Jumuiya ya Wakristo kutokana na mpigo wa kwanza wa tarumbeta?
20 Kupitia maazimio, trakti, vijitabu, vitabu, magazeti, na hotuba, mbiu hii na za baadaye zilipigiwa tarumbeta kwa njia ya kundi la Wakristo wapakwa-mafuta. Tokeo la mpigo wa tarumbeta ya kwanza lilikuwa kana kwamba Jumuiya ya Wakristo imepigwa kwa maji yaliyogandamana ya mvua-mawe inayotwanga. Hatia yayo ya damu, kwa sababu ya kushiriki katika vita vya karne ya 20, imefunuliwa, nayo imeonyeshwa kuwa inastahili wonyesho wenye moto wa hasira-kisasi ya Yehova. Jamii ya Yohana, ikiungwa mkono baadaye na “umati mkubwa,” imeendelea kurudisha mwangwi wa mpigo wa tarumbeta ya kwanza, ikivuta uangalifu kwenye oni la Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo, kuwa inastahili uharibifu.—Ufunuo 7:9, 15.
Kama Mlima Unaowaka Moto
21. Kunakuwa nini wakati malaika wa pili anapopuliza tarumbeta yake?
21 “Na malaika wa pili akapuliza tarumbeta yake. Na kitu fulani kama mlima mkubwa unaowaka moto kilivurumishwa ndani ya bahari. Na theluthi moja ya bahari ikawa damu; na theluthi moja ya viumbe ambao wamo ndani ya bahari ambao wana nafsi wakafa, na theluthi moja ya mashua zikaharibiwa.” (Ufunuo 8:8, 9, NW) Mandhari hii yenye kuogopesha inatoa picha ya nini?
22, 23. (a) Ni azimio gani lililokuja bila shaka likiwa tokeo la kuvumishwa kwa tarumbeta ya pili? (b) Ni nini kinachowakilishwa na “theluthi moja ya bahari”?
22 Sisi tunaweza kuielewa vizuri juu ya msingi wa ule mkusanyiko wa watu wa Yehova uliofanyiwa Los Angeles, Kalifornia, U.S.A., Agosti 18-26, 1923. Hotuba maalumu alasiri ya Jumamosi iliyotolewa na J. F. Rutherford ilikuwa juu ya kichwa “Kondoo na Mbuzi.” “Kondoo” walitambulishwa waziwazi kuwa wale watu wenye mwelekeo wa uadilifu ambao watarithi milki ya kidunia ya Ufalme wa Mungu. Azimio ambalo lilifuata lilivuta fikira kwenye unafiki wa “viongozi wa kidini waasi-imani na ‘wakuu wa makundi yao,’ ambao ni watu walimwengu wenye mavutano makubwa ya kifedha na kisiasa.” Iliomba ule “umayamaya wa wenye kupenda amani na utaratibu walio katika migawanyiko ya makanisa . . . kujiondoa wenyewe kutoka mifumo hiyo ya kieklesia yenye utovu wa adili ambayo imeitwa na Bwana kuwa ‘Babuloni’” na wajiweke tayari wenyewe “kupokea baraka za ufalme wa Mungu.”
23 Pasipo shaka, azimio hili lilikuja likiwa tokeo la kuvumishwa kwa tarumbeta ya pili. Wale ambao baada ya kupita wakati wangeitikia ujumbe huo wangejitenga na wale ambao Isaya alisema hivi kuwahusu: “Lakini waovu ni kama bahari ambayo inarushwarushwa, wakati inapokuwa haiwezi kutulia, maji yayo ambayo huendelea kurusharusha juu magugubahari na topetope.” (Isaya 57:20; 17:12, 13, NW) Hivyo, “bahari” hutoa vizuri picha ya binadamu wasiopumzika, wasiotulia, na wenye uasi wanaochochea kutopumzika na mapinduzi. (Linga Ufunuo 13:1.) Utakuja wakati ambapo hiyo “bahari” itakuwa haipo tena. (Ufunuo 21:1) Lakini kwa wakati uliopo, kwa mpigo wa tarumbeta ya pili, Yehova anatamka hukumu dhidi ya “theluthi moja” yayo—ile sehemu yenye utukutu iliyo katika milki ya Jumuiya ya Wakristo yenyewe.
24. Ni nini kinachotolewa picha na lile tungamo lililo kama mlima unaowaka moto lililovurumishwa ndani ya “bahari”?
24 Tungamo moja kubwa lililo kama mlima unaowaka moto lavurumishwa ndani ya “bahari” hii. Katika Biblia, mara nyingi sana milima hufananisha serikali. Mathalani, Ufalme wa Mungu unaonyeshwa kuwa kama mlima. (Danieli 2:35, 44) Babuloni yenye kuharibu ilipata kuwa ‘mlima ulioteketea.’ (Yeremia 51:25, NW) Lakini tungamo la mlima ambalo Yohana anaona lingali likiwaka moto. Kuvurumishwa kwalo ndani ya “bahari” kunawakilisha vizuri jinsi, wakati wa na baada ya vita ya kwanza ya ulimwengu, swali linalohusu serikali lilipata kuwa suala lenye kuwaka moto miongoni mwa aina ya binadamu, hasa katika yale mabara ya Jumuiya ya Wakristo. Katika Italia, Mussolini aliingiza Ufashisti. Ujeremani ilikubali Unazi wa Hitla, hali nchi nyinginezo zilijaribu namna mbalimbali za usoshalisti (ujamaa). Badiliko kubwa lilitukia katika Urusi, ambako pinduzi la Bolsheviki lilitokeza serikali ya kwanza ya Ukomunisti, kukiwa na tokeo la kwamba viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipoteza nguvu na uvutano wao katika ile ambayo hapo kwanza ilikuwa mojapo ngome zao kubwa.
25. Serikali iliendeleaje kuwa suala lenye kuwaka baada ya Vita ya Ulimwengu 2?
25 Majaribio ya Ufashisti na Unazi yalizimwa na vita ya pili ya ulimwengu, lakini serikali iliendelea kuwa suala lenye moto, nayo bahari ya kibinadamu iliendelea kusukasuka na kutupa juu serikali mpya za kimapinduzi. Katika ile miongo iliyofuata 1945, hizi ziliwekwa katika mahali kwingi, kama vile China, Vietnamu, Kyuba, na Nikaragua. Katika Ugiriki, jaribio katika serikali ya udikteta wa kijeshi lilishindwa. Katika Kampuchea (Kambodia), jaribio dogo katika Ukomunisti wa ufandamentalisti ulitokeza vifo vinavyoripotiwa kuwa milioni mbili na zaidi.
26. ‘Mlima unaowaka moto’ uliendeleaje kufanyiza mawimbi katika bahari ya aina ya binadamu?
26 Huo ‘mlima unaowaka moto’ uliendelea kufanyiza mawimbi katika bahari ya aina ya binadamu. Ming’ang’ano juu ya serikali imeripotiwa katika Afrika, mabara ya Amerika, Esia, na visiwa vya Pasifiki. Ni jambo linalostahili kuangaliwa kwamba mingi ya ming’ang’ano hii imetukia katika yale mabara ya Jumuiya ya Wakristo au mahali ambako wamisionari wa Jumuiya ya Wakristo wamekuwa wanaharakati wa kisiasa. Mapadri wa Roma Katoliki hata walijiunga na wakapiga vita wakiwa wanachama wa vikosi vya Kikomunisti vya wavamizi wa kupigania Ukomunisti. Wakati uo huo vikundi vya evanjeli ya Kiprotestanti vilifanya kazi katika Amerika ya Kati ili kubadili walichokiita “tamaa mbaya sana na yenye ukatili kwa ajili ya nguvu.” Lakini hakuna yoyote ya misukosuko hii katika “bahari” ya aina ya binadamu imeleta amani na usalama.—Linga Isaya 25:10-12; 1 Wathesalonike 5:3.
27. (a) “Theluthi moja ya bahari” imekuwaje kama damu? (b) ‘Theluthi moja ya viumbe katika bahari’ walikufaje na itakuwaje kwa “theluthi moja ya mashua”?
27 Ule mpigo wa pili wa tarumbeta hufunua kwamba wale wa aina ya binadamu ambao walijihusisha katika mipambano ya kimapinduzi juu ya serikali badala ya kujitiisha kwenye Ufalme wa Mungu ni wenye hatia ya damu. Hasa “theluthi ya bahari” ya Jumuiya ya Wakristo imekuwa kama damu. Vitu vyote vilivyo hai humo ni vifu machoni pa Mungu. Hakuna yoyote ya yale matengenezo ya kisoshalisti yanayoelea kama mashua katika theluthi hiyo ya bahari yanaweza kuepuka mvunjikomeli wa mwisho kabisa. Jinsi sisi tulivyo wenye furaha kwamba mamilioni ya watu wenye mfano wa kondoo sasa wametii mwito kama wa tarumbeta wajitenge na wale ambao wangali wanagaagaa katika utukuzo wa taifa usio na akili na hatia ya damu ya bahari hiyo!
Nyota Yaanguka Kutoka Mbinguni
28. Kunakuwa nini wakati malaika wa tatu anapopuliza tarumbeta yake?
28 “Na malaika wa tatu akapuliza tarumbeta yake. Na nyota kubwa yenye kuwaka kama taa ikaanguka kutoka mbinguni, na ikaanguka juu ya theluthi moja ya mito na juu ya vibubujiko vya maji. Na jina la nyota linaitwa Pakanga. Na theluthi ya maji ikageuka kuwa pakanga, na wengi wa wanadamu wakafa kwa hayo maji, kwa sababu haya yalikuwa yamefanywa kuwa machungu.” (Ufunuo 8:10, 11, NW) Hapa tena, sehemu nyingine za Biblia hutusaidia kujua jinsi andiko hili linavyotumika katika siku ya Bwana.
29. Ni nini kinachotimiza mfananisho wa “nyota kubwa yenye kuwaka kama taa,” na kwa nini?
29 Sisi tumekwisha kutana na mfananisho wa nyota katika jumbe za Yesu kwa yale makundi saba, ambazo katika hizo zile nyota saba hufananisha wale wazee katika makundi.b (Ufunuo 1:20) “Nyota” zilizopakwa mafuta, pamoja na wengine wote wa wapakwa-mafuta, wanakaa katika mahali pa kimbingu katika maana ya kiroho kutoka wakati ambao wao wanatiwa muhuri kwa roho takatifu hiyo ikiwa dalili ya urithi wao wa kimbingu. (Waefeso 2:6, 7) Hata hivyo, mtume Paulo alionya kwamba kutoka miongoni mwa hao wenye mfano wa nyota wangekuja waasi-imani, wanafaraka, ambao wangeongoza kundi vibaya. (Matendo 20:29, 30) Utoaminifu kama huo ungetokeza uasi-imani mkubwa, na hao wazee walioanguka wangekuja kuwa jumuiya ya “mtu wa kuasi” ambaye angejiinua mwenyewe kwenye cheo kama cha Mungu miongoni mwa aina ya binadamu. (2 Wathesalonike 2:3, 4) Maonyo ya Paulo yalitimizwa wakati viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipotokea katika ulimwengu. Kikundi hiki kinawakilishwa vizuri na ule ufananisho wa “nyota moja kubwa ikiwaka kama taa.”
30. (a) Wakati mfalme wa Babuloni alipoambiwa ameanguka kutoka mbinguni, ni nini kilichomaanishwa? (b) Anguko kutoka mbinguni laweza kurejezea nini?
30 Yohana anaona nyota hii hususa ikianguka kutoka mbinguni. Jinsi gani? Yaliyompata mfalme mmoja wa kale hutusaidia sisi kuelewa. Akisema kwa mfalme wa Babuloni, nabii Isaya alisema: “O jinsi wewe umeanguka kutoka mbinguni, wewe mwenye kung’aa, mwana wa mapambazuko! Jinsi wewe umekatwa chini kwenye dunia, wewe ambaye ulikuwa ukiondoa uwezo wa mataifa!” (Isaya 14:12, NW) Unabii huu ulitimizwa wakati Babuloni ilipoangushwa na majeshi ya Sairasi, naye mfalme wayo akashuka ghafula kutoka utawala wa ulimwengu mpaka kwenye ushinde wenye kuaibisha. Hivyo, anguko kutoka mbinguni laweza kurejezea kupoteza cheo cha juu na kuanguka kwenye aibu.
31. (a) Ni lini viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipoanguka kutoka cheo cha “kimbingu”? (b) Maji ambayo viongozi wa kidini wanatoa yamegeukaje yakawa “pakanga,” na kukiwa na tokeo gani kwa wengi?
31 Wakati viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walipoasi Ukristo wa kweli, wao walianguka kutoka cheo kilichotukuka cha “kimbingu” kinachoelezwa na Paulo kwenye Waefeso 2:6, 7, NW. Badala ya kutoa maji safi ya ukweli, wao walitoa “pakanga,” uwongo mchungu kama vile moto wa mateso, pargatori, Utatu, na watu kuandikiwa kimbele mwisho wao; pia waliongoza mataifa kwenye vita, wakishindwa kuwajenga wawe watumishi waadilifu wa Mungu. Tokeo? Kusumishwa kiroho kwa wale walioitikadi uwongo huo. Kisa chao kilifanana na kile cha Waisraeli wasio waaminifu wa siku ya Yeremia, ambao kwao Yehova alisema: “Hapa mimi ninafanya wao kula pakanga, na mimi nitawapa maji yaliyosumishwa wanywe. Kwa kuwa kutoka manabii wa Yerusalemu uasi-imani umetoka na kwenda kwenye bara lote.”—Yeremia 9:15; 23:15, NW.
32. Ni lini anguko la Jumuiya ya Wakristo kutoka mbingu za kiroho lilipopata kuwa wazi, nalo lilionyeshwaje kama drama?
32 Anguko hili kutoka mbingu za kiroho lilionekana wazi katika mwaka 1919 wakati, badala ya viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, baki dogo la Wakristo wapakwa-mafuta waliwekwa rasmi juu ya masilahi ya Ufalme. (Mathayo 24:45-47) Na katika 1922 anguko hilo lilionyeshwa kama drama wakati kikundi hiki cha Wakristo kilipoanza upya kampeni yacho ya kufichua wazi kushindwa kwa viongozi wa Jumuiya ya Wakristo.
33. Ni mfichuo gani wa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo uliofanywa kwenye mkusanyiko wa 1924 katika Kolumbasi, Ohaiyo, U.S.A.?
33 Yenye kutokeza kuhusiana na hili ni ile mbiu iliyopigwa kwenye ule ambao gazeti The Golden Age liliueleza kuwa “mkusanyiko ulio mkubwa zaidi ya yote wa Wanafunzi wa Biblia uliofanywa wakati wa enzi zilizopita.” Mkusanyiko huu ulikusanyika katika Kolumbasi, Ohaiyo, Julai 20-27, 1924. Pasipo shaka kwa mwelekezo wa malaika ambaye alivumisha ile tarumbeta ya tatu, azimio lenye kujaa kani lilikubaliwa huko na baadaye nakala milioni 50 zikagawanywa zikiwa trakti. Lilitangazwa chini ya kichwa Viongozi wa Kidini Washtakiwa. Kichwa kidogo kilitoa suala hili: “Mbegu ya Ahadi Dhidi ya Mbegu ya Nyoka.” Shtaka lenyewe lilifichua waziwazi viongozi wa kidini juu ya mambo kama vile kujitwalia kwao wenyewe majina ya cheo ya kujiweka juu sana, kufanya kwao wanabiashara wakubwa-wakubwa na wanasiasa wa kulipwa kuwa ndio wakuu wa makundi yao, kutamani kwao kung’aa mbele ya watu, na kukataa kwao kuhubiria watu ujumbe wa Ufalme wa Mesiya. Lilikazia kwamba kila Mkristo aliye wakfu amepewa utume na Mungu atangaze “siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao.”—Isaya 61:2.
34, 35. (a) Nguvu na uvutano wa viongozi wa kidini vimekuwaje tangu malaika wa tatu aanze kupuliza tarumbeta yake? (b) Wakati ujao una nini kwa ajili ya viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo?
34 Tangu malaika wa tatu aanze kupuliza tarumbeta yake, cheo cha viongozi wa kidini cha utawala miongoni mwa aina ya binadamu kimekuwa kikichurupuka mpaka, leo hii na zamani hizi, ni wachache sana kati yao ambao wangali wana nguvu kama za mungu walizofurahia katika karne zilizopita. Kwa sababu ya Mashahidi wa Yehova kuhubiri, idadi kubwa-kubwa za watu wamekuja kung’amua kwamba mafundisho mengi ya kidini wanayofundisha viongozi wa kidini ni sumu ya kiroho—“pakanga.” Zaidi ya hilo, katika Ulaya kaskazini nguvu ya viongozi wa kidini inakaribia sana kwisha, huku katika mabara mengine, serikali inapunguza sana uvutano wao. Katika Ulaya ya Kikatoliki na katika mabara ya Amerika mwenendo wa aibu wa viongozi wa kidini katika mambo ya kifedha, kisiasa, na kiadili umechafua sifa yao. Tokea sasa na kuendelea, hali yao inaweza kuzidi tu kuwa mbaya, kwa maana karibuni watapatwa na kile kile kitakachopata wanadini bandia wengine wote.—Ufunuo 18:21; 19:2.
35 Yehova hajamaliza bado kupiga Jumuiya ya Wakristo kwa tauni. Fikiria kinachokuwa baada ya mpigo wa nne wa tarumbeta.
Giza!
36. Baada ya malaika wa nne kupuliza tarumbeta yake kunakuwa nini?
36 “Na malaika wa nne akapuliza tarumbeta yake. Na theluthi moja ya jua ikapigwa na theluthi moja ya mwezi na theluthi moja ya nyota, ili kwamba theluthi yazo ipate kutiwa giza na mchana usipate mmuliko kwa theluthi moja yao, na usiku vivyo hivyo.” (Ufunuo 8:12, NW) Tauni ya tisa juu ya Misri ilikuwa tauni ya giza halisi. (Kutoka 10:21-29) Lakini ni nini giza hili la mfano ambalo linakuja kusumbua watu?
37. Mitume Petro na Paulo waliielezaje habari ya hali ya kiroho ya wale walio nje ya kundi la Kikristo?
37 Mtume Petro aliambia waamini wenzake kwamba walikuwa wamekuwa katika giza, kusema kiroho, kabla ya wao kuwa Wakristo. (1 Petro 2:9) Vilevile Paulo alitumia neno “giza” kueleza hali ya kiroho ya wale walio nje ya kundi la Kikristo. (Waefeso 5:8; 6:12; Wakolosai 1:13; 1 Wathesalonike 5:4, 5) Lakini namna gani wale walio katika Jumuiya ya Wakristo ambao hudai kuitikadi katika Mungu na ambao husema wao wanamkubali Yesu kuwa Mwokozi wao?
38. Malaika wa nne hupiga tarumbeta ya uhakika gani juu ya “nuru” ya Jumuiya ya Wakristo?
38 Yesu alisema kwamba Wakristo wa kweli wangejulikana kwa matunda yao na kwamba wengi wenye kudai kuwa wafuasi wake wangekuwa “wafanya kazi wa uasi-sheria.” (Mathayo 7:15-23, NW) Hakuna mmoja anayetazama matunda ya “theluthi” ya ulimwengu inayokaliwa na Jumuiya ya Wakristo anaweza kukana kwamba hiyo haipapasipapasi katika giza kubwa la kiroho. (2 Wakorintho 4:4) Inastahili sana lawama, kwa kuwa hiyo inadai kuwa ya Kikristo. Kwa sababu hiyo, inafaa sana malaika wa nne apige tarumbeta ya uhakika wa kwamba “nuru” ya Jumuiya ya Wakristo, kwa kweli, ni giza, na kwamba vyanzo vya “nuru” yayo ni vya Kibabuloni—visivyo vya Kikristo.—Marko 13:22, 23; 2 Timotheo 4:3, 4.
39. (a) Azimio lililokubaliwa kwenye mkusanyiko katika 1925 lilielezaje nuru bandia ya Jumuiya ya Wakristo? (b) Ni mfichuo gani mwingine uliofanywa katika 1955?
39 Kupatana na mbiu hiyo ya kimbingu, halaiki ya watu wa Mungu, walikusanyika katika mkusanyiko katika Indianapolis, Indiana, U.S.A., Agosti 29, 1925, na wakakubali lichapwe azimio lenye kusema mambo wazi likiwa na kichwa “Ujumbe wa Tumaini.” Kwa mara nyingine tena, nakala milioni 50 zilienezwa katika lugha kadhaa. Lilieleza kwamba kwa sababu ya nuru bandia inayotolewa na muungano wa wachumaji-faida wa kibiashara, viongozi wa kisiasa, na viongozi wa kidini, “vikundi vya watu vimeanguka ndani ya giza.” Nalo lilielekeza kwenye Ufalme wa Mungu kuwa ndio tumaini halisi kwa ajili ya kupokea “baraka za amani, ufanisi, afya, na uhai, uhuru na furaha ya milele.” Ilihitaji ushujaa kwa kikosi kidogo cha Wakristo wapakwa-mafuta kupiga mbiu ya jumbe kama hizo dhidi ya tengenezo kubwa mno la Jumuiya ya Wakristo. Lakini bila ugeugeu kutoka miaka ya mapema ya 1920 mpaka sasa, wamefanya hivyo. Katika nyakati za majuzi zaidi, katika 1955, kufichuliwa zaidi kwa jamii ya viongozi wa kidini kulifanywa na ugawanyaji wa ulimwenguni pote katika lugha nyingi wa kijitabu chenye kichwa Jumuiya ya Wakristo au Ukristo—Ni Kipi Kilicho “Nuru ya Ulimwengu”? Leo, unafiki wa Jumuiya ya Wakristo umekuwa wazi sana hivi kwamba wengi katika ulimwengu wanaweza kujionea wenyewe. Lakini watu wa Yehova hawajaacha kuifichua kuonyesha ilivyo hasa: ufalme wa giza.
Tai Anayeruka
40. Ile mipigo minne ya tarumbeta ilionyesha Jumuiya ya Wakristo kuwa nini?
40 Mipigo minne hii ya tarumbeta ilitokeza kugubuliwa kikweli kwa hali yenye ukiwa na yenye kuleta kifo ya Jumuiya ya Wakristo. Sehemu yayo ya “dunia” ilifichuliwa kuwa inastahili kupokea hukumu za Yehova. Serikali za kimapinduzi zilizozuka katika mabara yayo na kwingineko zilionyeshwa kuwa zenye kudhuru uhai wa kiroho. Ile hali iliyoanguka ya viongozi wa kidini wayo ililazwa wazi, na lile giza lote la hali yayo ya kiroho lilifichuliwa wote waone. Kwa kweli Jumuiya ya Wakristo ndiyo sehemu yenye kulaumika zaidi sana ya mfumo wa mambo wa Shetani.
41. Wakati wa kituo katika mfululizo wa mipigo ya tarumbeta, Yohana anaona na kusikia nini?
41 Kuna nini zaidi cha kufunua? Kabla ya kupata jibu kwa swali hili, kuna kituo kifupi katika mfululizo wa mipigo ya tarumbeta. Yohana anaeleza kile anachofuata kuona: “Na mimi nikaona, na mimi nikasikia tai mmoja akiruka katikati ya mbingu akisema kwa sauti kubwa: ‘Ole, ole, ole, kwa wale wanaokaa juu ya dunia kwa sababu ya mipigo inayobaki ya tarumbeta ya malaika watatu ambao wako karibu kupuliza tarumbeta zao!’”—Ufunuo 8:13, NW.
42. Ni nini linaloashiriwa na tai anayeruka na ujumbe wake ni upi?
42 Tai huruka juu katika anga, hivi kwamba watu katika eneo pana wanaweza kumwona. Ana mwono mkali isivyo kawaida naye anaweza kuona mbali sana na mahali alipo. (Ayubu 39:29) Mmoja wa viumbe wanne wenye uhai wa kimakerubi kuzunguka kiti cha ufalme cha Yehova alionyeshwa kwa picha ya tai anayeruka. (Ufunuo 4:6, 7) Awe ni kerubi huyu au ni mtumishi mwingine wa Mungu mwenye kuona mbali, yeye anapiga kwa sauti kubwa mbiu ya ujumbe wenye nguvu-msukumo: “Ole, ole, ole”! Acheni wakaaji wa dunia waangalie, wakati ile mipigo mitatu inayobaki ya tarumbeta inaposikiwa, kila mmoja wayo ukiwa unafungamanishwa na mmoja wa ole hizi.
[Maelezo ya Chini]
a Kwa kutofautisha, Ufunuo 7:16 huonyesha kwamba “umati mkubwa” hawapatwi na joto lenye kuunguza la kukosa kibali cha Yehova.
b Ingawa nyota saba katika mkono wa kulia wa Yesu ni picha ya waangalizi waliopakwa mafuta katika kundi la Kikristo, walio wazee katika makundi 100,000 hivi katika ulimwengu leo ni wale wa umati mkubwa. (Ufunuo 1:16; 7:9) Cheo chao ni nini? Kwa kuwa wao hupokea kuwekwa kwao kwa njia ya roho takatifu kupitia jamii iliyopakwa mafuta ya mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu, hawa wanaweza kusemwa kuwa wako chini ya mkono wa kulia wenye udhibiti wa Yesu kwani wao pia ni wachungaji walio chini yake. (Isaya 61:5, 6; Matendo 20:28) Wao huunga mkono “nyota saba” katika maana ya kwamba wao hutumikia mahali ambako ndugu waliopakwa mafuta wenye kustahili hawapatikani.
-
-
Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya WakristoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 139]
Maji ya Jumuiya ya Wakristo Yafunuliwa Kuwa Pakanga
Itikadi na Mielekeo ya Yanayosemwa
Jumuiya ya Wakristo Hasa na Biblia
Jina la kibinafsi la Mungu Yesu alisali jina la Mungu
si la maana: “Utumizi wa jina litakaswe. Petro alisema:
la pekee lolote kwa ajili ya “Kila mmoja ambaye huita
Mungu mmoja tu . . . haufai juu ya jina la Yehova
kabisa kwa imani ya ulimwengu ataokolewa.” (Matendo 2:21;
wote mzima ya Kanisa la Kikristo.” Yoeli 2:32; Mathayo 6:9, NW;
(Dibaji ya Revised Standard Version) Kutoka 6:3; Ufunuo 4:11;
15:3; 19:6)
Mungu ni Utatu: “Baba ni Biblia husema Yehova ni mkuu
Mungu, Mwana ni Mungu, kuliko Yesu naye ni Mungu
na Roho Mtakatifu ni Mungu, na kichwa cha Yesu.
na hata hivyo hakuna Miungu (Yohana 14:28; 20:17; 1 Wakorintho
watatu bali Mungu mmoja.” 11:3) Roho takatifu ni kani-
(The Catholic Encyclopedia, tendaji ya Mungu. (Mathayo 3:11;
chapa ya 1912) Luka 1:41; Matendo 2:4)
Nafsi ya kibinadamu ni Mtu ni nafsi. Wakati
isiyoweza kufa: “Mtu anapokufa wa kifo nafsi huacha kufikiri
nafsi na mwili wake hutengana. au kuhisi na hurudia mavumbi
Mwili wake . . . huoza . . . ambayo kwayo ilifanyizwa.
Lakini nafsi ya kibinadamu, haifi.” (Mwanzo 2:7, 3:19; Zaburi
(What Happens After Death, 146:3, 4; Mhubiri 3:19, 20;
kichapo cha Roma Katoliki) 9:5, 10; Ezekieli 18:4, 20, ZSB)
Waovu huadhibiwa baada ya Mshahara wa dhambi ni kifo,
kufa katika hell: “Kulingana si uhai katika mateso makali.
na itikadi ya Kikristo ya (Warumi 6:23) Wafu hupumzika
kimapokeo, hell ni mahali pa katika kaburi (Hadesi, Sheoli)
mateso makali na maumivu.” bila fahamu, wakingojea ufufuo.
(The World Book Encyclopedia, (Zaburi 89:48; Yohana 5:28, 29;
chapa ya 1987) 11:24, 25; Ufunuo 20:13, 14)
“Jina la cheo Mediatriksi Mpatanishi pekee kati ya
[mpatanishi wa kike] linatumika Mungu na wanadamu ni Yesu.
kuhusu [Mama Yetu].” (New (Yohana 14:6; 1 Timotheo 2:5;
Catholic Encyclopedia, Waebrania 9:15; 12:24)
chapa ya 1967)
Yapasa vitoto vichanga Ubatizo ni wa wale ambao
vibatizwe: “Tangu mwanzo wamekwisha fanywa wanafunzi na
wenyewe Kanisa limevipa wamefundishwa kutii amri za
vitoto vichanga Sakramenti Yesu. Ili mtu astahili ubatizo
ya Ubatizo. Zoea hili ni lazima aelewe Neno la
halikuonwa kuwa halali Mungu na kujizoeza imani.
kisheria tu, bali pia (Mathayo 28:19, 20; Luka 3:21-23;
lilifundishwa kuwa la lazima Matendo 8:35, 36)
kabisa kwa ajili ya wokovu.”
(New Catholic Encyclopedia
chapa ya 1967)
Makanisa yaliyo mengi yame- Wakristo wa Kwanza wote
gawanywa kuwa jamii ya watu walikuwa wahudumu nao walishiriki
wasio na cheo na jamii ya kuhubiri habari njema. (Matendo
viongozi wa kanisa, ambao 2:17, 18; Warumi 10:10-13;
huhudumia watu wasio na cheo. Warumi 16:1) Mkristo apaswa
Kwa kawaida viongozi wa kidini ‘kutoa bure’ si kwa ajili
hupewa mshahara kwa kubadili- ya mshahara. (Mathayo 10:7, 8)
shana na huduma yao na wanatu- Yesu alikataza katakata utumizi
kuzwa juu ya hao watu wasio wa majina ya cheo ya kidini.
na cheo kwa majina ya cheo kama (Mathayo 6:2; 23:2-12;
vile “Reverendi,” “Baba,” “Msifiwa.” 1 Petro 5:1-3)
Mifano, maaikoni, na misalaba, Lazima Wakristo wakimbie kila
hutumiwa katika ibada: ‘Mifano namna ya ibada ya sanamu,
ya Kristo, ya Bikira Mama ya kutia na ile inayoitwa eti
Mungu, na ya watakatifu wengine, ibada ya husiano. (Kutoka
yapasa . . . kutunzwa katika 20:4, 5; 1 Wakorintho 10:14;
makanisa na kupewa [staha kubwa] 1 Yohana 5:21) Wao huabudu
na heshima inayostahili. (Julisho-Wazi Mungu si kwa mwono bali
la Baraza la Trent [1545-63]) kwa roho na kweli. (Yohana
4:23, 24; 2 Wakorintho 5:7)
Washiriki wa Kanisa wanafundishwa Yesu alihubiri Ufalme wa
kwamba makusudi ya Mungu yata- Mungu, si mfumo fulani wa
timizwa kupitia siasa. Kardinali kisiasa, kuwa ndio tumaini
Spellman ambaye sasa amekufa kwa ajili ya aina ya binadamu.
alitaarifu hivi: “Kuna barabara (Mathayo 4:43; 6:9, 10)
moja tu ya kufikia amani . . . , Yeye alikataa kujihusisha
barabara kuu ya kidemokrasia.” katika siasa. (Yohana 6:14, 15)
Taarifa za habari huripoti juu ya Ufalme wake ulikuwa si sehemu
kujiingiza kwa dini katika siasa za ya ulimwengu huu; kwa sababu
ulimwengu (hata katika vitendo vya hiyo, wafuasi wake walipaswa
kufitini serikali) na uungaji-mkono wayo wawe si sehemu ya
wa UM kuwa “ndilo tumaini la mwisho ulimwengu. (Yohana 18:36;
la itifaki na amani.” 17:16) Yakobo alionya juu
ya urafiki na ulimwengu. (Yakobo 4:4)
-
-
Ole wa Kwanza—NzigeUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 22
Ole wa Kwanza—Nzige
1. Ni nani hufuatisha wakati malaika wanapovumisha mipigo ya tarumbeta zao, na ule mpigo wa tarumbeta ya tano hutangaza nini?
MALAIKA wa tano anajitayarisha kupuliza tarumbeta yake. Tayari tarumbeta nne za kimbingu zimevumishwa, na tauni nne zimekwisha elekezwa kwenye ile theluthi ya dunia ambayo Yehova anaona kuwa yenye kulaumika zaidi—Jumuiya ya Wakristo. Hali yayo yenye ugonjwa wa kufisha imekwisha gubuliwa. Wakati malaika wanapovumisha mipigo ya tarumbeta, watoa habari wa kibinadamu hufuatia duniani. Sasa tarumbeta ya tano ya kimalaika inakaribia kutangaza ole wa tano, wenye kuhofisha hata zaidi ya zile zilizotangulia. Unahusiana na tauni yenye kutisha ya nzige. Ingawa hivyo, kwanza acheni tuchunguze maandiko mengine ambayo yatatusaidia kuelewa tauni hii vizuri zaidi.
2. Ni kitabu kipi cha Biblia kinachoeleza tauni ya nzige inayofanana na ile ambayo Yohana anaona, na tokeo layo lilikuwa nini juu ya Waisraeli wa kale?
2 Kitabu cha Biblia cha Yoeli, kilichoandikwa wakati wa karne ya tisa K.W.K., kinaeleza habari ya tauni fulani ya wadudu, kutia na nzige, inayofanana na ile ambayo Yohana anaona. (Yoeli 2:1-11, 25)a Ilikusudiwa isumbue sana Israeli mwasi-imani lakini pia ingetokeza toba kwa Waisraeli mmoja mmoja na kurudi kwenye kibali cha Yehova. (Yoeli 2:6, 12-14) Wakati huo uwasilipo, Yehova angemimina roho yake juu ya “kila aina ya mnofu,” huku ishara zenye kutia hofu na maajabu yenye kushtua yangetangulia “kuja kwa ile siku kuu na yenye kuvuvia hofu ya Yehova.”—Yoeli 2:11, 28-32, NW.
Tauni ya Karne ya Kwanza
3, 4. (a) Ni wakati gani kulipokuwa na utimizo wa Yoeli sura ya 2, na jinsi gani? (b) Ni jinsi gani kulikuwako na tauni kama ya kundi la nzige katika karne ya kwanza W.K., tauni hiyo iliendelea kwa muda gani?
3 Kulikuwako utimizo wa Yoeli sura ya pili katika karne ya kwanza. Ilikuwa ndipo kwenye Pentekoste ya 33 W.K., roho takatifu ilipomiminwa, ikipaka mafuta Wakristo wa karne ya kwanza na kuwatia nguvu ili waseme “yale mambo matukufu ya Mungu” katika ndimi nyingi. Tokeo, umati mkubwa ulikusanyika. Mtume Petro alisema na watazamaji hawa waliokuwa wameshangaa, akidondoa Yoeli 2:28, 29 na kueleza kwamba wao walikuwa wakishuhudia utimizo wao. (Matendo 2:1-21, NW) Lakini hakuna maandishi yanayoonyesha kwamba walikuwako wadudu halisi wakati huo, wakisumbua baadhi yao na kuongoza wengine watubu.
4 Je! kulikuwako tauni ya kitamathali wakati wa siku hizo? Ndiyo, kweli kweli! Ilikuja ikiwa tokeo la kazi isiyokoma ya kuhubiri ya Wakristo hao waliokuwa ndipo tu wametoka kupakwa mafuta.b Kupitia wao, Yehova alialika wale Wayahudi ambao wangesikiliza watubu na kufurahia baraka kutoka kwake. (Matendo 2:38-40; 3:19) Watu mmoja mmoja ambao waliitikia walipokea kibali chake kwa kadiri yenye kutazamisha. Lakini kwa waliokataa mwaliko huo, wale Wakristo wa kwanza walikuwa kama kundi la nzige lenye kukumba. Wakianzia Yerusalemu, walisambaa Yudea yote na Samaria. Upesi walikuwa kila mahali, wakitesa-tesa Wayahudi wasioitikadi kwa kupiga peupe mbiu ya ufufuo wa Yesu, pamoja na yote ambayo huo ulimaanisha. (Matendo 1:8; 4:18-20; 5:17-21, 28, 29, 40-42; 17:5, 6; 21:27-30) Tauni hiyo iliendelea mpaka “siku yenye kuvuvia hofu,” katika 70 W.K., wakati Yehova alipoleta majeshi ya Roma dhidi ya Yerusalemu kuliangamiza. Wakristo wale tu ambao kwa imani waliita juu ya jina la Yehova ndio waliookolewa.—Yoeli 2:32; Matendo 2:20, 21; Mithali 18:10, NW.
Tauni ya Nzige Leo
5. Unabii wa Yoeli umekuwaje na utimizo tangu 1919?
5 Kupatana na kuwaza kuzuri, sisi tungetarajia unabii wa Yoeli uwe na utimizo kamili katika wakati wa mwisho. Na ndivyo imekuwa! Kwenye mkusanyiko wa Wanafunzi wa Biblia katika Sida Pointi Ohaiyo, U.S.A., Septemba 1-8, 1919, mmimino wa roho ya Yehova unaostahili kuangaliwa uliwatendesha watu wake wapange kitengenezo tena kampeni ya pote katika tufe ya kuhubiri. Kati ya wote waliodai kuwa Wakristo, wao pekee ndio waliotambua kwamba Yesu alikuwa ameketishwa katika kiti cha ufalme akiwa Mfalme wa kimbingu katika 1914, nao walitumia jitihada yote katika kutangaza kotekote hizo habari njema. Kutoa ushuhuda kwao kusikokoma kukawa tauni yenye kutesa kwa Jumuiya ya Wakristo yenye kuasi imani.—Mathayo 24:3-8, 14; Matendo 1:8.
6. (a) Yohana aliona nini wakati malaika wa tano alipopuliza tarumbeta yake? (b) “Nyota” hii inafananisha nani, na kwa nini?
6 Ufunuo, ulioandikwa miaka yapata 26 baada ya uharibifu wa Yerusalemu, hueleza pia habari ya tauni hiyo. Unaongezea nini elezo la unabii wa Yoeli? Acheni sisi tuchukue maandishi, kama Yohana anavyoripoti: “Na malaika wa tano akapuliza tarumbeta yake. Na mimi nikaona nyota moja ambayo ilikuwa imeanguka kwenye dunia kutoka mbinguni, na ufunguo wa shimo la abiso akapewa yeye.” (Ufunuo 9:1, NW) “Nyota” hii ni tofauti na ile ya Ufunuo 8:10 ambayo Yohana aliona ikiwa katika tendo la kuanguka. Yeye anaona “nyota ambayo ilikuwa imeanguka kutoka mbinguni” na ambayo sasa ina mgawo kwa habari ya dunia hii. Je! hii ni mtu wa roho au wa mnofu? Mshikaji wa huu “ufunguo wa shimo la abiso” anaelezwa habari zake baadaye kuwa akivurumisha Shetani ndani ya “abiso.” (Ufunuo 20:1-3, NW) Yeye lazima awe mtu wa roho mwenye nguvu. Kwenye Ufunuo 9:11, Yohana anatuambia kwamba hao nzige wana “mfalme, malaika wa abiso.” Mistari yote miwili lazima iwe inaelekeza kwa mtu yule yule mmoja, kwa maana yule malaika anayeshika ule ufunguo wa abiso kimantiki angekuwa malaika wa abiso. Na hiyo nyota lazima iwe ni ufananisho wa Mfalme aliyewekwa rasmi wa Yehova, kwa maana Wakristo wanakiri Mfalme mmoja tu wa kimalaika, Yesu Kristo.—Wakolosai 1:13; 1 Wakorintho 15:25.
7. (a) Kunakuwa nini “shimo la abiso” linapofunguliwa? (b) “Abiso” ni nini na ni nani waliotumia wakati mfupi ndani yayo?
7 Lile simulizi linaendelea: “Na yeye akafungua shimo la abiso, na moshi ukapaa kutoka shimo kama moshi wa tanuri kubwa, na jua likatiwa giza, pia hewa, kwa moshi wa shimo lile. Na katika moshi wakatoka nzige wakaenda juu ya dunia; na mamlaka walipewa wao, mamlaka ile ile kama ambayo nge wa dunia wanayo.” (Ufunuo 9:2, 3, NW) Kimaandiko, “abiso” ni mahali pa kutotenda, hata pa kifo. (Linga Warumi 10:7; Ufunuo 17:8; 20:1, 3.) Kikosi kidogo cha ndugu za Yesu kilitumia wakati mfupi katika “abiso” kama hiyo ya kutotenda kwa kadiri mwishoni mwa vita ya kwanza ya ulimwengu (1918-19). Lakini wakati Yehova alipomimina roho yake juu ya watumishi wake waliotubu katika 1919, wao walitoka wakiwa kundi wakabili tatizo la kazi iliyokuwa mbele.
8. Inakuwaje kwamba kuachiliwa kwa wale nzige kunaandamana na “moshi” mwingi?
8 Yohana anapotazama, kuachiliwa kwa nzige kunaandamana na moshi mwingi, kama “moshi wa tanuri kubwa.”c Ndivyo ilivyothibitika kuwa katika 1919. Hali ilikuwa yenye giza kwa Jumuiya ya Wakristo na kwa ulimwengu kwa ujumla. (Linga Yoeli 2:30, 31.) Kuachiliwa kwa hao nzige wa jamii ya Yohana kulikuwa ushinde kikweli kwa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, ambao walikuwa wametunga hila ya kuua kabisa kazi ya Ufalme na ambao sasa walikataa Ufalme wa Mungu. Ithibati ya giza lenye kufunika kama moshi ilianza kuenea juu ya Jumuiya ya Wakristo yenye kuasi imani wakati hicho kikosi cha nzige kilipopewa mamlaka na kikaanza kuitumia katika kupiga mbiu ya jumbe za hukumu zenye kujaa nguvu. “Jua” la Jumuiya ya Wakristo mwonekano wayo wa kuwa mtio-nuru—lilipatwa na giza, na “hewa” ikawa nzito kwa majulisho-wazi ya hukumu za kimungu wakati “mtawala wa mamlaka ya hewa” alipoonyeshwa kuwa ndiye mungu wa Jumuiya ya Wakristo.—Waefeso 2:2, NW; Yohana 12:31; 1 Yohana 5:19.
Nzige Hao Wenye Kutesa!
9. Ni maagizo gani ya pigano waliyopokea hao nzige?
9 Ni maagizo gani ya pigano waliyopokea hao nzige? Yohana anaripoti: “Na wao waliambiwa wasidhuru mmea wowote wa dunia wala kitu chochote cha chanikiwiti wala mti wowote, ila wale watu tu ambao hawana muhuri wa Mungu juu ya vipaji vya nyuso zao. Na hao nzige walipewa ruhusa, si kuua wao, bali kwamba hawa wapaswe kuteswa kwa miezi mitano, na mateso yaliyokuwa juu yao yalikuwa kama mateso ya nge wakati anapopiga mtu. Na katika siku hizo watu watatafuta kifo lakini hawatapata hicho, na wao watatamani kufa lakini kifo hufuliza kukimbia kutoka kwao.”—Ufunuo 9:4-6, NW.
10. (a) Tauni hiyo inaelekezwa kwa nani hasa, na kukiwa na tokeo gani kwao? (b) Ni mateso ya namna gani yanayohusika? (Ona pia kielezi cha chini.)
10 Angalia kwamba tauni hii haielekezwi kwanza kwa watu au wale mashuhuri miongoni mwao—ile ‘mimea na miti ya dunia.’ (Linga Ufunuo 8:7.) Nzige wapaswa kudhuru tu wale watu ambao hawana “muhuri wa Mungu juu ya vipaji vya nyuso zao,” wale katika Jumuiya ya Wakristo ambao hudai kuwa wametiwa muhuri lakini rekodi inaonyesha dai hilo kuwa la uwongo. (Waefeso 1:13, 14) Hivyo, matamko yenye kutesa ya nzige wa ki-siku-hizi yalielekezwa kwanza dhidi ya viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo. Ni lazima watu hawa wenye kujitanguliza wawe waliteseka kama nini waliposikia ikitangazwa peupe kwamba hawakuwa wakishindwa tu kuongoza makundi yao yaende mbinguni bali pia wao wenyewe hawangefika huko!d Kwa kweli, kimekuwa kisa cha ‘kipofu akiongoza kipofu’!—Mathayo 15:14.
11. (a) Nzige wanapewa mamlaka watese adui za Mungu kwa muda gani, na ni kwa nini kwa kweli huo si muda mfupi? (b) Mateso hayo ni makali kadiri gani?
11 Mateso huendelea kwa muda wa miezi mitano. Je! huo ni wakati mfupi kadiri hiyo? Si hivyo kwa maoni yanayohusu nzige halisi. Miezi mitano hueleza habari ya muda wa kawaida wa maisha halisi ya mmoja wa wadudu hawa. Kwa sababu hiyo, ingekuwa ni kadiri ya muda wa kuishi kwao kwamba nzige wa ki-siku-hizi wangeendelea kuchoma kwa uchungu adui za Mungu. Zaidi ya hilo, mateso ni makali sana hivi kwamba watu hutafuta kufa. Kweli, sisi hatuna rekodi kuonyesha kwamba wowote wa hao waliochomwa kwa uchungu na nzige kwa kweli walijaribu kujiua wenyewe. Lakini huo usemi husaidia sisi kupata picha ya ukali wa mateso—kana kwamba kwa shambulio lisilokoma la nge. Yako kama yale mateso yaliyotangulia kuonwa na Yeremia kwa Waisraeli wasioaminika ambao wangetawanywa na Wababuloni washindi na ambao kwao kifo kingependelewa kuliko uhai.—Yeremia 8:3; ona pia Mhubiri 4:2, 3.
12. Ni kwa nini nzige wanapewa ruhusa ya kutesa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo katika maana ya kiroho lakini si kuwaua?
12 Ni kwa nini, kusema kwa njia ya kiroho, ruhusa inapewa kutesa hao na si kuwaua? Huu ni ole wa kwanza katika kufichua uwongo wa Jumuiya ya Wakristo na kushindwa kwayo, lakini ni baadaye tu, kadiri siku ya Bwana iendeleavyo, ndipo hali yayo iliyo kama kifo inapotangazwa peupe kikamili. Itakuwa wakati wa ole wa pili ndipo theluthi ya watu wanauawa.—Ufunuo 1:10; 9:12, 18; 11:14.
Nzige Wapewa Vifaa kwa Ajili ya Pigano
13. Nzige wana mwonekano gani?
13 Lo! nzige hao wana mwonekano wa kutazamisha kama nini! Yohana anaeleza habari yao: “Na mifanano ya nzige ilishabihi farasi walio tayari kwa ajili ya pigano; na juu ya vichwa vyao palikuwa na kilichoonekana kuwa mataji kama dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu, lakini walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama yale ya masimba; na walikuwa na mabamba-kifua kama mabamba-kifua ya chuma. Na mvumo wa mabawa yao ulikuwa kama mvumo wa magari ya farasi wengi wenye kukimbia kuingia ndani ya pigano.”—Ufunuo 9:7-9, NW.
14. Ni kwa nini elezo la Yohana kuhusu hao nzige lilikifaa kile kikundi cha Wakristo waliohuishwa katika 1919?
14 Hii hutoa vizuri kielezi cha kikundi kishikamanifu cha Wakristo waliohuishwa katika 1919. Kama farasi, walikuwa tayari kwa ajili ya pigano, wakiwa na hamu nyingi ya kupigania ukweli katika njia aliyoeleza mtume Paulo. (Waefeso 6:11-13; 2 Wakorintho 10:4) Juu ya vichwa vyao Yohana huona kinachoonekana kuwa mataji kama ya dhahabu. Haingefaa wao kuwa na taji halisi kwa sababu wao hawaanzi kutawala wakati wangali duniani. (1 Wakorintho 4:8; Ufunuo 20:4) Lakini katika 1919 wao tayari walikuwa na mwonekano wa kifalme. Wao walikuwa ndugu za Mfalme, na mataji yao ya kimbingu walikuwa wamewekewa akiba maadamu wao wangeendelea kuwa waaminifu mpaka mwisho.—2 Timotheo 4:8; 1 Petro 5:4.
15. Ni jambo gani linalomaanishwa na (a) mabamba-kifua ya chuma ya hao nzige? (b) nyuso kama za wanadamu? (c) nywele kama za wanawake? (d) meno kama yale ya masimba? (e) kufanya kelele nyingi?
15 Katika njozi, hao nzige wana mabamba-kifua ya chuma, kufananisha uadilifu usiovunjika. (Waefeso 6:14-18) Pia wao wana nyuso kama za wanadamu, sura hii ikielekeza kwenye sifa ya upendo kwa kuwa mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu, ambaye ni upendo. (Mwanzo 1:26; 1 Yohana 4:16) Nywele zao ni ndefu kama za mwanamke, ambazo hutoa vizuri picha ya utii wao kwa Mfalme wao, “malaika wa abiso.” Na meno yao hushabihi meno ya simba. Simba hutumia meno yake kurarua nyama. Tangu 1919 na kuendelea, jamii ya Yohana imekuwa ikiweza kutwaa chakula kigumu cha kiroho, hasa zile kweli juu ya Ufalme wa Mungu unaotawalwa na “simba ambaye ni wa kabila la Yuda,” Yesu Kristo. Kama vile simba hufananisha ushujaa, ndivyo ushujaa mwingi umekuwa ukihitajiwa ili kuyeyusha tumboni huu ujumbe wenye kupiga sana, kuutia katika vichapo, na kuugawanya kuzunguka tufe lote. Nzige hao wa kitamathali wamefanyiza kelele nyingi, kama “mvumo wa magari ya farasi wengi wenye kukimbia kuingia ndani ya pigano.” Wakifuata kielelezo cha Wakristo wa karne ya kwanza, wao hawakusudii kukaa kimya.—1 Wakorintho 11:7-15; Ufunuo 5:5, NW.
16. Ni nini maana ya kwamba hao nzige walikuwa na “mikia na michomo kama nge”?
16 Kuhubiri huku hutia ndani zaidi ya neno la kunenwa tu! “Pia, wao wana mikia na michomo yenye uchungu kama nge; na katika mikia yao mna mamlaka yao kudhuru watu kwa miezi mitano.” (Ufunuo 9:10, NW) Hiyo ingeweza kumaanisha nini? Waendapo huku na huku katika kazi yao ya Ufalme, Mashahidi wa Yehova, kwa maneno na vichapo wanatoa taarifa zenye mamlaka zinazotegemea Neno la Mungu. Ujumbe wao una mchomo wenye uchungu kama wa nge kwa sababu huonya juu ya siku ya kisasi ya Mungu inayokaribia. (Isaya 61:2) Kabla ya hiki kizazi cha sasa cha nzige wa kiroho kumaliza muda wa uhai wacho, kazi yacho iliyoamuriwa kimungu ya kujulisha wazi hukumu za Yehova itakuwa imemalizika—kwa dhara la wakufuru wote wenye shingo ngumu.
17. (a) Ni nini kilichotangazwa kwenye mkusanyiko wa 1919 wa Wanafunzi wa Biblia ambacho kingeongeza mchomo mkali wenye uchungu wa kazi yao ya kutoa ushuhuda? (b) Viongozi wa kidini wameteswa-teswaje, nao walitendaje katika kuitikia?
17 Kikosi hicho cha nzige kilifurikwa na shangwe wakati gazeti jingine jipya, The Golden Age, lilipotangazwa kwenye mkusanyiko wao wa 1919. Lilikuwa gazeti lenye kutokea kila majuma mawili, lililokusudiwa kuongeza mchomo mkali wenye uchungu wa kazi yao ya kutoa ushuhuda.e Toleo lalo Na. 27, la Septemba 29, 1920, lilifunua udanganyifu wa viongozi wa kidini katika kunyanyasa Wanafunzi wa Biblia katika United States wakati wa kipindi cha 1918-19. Muda wote wa miaka ya 1920 na 1930, The Golden Age lilitesa-tesa viongozi wa kidini kwa makala zaidi zenye kuchoma kwa uchungu na kartuni ambazo zilifichua kugaagaa kwao kwa ujanja katika siasa, na hasa ile miafaka iliyofanywa na jamii ya mapadri wa Kikatoliki pamoja na madikteta wa Nazi na Ufashisti. Katika kuitikia, hao viongozi wa kidini ‘walitunga madhara kwa sheria’ na wakapanga vikundi vya wenye ghasia watumie jeuri juu ya watu wa Yehova.—Zaburi 94:20.
Watawala wa Ulimwengu Wataarifiwa
18. Ni kazi gani ambayo nzige walikuwa nayo kufanya, na ni nini kilichofuata katika kuitikia mpigo wa tarumbeta ya tano?
18 Nzige wa ki-siku-hizi walikuwa na kazi ya kufanya. Zile habari njema za Ufalme zilikuwa sharti zihubiriwe. Makosa yalikuwa sharti yafichuliwe. Kondoo waliopotea walikuwa sharti watafutwe. Wakati nzige walipokuwa wakienda huku na huku katika kazi zao hizi, ulimwengu ulilazimika kuamka na kujua jambo hilo. Katika kutii mipigo ya tarumbeta ya malaika, ile jamii ya Yohana imeendelea kuifichua Jumuiya ya Wakristo kuwa inastahili kupatwa na hukumu kali za Yehova. Katika kuitikia tarumbeta ya tano, upande fulani hasa wa hukumu hizi ulikaziwa kwenye mkusanyiko wa Wanafunzi wa Biblia katika London, Uingereza, Mei 25-31, 1926. Huo ulitoa azimio “Ushahidi kwa Watawala wa Ulimwengu,” na hotuba ya watu wote katika Royal Albert Hall juu ya “Sababu Serikali za Ulimwengu Zinaterereka—Kiponyi,” maandishi kamili ya haya yote mawili yalichapwa katika nyusipepa mbili kuu za London kesho yake. Baadaye, kile kikosi cha nzige kiligawa ulimwenguni pote nakala milioni 50 za azimio hilo zikiwa trakti—mateso kweli kweli kwa viongozi wa kidini! Miaka kadhaa baadaye, watu katika Uingereza walikuwa wangali wakisema juu ya mfichuo huo wenye kuchoma kwa uchungu.
19. Ni kifaa gani zaidi cha kupiga vita walichopokea hao nzige, nacho kilikuwa na jambo gani la kusema juu ya hati ya julisho-wazi la London?
19 Kwenye mkusanyiko huu, nzige walipokea kifaa kingine cha kutumia katika kupiga vita, kitabu kipya chenye kujulikana sana chenye kichwa Deliverance. Kilitia ndani mazungumzo ya Kimaandiko ya ile ishara kuthibitisha kwamba serikali ‘mtoto mwanamume,’ Ufalme wa kimbingu wa Kristo, ulikuwa umezaliwa katika 1914. (Mathayo 24:3-14; Ufunuo 12:1-10, NW) Baada ya hapo, kilidondoa kutoka julisho-wazi lililochapwa London katika 1917 na likatiwa sahihi na viongozi wa kidini wanane, walioelezwa habari zao kuwa “wamo miongoni mwa wahubiri walio mashuhuri zaidi sana ulimwenguni” na waliwakilisha migawanyiko mashuhuri zaidi ya Kiprotestanti—ya Kibaptisti, Kikongrigetionali, Kipresbeteri, Kiepiskopali, na Kimethodisti. Hata julisho-wazi hili lilipiga mbiu kwamba “hatari iliyopo sasa huelekeza kwenye kikomo cha majira ya Mataifa” na kwamba “ule ufunuo wa Bwana unaweza kutarajiwa dakika yo yote.” Ndiyo, hao viongozi wa kidini walikuwa wameitambua ishara ya kuwapo kwa Yesu! Lakini je! wao walitaka kufanya lolote juu yayo? Kile kitabu Deliverance hutupasha sisi habari hii: “Ile sehemu ya kutazamisha zaidi sana ya kisa hiki ni kwamba wanaume wale wale waliotia sahihi hati julisho-wazi baadaye walikataa katakata na wakakana ithibati ambayo inathibitisha kwamba sisi tuko kwenye mwisho wa ulimwengu na katika siku ya kuwapo kwa pili kwa Bwana.”
20. (a) Viongozi wa kidini wamefanya chaguo gani kwa habari ya kikosi cha nzige na Mfalme wao? (b) Ni nani ambaye Yohana husema yu juu ya hicho kikosi cha nzige, na jina lake ni gani?
20 Badala ya kuutangaza Ufalme wa Mungu unaokuja, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wamechagua kubaki na ulimwengu wa Shetani. Wao hawataki kuwa sehemu moja na kikosi cha nzige na Mfalme wao, ambao kwa habari yao Yohana anasema: “Wao wana mfalme juu yao, malaika wa abiso. Katika Kiebrania jina lake ni Abadoni [maana yalo “Uharibifu”], lakini katika Kigiriki yeye ana jina Apolioni [maana yalo “Mharabu,”].” (Ufunuo 9:11, NW) Akiwa “malaika wa abiso” na “Mharabu,” kwa kweli Yesu alikuwa ameachilia ole wenye kusumbua juu ya Jumuiya ya Wakristo. Lakini zitafuata zaidi!
[Maelezo ya Chini]
a Linga Yoeli 2:4, 5, 7 (ambapo wadudu wanaelezwa kuwa farasi, kikundi cha watu, na watu, na kama wakivuma kama gari la kukokotwa na farasi) na Ufunuo 9:7-9; pia, linga Yoeli 2:6, 10 (ikieleza habari ya tokeo lenye uchungu la tauni yenye kuletwa na wadudu hao) na Ufunuo 9:2, 5.
b Ona makala “Wenye Umoja Dhidi ya Mataifa Katika Bonde la Uamuzi” katika toleo la Desemba 1, 1961, la The Watchtower.
c Angalia kwamba andiko hili haliwezi kutumiwa kuthibitisha kwamba ndani ya abiso ulikuwamo moto, kana kwamba abiso ilikuwa namna fulani ya moto wa mateso. Yohana anasema yeye aliona moshi mzito uliokuwa “kama,” au mfano wa moshi wa tanuri kubwa. (Ufunuo 9:2) Yeye haripoti kuwa anaona miale hasa katika abiso.
d Lile neno la Kigiriki lililotumiwa hapa hutokana na neno la asili ba·sa·niʹzo, ambalo nyakati nyingine hutumiwa kuhusu mateso halisi; hata hivyo, laweza kutumiwa pia kuhusu mateso ya akilini. Mathalani, kwenye 2 Petro 2:8, NW tunasoma kwamba Loti “alikuwa akitesa nafsi yake yenye uadilifu” kwa sababu ya uovu alioona katika Sodoma. Viongozi wa kidini wa wakati wa kimitume walipatwa na mateso ya kiakili ingawa, bila shaka, ni kwa sababu tofauti sana.
e Gazeti hili lilipewa jina jipya Consolation katika 1937 na Awake! katika 1946.
-
-
Ole wa Pili—Majeshi ya Wapanda-FarasiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 23
Ole wa Pili—Majeshi ya Wapanda-Farasi
1. Zijapokuwa jitihada za viongozi wa kidini za kufutilia mbali nzige, kumekuwa nini, na kuja kwa ole zaidi mbili kunaonyesha nini?
KUANZIA 1919 na kuendelea, shambulio la nzige wa ufananisho juu ya Jumuiya ya Wakristo limesumbua sana viongozi wa kidini. Wao wamejaribu kufutilia mbali hao nzige, lakini hao wameendelea kuja wakiwa na uthabiti zaidi ya wakati uliotangulia. (Ufunuo 9:7) Na si hayo tu. Yohana anaandika: “Ole mmoja umepita. Tazama! Ole nyingine mbili zaidi zaja baada ya vitu hivi.” (Ufunuo 9:12, NW) Tauni zenye kutesa zaidi ziko akibani kwa ajili ya Jumuiya ya Wakristo.
2. (a) Kunakuwa nini wakati malaika wa sita anapopuliza tarumbeta yake? (b) Ile “sauti moja kutoka pembe za madhabahu ya dhahabu” inawakilisha nini? (c) Ni kwa nini malaika wanne wanatajwa?
2 Ni nini chanzo cha ole wa pili? Yohana anaandika: “Na malaika wa sita akapuliza tarumbeta yake. Na mimi nikasikia sauti moja kutoka pembe za madhabahu ya dhahabu iliyo mbele za Mungu ikisema kwa malaika wa sita, ambaye alikuwa na tarumbeta: ‘Fungua malaika wanne ambao wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati.’” (Ufunuo 9:13, 14, NW) Kuachiliwa kwa malaika hao ni katika kujibu sauti ambayo inakuja kutoka pembe za madhabahu ya dhahabu. Hii ni madhabahu ya dhahabu ya uvumba, na mara mbili katika wakati uliopita uvumba wa mabakuli ya dhahabu kutoka madhabahu hii umeshirikishwa na sala za watakatifu. (Ufunuo 5:8; 8:3, 4) Kwa sababu hiyo, hii sauti moja inawakilisha sala za umoja za watakatifu duniani. Wanaomba kwamba wao wenyewe waokolewe kwa ajili ya utumishi zaidi wa kutumia nishati wakiwa “wajumbe” wa Yehova, hiyo ikiwa ndiyo maana ya msingi ya neno la Kigiriki ambalo hapa limetafsiriwa “malaika.” Ni kwa nini kuna malaika wanne? Nambari hii ya ufananisho yaonekana ikionyesha kwamba wao wangekuwa wamepangwa kitengenezo sana hata kuenea dunia yote nzima.—Ufunuo 7:1; 20:8.
3. Ni jinsi gani malaika wanne walikuwa “wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati”?
3 Ni jinsi gani malaika hao walikuwa “wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati”? Katika nyakati za kale mto Eufrati ulikuwa ndio mpaka wa kaskazini-mashariki wa lile bara ambalo Yehova alikuwa amemwahidi Abrahamu. (Mwanzo 15:18; Kumbukumbu 11:24) Kwa wazi, hao “malaika” walikuwa wamezuiliwa mpakani mwa bara lao walilopewa na Mungu, au milki ya kidunia ya utendaji, wakizuiwa wasiingie kabisa ndani ya utumishi ambao Yehova alikuwa amewatayarishia. Pia Eufrati ulikuwa umeshirikishwa sana na lile jiji la Babuloni, na baada ya anguko la Yerusalemu katika 607 K.W.K., Waisraeli wa mnofu walitumia miaka 70 huko katika utekwa, ‘wakiwa wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati.’ (Zaburi 137:1) Mwaka wa 1919 uliwapata Waisraeli wa kiroho wakiwa wamefungwa katika kizuizi kama hicho, wakiwa wamehuzunika na wakiomba Yehova wapate mwongozo.
4. Ni utume gani ambao malaika wanne wanao, na umetimizwaje?
4 Kwa furaha, Yohana anaweza kuripoti: “Na wale malaika wanne walifunguliwa, ambao wametayarishwa kwa ajili ya saa na siku na mwezi na mwaka, kuua theluthi ya wanadamu.” (Ufunuo 9:15, NW) Yehova ni Mtunza-Wakati aliye sahihi. Yeye ana ratiba ya wakati naye anashikamana nayo. Kwa sababu hiyo, wajumbe hawa wanaachiliwa barabara kulingana na ratiba na kwa wakati ili watimize kazi waliyo nayo kufanya. Wazia shangwe yao walipotoka kwenye utumwa katika 1919, wakiwa tayari kwa kazi! Wao wana utume si wa kutesa tu bali mwishowe wa “kuua theluthi ya wanadamu.” Huu unahusiana na zile tauni zilizotolewa habari na ile mipigo ya tarumbeta nne za kwanza, zilizotesa theluthi ya dunia, bahari, wale viumbe walio ndani ya bahari, vibubujiko na mito, na vyanzo vya kimbingu vya nuru. (Ufunuo 8:7-12) Malaika wanne wanazidi hapo. Wao ‘wanaua,’ wakifichua kabisa kabisa hali ya kiroho yenye ufu ya Jumuiya ya Wakristo. Matamko yaliyotolewa kwa tarumbeta kuanzia 1922 na kuendelea kufikia wakati huu, yametimiza hilo.
5. Kwa habari ya Jumuiya ya Wakristo, mvumo wa mpigo wa tarumbeta ya sita ulikuwaje na mwangwi katika 1927?
5 Kumbuka, malaika wa kimbingu ndipo ametoka kuvumisha tarumbeta ya sita. Kwa kuitikia, wa sita wa ule mfululizo wa mikusanyiko ya kimataifa ya kila mwaka ya Wanafunzi wa Biblia ulifanywa Toronto, Ontario, Kanada. Huko programu ya Jumapili, Julai 24, 1927, ilipelekwa hewani kupitia stesheni za redio 53, mwenezo mkubwa zaidi wa msambazo wa stesheni za redio hadi wakati huo. Ujumbe huo wa kusemwa ulifikia wasikilizaji ambao inawezekana kuwa walikuwa mamilioni mengi. Kwanza, azimio lenye kani nyingi lilifichua Jumuiya ya Wakristo kuwa imekufa kiroho na likatoa mwaliko huu: “Katika saa hii ya hangaiko Yehova Mungu anaalika vikundi vya watu watoke katika, na kuacha kabisa ‘Jumuiya ya Wakristo’ au ‘Ukristo uliopangwa kitengenezo’ na kugeukia mbali nayo kabisa . . . ; [acheni] vikundi vya watu vijitoe kimoyo kabisa kwa Yehova Mungu na Mfalme na ufalme wake.” “Uhuru kwa Ajili ya Vikundi vya Watu” ndicho kilichokuwa kichwa cha hotuba ya watu wote iliyofuata. J. F. Rutherford aliitoa katika ule mtindo wake wa kawaida wenye nguvu-msukumo, wenye kufaa “moto na moshi na salfa” ambavyo Yohana anafuata kuona katika njozi.
6. Yohana anaelezaje habari ya majeshi ya wapanda-farasi anayofuata kuona?
6 “Na idadi ya majeshi ya wapanda-farasi ilikuwa mamiriadi mawili ya mamiriadi: mimi nilisikia idadi yao. Na hivi ndivyo mimi niliona wale farasi katika njozi, na walioketi juu yao: wao walikuwa na mabamba-kifua mekundu-moto na hayakintho-buluu na salfa-manjano; na vichwa vya farasi vilikuwa kama vichwa vya masimba, na katika vinywa vyao moto na moshi na salfa vilitoka. Kwa tauni tatu hizi theluthi ya wanadamu waliuawa, kwa moto na moshi na salfa ambavyo vilitoka katika vinywa vyao.”—Ufunuo 9:16-18, NW.
7, 8. (a) Majeshi ya wapanda-farasi hutoka kwa kishindo yakiwa chini ya mwelekezo wenye uongozi wa nani? (b) Ni katika njia zipi majeshi ya wapanda-farasi ni kama nzige walioyatangulia?
7 Kwa wazi, majeshi ya wapanda-farasi hawa huenda kwa kishindo chini ya mwelekezo wenye kuongoza wa malaika wanne. Lo! ni tamasha yenye kutia hofu kama nini! Wazia tendo-mwitikio lako kama wewe ungekuwa ndiwe shabaha ya shambulio kama hilo la majeshi ya wapanda-farasi! Mwonekano wao wenyewe ungepiga moyo wako kwa hofu. Ingawa hivyo, je! wewe umeona jinsi majeshi ya wapanda-farasi hawa wanavyofanana na nzige waliowatangulia? Nzige walikuwa kama farasi; katika majeshi ya wapanda-farasi kuna farasi. Kwa hiyo, vikosi vyote viwili vinahusika katika vita ya kitheokrasi. (Mithali 21:31) Nzige walikuwa na meno kama ya masimba; farasi wa majeshi ya wapanda-farasi wana vichwa kama vya masimba. Kwa hiyo, vikosi vyote viwili vinafungamanishwa na Simba wa kabila la Yuda mwenye ushujaa Yesu Kristo, ambaye ndiye Kiongozi, Kamanda, na Kielelezo wao.—Ufunuo 5:5, NW; Mithali 28:1.
8 Nzige na majeshi ya wapanda-farasi pamoja hushiriki katika kazi ya hukumu ya Yehova. Nzige waliibuka katika moshi ambao ulionya kimbele juu ya ole na moto wenye uharibifu kwa Jumuiya ya Wakristo; katika vinywa vya farasi mnatoka moto, moshi, na salfa. Nzige walikuwa na mabamba-kifua ya chuma, kuashiria kwamba mioyo yao ililindwa na kujitoa kusikopindika kwa ajili ya uadilifu; majeshi ya wapanda-farasi yalivaa mabamba-kifua yenye rangi nyekundu, buluu, na manjano, kurudisha moto, moshi, na salfa ya jumbe za hukumu zenye kuleta kifo zinazofoka katika vinywa vya farasi. (Linga Mwanzo 19:24, 28; Luka 17:29, 30.) Nzige walikuwa na mikia kama nge kwa ajili ya kutesa; farasi wana mikia kama manyoka kwa ajili ya kuua! Inaonekana kwamba kilichoanzwa na nzige chapasa kifuatiliwe na majeshi ya wapanda-farasi kwa mkazo mkubwa zaidi hadi utimilifu.
9. Majeshi ya wapanda-farasi hufananisha nini?
9 Kwa hiyo haya majeshi ya wapanda-farasi hufananisha nini? Kama vile jamii ya Yohana iliyopakwa mafuta ilivyoanza mbiu kama ya tarumbeta ya hukumu ya Yehova ya kisasi cha kimungu dhidi ya Jumuiya ya Wakristo, wakiwa na mamlaka ya ‘kuchoma kwa uchungu na kudhuru,’ ndivyo sisi tungetazamia kikundi icho hicho chenye uhai kitumiwe katika ‘kuua,’ yaani, katika kujulisha kwamba Jumuiya ya Wakristo pamoja na viongozi wa kidini wayo ni wafu kiroho kabisa kabisa, wakiwa wametupiliwa mbali na Yehova na wako tayari kwa ajili ya “tanuri ya moto” ya uharibifu wa milele. Kweli kweli, sehemu yote ya Babuloni Mkubwa lazima ipotelee mbali. (Ufunuo 9:5, 10; 18:2, 8; Mathayo 13:41-43, NW) Hata hivyo, kwa kutangulia uharibifu wayo, jamii ya Yohana inatumia “ule upanga wa roho, yaani, neno la Mungu,” katika kufichua hali kama ya kifo ya Jumuiya ya Wakristo. Malaika wanne na wapanda-farasi hutoa mwelekezo kwa huu uuaji wa kitamathali wa “theluthi ya wanadamu.” (Waefeso 6:17; Ufunuo 9:15, 18, NW) Hiyo huonyesha upangaji unaofaa wa kitengenezo na mwelekezo wa kitheokrasi chini ya uangalizi wa Bwana Yesu Kristo wakati kikosi cha watangazaji Ufalme kinapotoka kasi kushambulia piganoni.
Mamiriadi Mawili ya Mamiriadi
10. Ni katika maana gani kuna mamiriadi mawili ya mamiriadi ya majeshi ya wapanda-farasi?
10 Kunawezaje kuwa na mamiriadi mawili ya mamiriadi ya haya majeshi ya wapanda-farasi? Kihalisi miriadi moja ni 10,000. Kwa sababu hiyo, mamiriadi mawili ya mamiriadi yangekuwa milioni 200.a Kwa furaha, sasa kuna mamilioni ya watangazaji wa Ufalme, lakini hesabu yao ni kasoro sana ya mamia ya mamilioni! Ingawa hivyo, kumbuka maneno ya Musa kwenye Hesabu 10:36, NW: “Urudi, O Yehova kwenye mamiriadi ya maelfu ya Israeli.” (Linga Mwanzo 24:60.) Kihalisi, hiyo ingemaanisha, ‘Urudi kwenye makumi ya mamilioni ya Israeli.’ Hata hivyo, Israeli walikuwa hesabu yapata milioni mbili au tatu katika siku ya Musa. Basi, Musa alikuwa akisema nini? Hapana shaka yeye alikuwa akilini na wazo la kwamba Waisraeli wapaswa kuwa wasiohesabika kama “nyota za mbingu na kama chembe za mchanga ambazo ziko ufuoni mwa bahari,” badala ya kuhesabiwa. (Mwanzo 22:17; 1 Nyakati 27:23, NW) Hivyo, yeye alitumia neno la “miriadi” kuonyesha hesabu kubwa lakini isiyoonyeshwa waziwazi. Hivyo, The New English Bible hufasiri mstari huu hivi: “Pumzika, BWANA wa maelfu yasiyohesabika ya Israeli.” Hii inaafikiana na fasili ya pili ya neno la “miriadi” linalopatikana katika kamusi za Kigiriki na Kiebrania: “halaiki isiyohesabika,” “halaiki.”—The New Thayer’s Greek-English Lexicon of the New Testament; A Hebrew and English Lexicon of the Old Testament ya Gesenius, iliyotafsiriwa na Edward Robinson.
11. Ili jamii ya Yohana iwe mamiriadi hata katika maana ya ufananisho, ni jambo gani lingehitajiwa?
11 Hata hivyo, wale wa jamii ya Yohana ambao wangali wanabaki duniani hesabu yao ni chache zaidi ya 10,000—punde kuliko miriadi moja halisi. Wangewezaje kulinganishwa na maelfu yasiyohesabika ya majeshi ya wapanda-farasi? Ili wawe mamiriadi hata katika maana ya ufananisho, je! wasingehitaji kupata miimarisho? Hilo ndilo wamekuwa wakihitaji, na kwa fadhili zisizostahiliwa za Yehova, hilo ndilo wamepokea! Hiyo imetoka wapi?
12, 13. Ni matukio gani ya kihistoria kutoka 1918 mpaka 1935 yaliyoonyesha chanzo cha miimarisho?
12 Tangu 1918 hadi 1922 jamii ya Yohana ilianza kutolea binadamu wenye taabu taraja lenye furaha la kwamba “mamilioni wanaoishi sasa hawatakufa kamwe.” Katika 1923, pia ilifanywa ijulikane kwamba “kondoo” wa Mathayo 25:31-34 wangerithi uhai duniani chini ya Ufalme wa Mungu. Tumaini linalofanana na hilo lilitolewa katika kijitabu Freedom for the Peoples, kilichotolewa kwenye mkusanyiko wa kimataifa katika 1927. Katika miaka ya mapema ya 1930 jamii nyoofu ya Yehonadabu na wale ‘watu wanaolia na kuugua’ juu ya hali ya kiroho yenye kusikitisha ya Jumuiya ya Wakristo walionyeshwa kuwa ni wale wale kondoo walio na mataraja ya uhai wa kidunia. (Ezekieli 9:4; 2 Wafalme 10:15, 16) Likielekeza hao kwenye “majiji ya makimbilio” ya ki-siku-hizi, The Watchtower la Agosti 15, 1934, lilitaarifu hivi: “Wale wa jamii ya Yonadabu wamesikia mvumo wa tarumbeta ya Mungu na wametii onyo kwa kukimbilia tengenezo la Mungu na kushirikiana na watu wa Mungu, na ni lazima wakae humo.”—Hesabu 35:6, NW.
13 Katika 1935 wale wa jamii hii ya Yonadabu walialikwa kipekee wahudhurie mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C. U.S.A. Huko, Ijumaa, Mei 31, J. F. Rutherford alitoa hotuba yake yenye kujulikana sana “Mkutano Mkubwa,” ambayo katika hiyo yeye alionyesha waziwazi kwamba kikundi hiki cha Ufunuo 7:9 kilikuwa ni kile kile kama wale “kondoo” wa Mathayo 25:33—kikundi kilicho wakfu chenye matumaini ya kidunia. Kama utangulizi wa mambo yatakayokuja, kwenye mkusanyiko huo Mashahidi wapya 840 walibatizwa, walio wengi wao wakiwa wa wale wa umati mkubwa.b
14. Je! umati mkubwa ungekuwa na sehemu katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi wa ufananisho, na ni azimio gani lililoonyeshwa katika 1963?
14 Je! huu umati mkubwa umekuwa na sehemu katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi lililoanza 1922 na ambalo lilipokea mkazo kwenye mkusanyiko wa Toronto katika 1927? Chini ya mwelekezo wa malaika wanne, jamii ya Yohana iliyopakwa mafuta, hakika wanayo. Kwenye mkusanyiko wenye kuzunguka ulimwengu “Habari Njema za Milele” mkusanyiko wa 1963, walijiunga na jamii ya Yohana katika azimio lenye kuamsha. Hilo lilijulisha wazi kwamba ulimwengu “wakabili tetemeko la dunia la matata ya ulimwengu kama ambalo haujapata kujua kamwe, na matengenezo yao yote ya kisiasa na Babuloni wa kidini wao yatatikiswa yawe vipande vipande.” Azimio lilitolewa kwamba “sisi tutaendelea kujulisha wazi watu wote bila upendeleo ‘habari njema za milele’ kuhusu ufalme wa Mungu wa Kimesiya na kuhusu hukumu zake, ambazo ni kama tauni kwa adui zake lakini ambazo zitatekelezwa kwa ajili ya ukombozi wa watu wote wanaotamani kuabudu Mungu Muumba kwa kukubalika, kwa roho na kwa ukweli.” Azimio hilo lilikubaliwa kwa idili katika makusanyiko 24 kuzunguka tufe lote na jumla ya wakusanyikaji 454,977, ambao zaidi ya asilimia 95 walikuwa wa ule umati mkubwa.
15. (a) Katika 2005 umati mkubwa ulijumlika kuwa asilimia gani ya kani-kazi ambayo Yehova anatumia shambani? (b) Ile sala ya Yesu kwenye Yohana 17:20, 21 inaonyeshaje umoja wao pamoja na jamii ya Yohana?
15 Umati mkubwa umeendelea kujulisha peupe umoja wao usio na masharti pamoja na ile jamii ya Yohana katika kumimina tauni juu ya Jumuiya ya Wakristo. Katika 2005 huu umati mkubwa ulijumlika kuwa asilimia 99.8 ya kani-kazi ambayo Yehova anatumia katika shamba. Washiriki wao wanapatana kabisa kabisa na jamii ya Yohana, ambao kwa habari yao Yesu alisali kwenye Yohana 17:20, 21, NW hivi: “Mimi nafanya ombi, si kuhusu hawa tu, bali pia kuhusu wale wanaoweka imani yao katika mimi kupitia neno lao; ili kwamba wote wapate kuwa mmoja, kama vile wewe, Baba, ulivyo katika muungano pamoja na mimi na mimi katika muungano pamoja na wewe, kwamba wao pia wapate kuwa katika muungano pamoja na sisi, ili kwamba ulimwengu upate kuitikadi kwamba wewe ulituma mimi niende.” Jamii ya Yohana inapoongoza ikiwa chini ya Yesu, umati mkubwa unashiriki pamoja nao katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi lenye mkumbo ulio mkubwa zaidi sana katika historia yote ya kibinadamu!c
16. (a) Yohana anaelezaje habari ya vinywa na mikia ya farasi wa ufananisho? (b) Vinywa vya watu wa Yehova vimetayarishwaje kwa ajili ya utumishi? (c) Ni nini kinacholingana na uhakika wa kwamba “mikia yao ni kama manyoka”?
16 Hayo majeshi ya wapanda-farasi yanahitaji vifaa vya vita. Na lo! jinsi Yehova ameandaa hivi vizuri ajabu! Yohana anaeleza habari yavyo: “Kwa maana mamlaka yao imo katika vinywa vyao na katika mikia yao; kwa maana mikia yao ni kama manyoka na ina vichwa, na kwa hivyo wao hufanya dhara.” (Ufunuo 9:19, NW) Yehova ameweka rasmi wahudumu wake walio wakfu na kubatizwa kwa ajili ya utumishi huu. Yeye amewafundisha jinsi ya ‘kuhubiri neno’ kupitia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na mikutano mingine ya kundi na mashule, hivi kwamba wanapata uwezo wa kusema kwa mamlaka kwa “ulimi wa waliofundishwa.” Yeye ameweka maneno yake katika vinywa vyao na akawatuma watoke kwenda kujulisha hukumu zake “peupe na kutoka nyumba kwa nyumba.” (2 Timotheo 4:2; Isaya 50:4; 61:2; Yeremia 1:9, 10; Matendo 20:20, NW) Kwa maelfu ya mamilioni ya Biblia, vitabu, broshua, na magazeti yaliyogawanywa miaka iliyopita, jamii ya Yohana na umati mkubwa wameacha nyuma yao ujumbe wenye kuchoma kwa uchungu unaolingana na “mikia.” Kwa wapinzani wao, wanaoarifiwa juu ya “dhara” linalokuja kutoka kwa Yehova, haya majeshi ya wapanda-farasi yanaonekana kikweli kuwa mamiriadi mawili ya mamiriadi.—Linga Yoeli 2:4-6.
17. Je! Mashahidi wa Yehova wana sehemu yoyote katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi katika yale mabara ambako fasihi haziwezi kuenezwa kwa sababu kazi ni marufuku? Fafanua.
17 Washiriki wa sehemu yenye bidii zaidi sana ya haya majeshi ya wapanda-farasi ni ndugu walio katika mabara ambako kazi ya Mashahidi wa Yehova ni marufuku. Kama kondoo katikati ya mbwa-mwitu, hawa hawana budi kuwa “wenye tahadhari kama nyoka na hata hivyo bila hatia kama njiwa.” Kwa kutii Yehova wao ‘hawawezi kuacha kusema vitu ambavyo wameona na kusikia.’ (Mathayo 10:16; Matendo 4:19, 20; 5:28, 29, 32, NW) Kwa kuwa wana vifaa vichache vilivyochapwa vya kugawa peupe au hawana kabisa, je! ni lazima sisi tukate kauli kwamba wao hawana hisa katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi? Sivyo hata kidogo! Wao wana vinywa vyao na mamlaka kutoka kwa Yehova kuvitumia kusema ukweli wa Biblia. Wao wanafanya hivyo, vivi hivi na kwa usadikishi, wakianzisha mafunzo katika Biblia na ‘wakileta wengi kwenye uadilifu.’ (Danieli 12:3, NW) Ingawa huenda wao wasichome kwa uchungu kwa mikia yao katika maana ya kuacha nyuma fasihi zenye kupiga sana, moto, moshi, na salfa vya mfano hutoka katika vinywa vyao wanapotoa ushuhuda kwa busara na kwa uangalifu kuhusu siku ya utetezi ya Yehova inayokaribia.
18. Ni katika lugha ngapi na kwa hesabu gani kikosi hiki cha wapanda-farasi kimegawa ujumbe wenye kusumbua kwa namna iliyochapwa?
18 Kwingineko, fasihi za Ufalme huendelea kufichua mafundisho na njia za Kibabuloni za Jumuiya ya Wakristo, na kitamathali, zikileta “dhara” inalostahili. Kwa kutumia njia za kupiga chapa za ki-siku-hizi, kwa miaka 68 kabla ya 2005, haya majeshi ya wapanda-farasi wengi waliweza kugawa katika lugha za dunia zaidi ya 450, mabilioni ya Biblia, vitabu, magazeti, na broshua—mara nyingi zaidi ya mamiriadi mawili ya mamiriadi halisi. Lo! ni mchomo mchungu ulioje ambao mikia hiyo imetoa!
19, 20. (a) Ingawa shabaha hasa ya jumbe zenye kusumbua imekuwa Jumuiya ya Wakristo, wengine katika mabara yaliyo mbali na Jumuiya ya Wakristo wameitikiaje? (b) Yohana anaelezaje habari ya tendo-mwitikio la watu kwa ujumla?
19 Yehova alikusudia kwamba yaupasa ujumbe huu wenye kusumbua ‘uue theluthi ya wanadamu.’ Kwa sababu hiyo, shabaha yao hasa imekuwa Jumuiya ya Wakristo. Lakini umefikia mabara yaliyo nje ya Jumuiya ya Wakristo, kutia na mengi ambako unafiki wa dini za Jumuiya ya Wakristo unajulikana vizuri. Je! watu wa mabara haya wamekaribia Yehova zaidi kama tokeo la kuona kupigwa tauni kwa hili tengenezo la kidini lenye ufisadi? Wengi wamefanya hivyo! Kumekuwako na itikio la utayari miongoni mwa watu wasikivu na wenye kupendeka ambao wanaishi katika maeneo yaliyo nje ya kizio cha karibu cha uvutano wa Jumuiya ya Wakristo. Lakini kwa habari ya watu kwa ujumla, Yohana anaeleza habari ya tendo-mwitikio lao: “Lakini wabakio kati ya wanadamu ambao hawakuuawa na tauni hizi hawakutubu kazi za mikono yao, ili kwamba isiwapase kuabudu roho waovu na sanamu za dhahabu na fedha na shaba na jiwe na mti, ambazo haziwezi wala kuona wala kusikia wala kutembea; na wao hawakutubu mauaji kimakusudi yao wala mazoea yao ya uwasiliano na roho wala uasherati wao wala wivi wao.” (Ufunuo 9:20, 21, NW) Hakutakuwa na muongolewo wa waovu wasiotubu ulimwenguni pote. Wote wanaoendelea katika njia zao zenye uovu watalazimika kukabili hukumu mbaya kutoka kwa Yehova katika siku kubwa ya utetezi wake. Lakini “kila mmoja ambaye huita juu ya jina la Yehova ataponyoka akiwa salama.”—Yoeli 2:32; Zaburi 145:20; Matendo 2: 20, 21, NW.
20 Yale ambayo tumezungumzia ni sehemu tu ya ole wa pili. Kuna zaidi yanayokuja kabla ya ole huu kufikia mwisho wao, kama vile tutakavyoona katika sura zinazofuata.
[Maelezo ya Chini]
a Commentary on Revelation, ya Henry Barclay Swete husema hivi kuhusu hesabu “mamiriadi mawili ya mamiriadi”: “Hesabu hizi kubwa mno hukataza sisi kutafuta utimizo halisi, na elezo linalofuata huunga mkono mkataa huu.”
b Ona kurasa 119-26 zilizotangulia; pia Vindication, Kitabu cha Tatu, kilichotangazwa katika 1932 na Mashahidi wa Yehova, kurasa 83-4.
c Tofauti na nzige, majeshi ya wapanda-farasi yaliyoonwa na Yohana hayakuvaa “kilichoonekana kuwa mataji kama dhahabu.” (Ufunuo 9:7, NW) Hili linapatana na uhakika wa kwamba umati mkubwa, ambao leo ndio sehemu iliyo kubwa zaidi ya majeshi ya wapanda-farasi hautumaini kutawala katika Ufalme wa Mungu wa kimbingu.
-
-
Ujumbe Mtamu na MchunguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 24
Ujumbe Mtamu na Mchungu
Njozi ya 6—Ufunuo 10:1–11:19
Habari: Njozi ya hati-kunjo ndogo; maono ya hekaluni; kupulizwa kwa tarumbeta ya saba
Wakati wa utimizo: Tangu Yesu kuketishwa katika kiti cha ufalme 1914 mpaka dhiki kubwa
1, 2. (a) Ole wa pili ulitokeza nini, na ole huu utajulishwa wazi lini kwamba umekwisha? (b) Sasa Yohana anaona nani akishuka kutoka mbinguni?
ULE ole wa pili umekuwa wenye kukumba sana. Umesumbua Jumuiya ya Wakristo na viongozi wayo, “theluthi ya wanadamu,” ambao wamefichuliwa hivyo kuwa ni wafu kiroho. (Ufunuo 9:15, NW) Lazima Yohana awe alitaka kujua baada ya hapo ole wa tatu ungeweza kuleta nini. Lakini ngoja! Ole wa pili haujakwisha bado—mpaka tufikie lile jambo ambalo limerekodiwa kwenye Ufunuo 11:14. Kabla ya wakati huo, Yohana atashuhudia badiliko la matukio ambalo yeye mwenyewe anatwaa sehemu ya kutenda. Linaanza kwa mwono wenye kuvuvia kicho.
2 “Na mimi nikaona malaika mwingine kabambe akishuka kutoka katika mbingu, akiwa amepambwa wingu, na upinde-mvua ulikuwa juu ya kichwa chake, na uso wake ulikuwa kama jua, na nyayo zake zilikuwa kama nguzo zenye moto.”—Ufunuo 10:1, NW.
3. (a) Ni nani aliye “malaika kabambe”? (b) Ni nini maana ya upinde-mvua juu ya kichwa chake?
3 Ni nani huyu “malaika kabambe”? Kwa wazi yeye ni Yesu Kristo aliyetukuzwa akiwa katika daraka jingine. Yeye amepambwa wingu la kutokuonekana, jambo ambalo linatukumbusha maneno ya mapema zaidi ya Yohana: “Tazama! Yeye anakuja pamoja na mawingu, na kila jicho litaona yeye, na wale ambao walidunga yeye.” (Ufunuo 1:7, NW; linga Mathayo 17:2-5.) Upinde-mvua huo juu ya kichwa chake hukumbusha sisi njozi ya Yohana ya mapema zaidi ya kiti cha ufalme cha Yehova, chenye “upinde-mvua kama emeraldi katika kuonekana.” (Ufunuo 4:3, NW; linga Ezekieli 1:28.) Upinde-mvua ulidokeza utulivu na amani inayozunguka kiti cha ufalme cha Mungu. Katika njia iyo hiyo, upinde-mvua huu juu ya kichwa cha malaika ungemtambulisha yeye kuwa mjumbe maalumu wa amani, “Mwana-Mfalme wa Amani” wa Yehova aliyetabiriwa.—Isaya 9:6, 7, NW.
4. Ni nini kinachoonyeshwa na (a) uso wa malaika kuwa “kama jua”? (b) nyayo za malaika kuwa “kama nguzo zenye moto”?
4 Uso wa malaika kabambe ulikuwa “kama jua.” Mapema zaidi, katika njozi yake ya Yesu kwenye hekalu la kimungu, Yohana alikuwa amesema kwamba wajihi wa Yesu ulikuwa kama “jua wakati linapong’aa katika nguvu zalo.” (Ufunuo 1:16, NW) Yesu akiwa ndiye “jua la uadilifu,” hung’aa akiwa na ponyo katika mabawa yake kwa manufaa ya wale ambao huhofu jina la Yehova. (Malaki 4:2) Si uso pekee bali pia nyayo za malaika huyu ni zenye utukufu, “kama nguzo zenye moto.” Msimamo wake imara ni ule wa Mmoja ambaye Yehova amempa “mamlaka yote . . . katika mbingu na juu ya dunia.”—Mathayo 28:18; Ufunuo 1:14, 15, NW.
5. Yohana anaona nini katika mkono wa malaika kabambe?
5 Yohana huonelea zaidi: “Na katika mkono wake yeye alikuwa na hati-kunjo ndogo iliyofunguliwa. Na yeye akaweka wayo wake wa kulia juu ya bahari, lakini ule wa kushoto juu ya dunia.” (Ufunuo 10:2, NW) Hati-kunjo nyingine? Ndiyo, lakini wakati huu haikutiwa kifungo. Tukiwa pamoja na Yohana sisi tunaweza kutarajia kuona upesi mafumbo zaidi yenye kusisimua. Ingawa hivyo, kwanza tunapewa mazingira ya kitakachofuata.
6. (a) Ni kwa nini inafaa kwamba nyayo za Yesu ziko juu ya bahari na dunia? (b) Zaburi 8:5-8 ilitimizwa kabisa kabisa wakati gani?
6 Acheni turudi kwenye elezo kuhusu Yesu. Nyayo zake zenye moto ziko juu ya dunia na bahari, ambazo juu yazo yeye anatumia mamlaka kamili. Ni kama vile imetaarifiwa katika zaburi ya kiunabii: “Pia wewe [Yehova] uliendelea kumfanya yeye [Yesu] punde kidogo kuliko wafanana-mungu, kwa utukufu na umaridadi mno ndipo wewe ukavika yeye taji. Wewe ulifanya yeye amiliki juu ya kazi za mikono yako; kila kitu wewe umeweka chini ya nyayo zake: ng’ombe wadogo na maksai vyote hivyo, na pia hayawani wa konde lililo wazi, ndege wa mbingu na samaki wa bahari, kitu chochote kinachopita katika vijia vya zile bahari.” (Zaburi 8:5-8, NW; ona pia Waebrania 2:5-9.) Zaburi hii ilitimizwa kikamili katika 1914, wakati Yesu alipowekwa awe Mfalme wa Ufalme wa Mungu nao wakati wa mwisho ukaanza. Hivyo, yale anayoona Yohana hapa katika njozi yanahusu tangu mwaka huo.—Zaburi 110:1-6; Matendo 2:34-36; Danieli 12:4.
Ngurumo Saba
7. Ni kwa jinsi gani malaika kabambe hupiga kilio kikuu, na ni nini maana ya kilio chake?
7 Fikirio la Yohana juu ya malaika kabambe huyu linakatizwa na huyo malaika mwenyewe: “Na yeye [huyo malaika] akapiga kilio kwa sauti kubwa kama vile wakati simba anaponguruma. Na wakati yeye alipopiga kilio kikuu, ngurumo saba zikatamka sauti zazo zenyewe.” (Ufunuo 10:3, NW) Mpaazo kama huo wenye nguvu ungedaka uangalifu wa Yohana, ukithibitisha kwamba kwa kweli Yesu ndiye “Simba ambaye ni wa kabila la Yuda.” (Ufunuo 5:5, NW) Pia Yohana angejua kwamba Yehova, vilevile, nyakati nyingine husemwa kuwa ‘hunguruma.’ Kunguruma kwa Yehova hutoa habari kiunabii ya kukusanywa kwa Israeli wa kiroho na kuja kwa “siku ya Yehova” ya uharibifu. (Hosea 11:10; Yoeli 3:14, 16; Amosi 1:2; 3:7, 8, NW) Kwa wazi, basi, ule mlio kama wa simba wa huyu malaika kabambe huonya kimbele juu ya matukio makubwa yanayofanana na hilo kwa ajili ya bahari na dunia. Unaita ngurumo saba ziseme.
8. Ni nini zilizo ‘sauti za ngurumo saba’?
8 Wakati uliotangulia Yohana amesikia sauti zikitoka katika kiti cha ufalme chenyewe cha Yehova. (Ufunuo 4:5) Huko nyuma katika siku ya Daudi, nyakati nyingine ngurumo halisi ilikuwa ikisemwa kuwa ni “sauti ya Yehova.” (Zaburi 29:3, NW) Wakati Yehova alipotangaza kwa sauti yenye kusikika kusudi lake la kutukuza jina lake mwenyewe katika siku za huduma ya kidunia ya Yesu, kwa wengi ilisikika kama ngurumo. (Yohana 12:28, 29) Kwa sababu hiyo, inapatana na akili nzuri kukata maneno kwamba ‘zile sauti za ngurumo saba’ ni tamko la Yehova mwenyewe la makusudi yake. Uhakika wa kwamba kulikuwa na ngurumo saba hudokeza ukamili wa yale ambayo Yohana alisikia.
9. Sauti kutoka katika mbingu inaamuru nini?
9 Lakini sikiliza! Sauti nyingine yatoka ikivuma. Inaleta amri ambayo lazima ionekane ngeni kwa Yohana: “Sasa wakati ngurumo saba ziliposema, mimi nilikuwa karibu kutaka kuandika; lakini mimi nikasikia sauti moja kutoka katika mbingu ikisema: ‘Tia kifungo vitu ambavyo ngurumo saba zilisema, na usiandike hivyo.” (Ufunuo 10:4, NW) Lazima Yohana awe alikuwa na hamu nyingi ya kusikia na kuandika jumbe hizo zenye ngurumo, kama vile jamii ya Yohana leo imengojea kwa hamu nyingi Yehova afumbue makusudi yake ya kimungu yachapwe. Mafunuo kama hayo huja tu katika wakati wa Yehova uliowekwa.—Luka 12:42; ona pia Danieli 12:8, 9.
Tamati ya Siri Takatifu
10. Malaika kabambe anaapa kwa nani, na kwa tamshi gani?
10 Kwa wakati uliopo, Yehova ana utume mwingine kwa ajili ya Yohana. Baada ya ngurumo saba kuwa zimenguruma, malaika kabambe anasema tena: “Na malaika ambaye mimi niliona akisimama juu ya bahari na juu ya dunia aliinua mkono wake wa kulia kwenye mbingu, na kwa yule Mmoja ambaye huishi milele na milele, ambaye aliumba mbingu na vitu vilivyo ndani yayo na dunia na vitu vilivyo ndani yayo na bahari na vitu vilivyo ndani yayo, yeye akaapa: ‘Kutakuwa hakuna ukawio zaidi tena.’” (Ufunuo 10:5, 6, NW) Malaika kabambe anaapa kwa nani? Yesu aliyetukuzwa anaapa, si kwa yeye mwenyewe, bali kwa ile Mamlaka iliyo juu zaidi ya zote, Yehova, Muumba mbingu na dunia asiyeweza kufa. (Isaya 45:12, 18) Kwa kiapo hiki, malaika huyo anahakikishia Yohana kwamba hakutakuwa na ukawio tena kwa upande wa Mungu.
11, 12. (a) Ni nini kinachomaanishwa na “kutakuwa hakuna ukawio zaidi tena”? (b) Ni nini kinacholetwa kwenye tamati?
11 Neno la Kigiriki lililotafsiriwa hapa “ukawio” ni khroʹnos, ambalo kihalisi humaanisha “wakati.” Hivyo wengine wamehisi kwamba julisho-wazi hili la malaika lapaswa kutafsiriwa: “Kutakuwa hakuna wakati zaidi tena,” kana kwamba wakati kama tuujuavyo utakoma. Lakini neno khroʹnos hapa linatumiwa bila neno kidhihirisho. Hivyo, halimaanishi wakati katika maana ya ujumla, bali, “wakati fulani” au “kipindi fulani cha wakati.” Kwa maneno mengine, hakutakuwa na kipindi zaidi cha wakati (au, ukawio) kwa Yehova. Kitenzi cha Kigiriki kinachotokana na khroʹnos kinatumiwa pia kwenye Waebrania 10:37, ambapo Paulo akinukuu kutoka Habakuki 2:3, 4, (NW) huandika kwamba “yeye ambaye anakuja . . . hatakawia.”
12 “Hakuna ukawio zaidi tena”—Lo! jinsi maneno hayo yanavyovutia jamii ya Yohana leo inayozeeka! Ni katika jambo gani hakuna ukawio? Yohana anatujulisha: “Lakini katika siku za kuvumisha kwa malaika wa saba, wakati yeye yu karibu kupuliza tarumbeta yake, siri takatifu ya Mungu kulingana na habari njema ambazo yeye alijulisha wazi kwa watumwa wake mwenyewe manabii kweli kweli huletwa kwenye tamati.” (Ufunuo 10:7, NW) Wakati wa Yehova umefika wa kuleta “siri takatifu” yake kwenye upeo wa furaha, pamoja na fanikio tukufu!
13. Ni nini iliyo siri takatifu ya Mungu?
13 Ni nini hii “siri takatifu”? Inahusu mbegu iliyoahidiwa kwa mara ya kwanza katika Edeni, ambayo ilithibitika hasa kuwa Yesu Kristo. (Mwanzo 3:15; 1 Timotheo 3:16, NW) Inahusu pia utambulisho wa mwanamke ambaye kwake hiyo Mbegu inatoka. (Isaya 54:1; Wagalatia 4:26-28) Zaidi ya hilo, huingiza pia washiriki wa pili wa jamii ya mbegu na Ufalme ambao katika huo hiyo Mbegu hutawala. (Luka 8:10; Waefeso 3:3-9; Wakolosai 1:26, 27; 2:2; Ufunuo 1:5, 6) Habari njema kuhusu huu Ufalme wa kimbingu usio na kifani lazima zihubiriwe katika dunia yote katika wakati wa mwisho.—Mathayo 24:14.
14. Ni kwa nini ole wa tatu unafungamanishwa na Ufalme wa Mungu?
14 Hakika, hizi ndizo habari zilizo bora zaidi ya zote. Hata hivyo, kwenye Ufunuo 11:14, 15, ole wa tatu unafungamanishwa na Ufalme. Kwa nini? Kwa sababu wale wa aina ya binadamu ambao wanapendelea mfumo wa mambo wa Shetani, kupigwa tarumbeta ya habari njema kwamba siri takatifu ya Ufalme wa Mungu imeletwa kwenye tamati—yaani Ufalme wa Kimesiya wa Mungu upo hapa—ni habari zenye kujaa ole. (Linga 2 Wakorintho 2:16.) Humaanisha kwamba mpango wa ulimwengu ambao wao wanapenda sana unakaribia kuharibiwa. Sauti za ngurumo saba, zilizo na maonyo ya dhoruba yenye kuogofya zinazidi kuwa wazi na zenye sauti kubwa zaidi inapokaribia ile siku kuu ya Yehova ya kisasi.—Sefania 1:14-18.
Hati-Kunjo Iliyofunguliwa
15. Sauti kutoka katika mbingu na yule malaika kabambe yaambia Yohana nini, na ni nini tokeo kwa Yohana?
15 Wakati Yohana anapongojea kupulizwa kwa hii tarumbeta ya saba na kuletwa kwenye tamati kwa siri takatifu ya Mungu, yeye anapewa mgawo zaidi: “Na sauti ambayo mimi nilisikia kutoka katika mbingu inanena tena na mimi na kusema: ‘Nenda, kachukue hati-kunjo iliyo katika mkono wa malaika ambaye anasimama juu ya bahari na juu ya dunia.’ Na mimi nikaenda kwa malaika na nikamwambia anipe mimi hati-kunjo ndogo. Na yeye akasema kwangu mimi: ‘Ichukue na uile yote, na itafanya tumbo lako kuwa chungu, lakini katika kinywa chako itakuwa tamu kama asali.’ Na mimi nikachukua hati-kunjo ndogo kutoka mkono wa malaika na mimi nikaila yote, na katika kinywa changu ilikuwa tamu kama asali; lakini wakati mimi nilipokuwa nimeila, tumbo langu lilifanywa kuwa chungu. Na wao husema kwangu mimi: ‘Wewe ni lazima utoe unabii tena kwa habari ya vikundi vya watu na mataifa na ndimi na wafalme wengi.’”—Ufunuo 10:8-11, NW.
16. (a) Nabii Ezekieli alikuwaje na ono kama la Yohana? (b) Ni kwa nini hati-kunjo ndogo ilikuwa na ladha tamu kwa Yohana, lakini kwa nini ikawa chungu kutulia tumboni?
16 Ono la Yohana ni kama lile la nabii Ezekieli wakati wa uhamisho katika bara la Babuloni. Yeye pia aliamriwa ale hati-kunjo iliyokuwa na ladha tamu katika kinywa chake. Lakini wakati ilipojaa tumbo lake, ilimfanya awe na daraka la kutabiri vitu vichungu kwa nyumba ya Israeli yenye kuasi. (Ezekieli 2:8–3:15) Hati-kunjo iliyofunguliwa ambayo Yesu Kristo aliyetukuzwa anampa Yohana hali kadhalika ni ujumbe wa kimungu. Yohana anapaswa kuhubiria “vikundi vya watu na mataifa na ndimi na wafalme wengi.” Kujilisha hati-kunjo hii ni kutamu kwake kwa sababu inatokana na chanzo cha kimungu. (Linga Zaburi 119:103; Yeremia 15:15, 16.) Lakini yeye anaiona kuwa chungu kutulia tumboni kwa sababu—kama ilivyokuwa kwa Ezekieli wakati uliopita—inatabiri mambo yasiyo matamu kwa binadamu waasi.—Zaburi 145:20.
17. (a) Ni nani wanaoambia Yohana atoe unabii “tena,” na hiyo inamaanisha nini? (b) Ni wakati gani usimulizi-taswira wa kidrama alioona Yohana ulitazamiwa kutimizwa?
17 Wale wanaoambia Yohana kutabiri tena bila shaka ni Yehova Mungu na Yesu Kristo. Yohana, ijapokuwa yeye amehamishwa kupelekwa kwenye kisiwa cha Patmosi, tayari yeye ametoa unabii kwa habari ya vikundi vya watu, mataifa, ndimi, na wafalme kupitia habari iliyorekodiwa kufikia hapa katika kitabu cha Ufunuo. Neno “tena” humaanisha kwamba lazima yeye aandike na kutangaza habari inayobaki ambayo ilirekodiwa katika kitabu cha Ufunuo. Lakini kumbuka, Yohana kwa kweli anashiriki hapa njozi ya kiunabii. Kwa hakika, anayorekodi ni unabii wa kutimizwa baada ya 1914, wakati malaika kabambe anapochukua kikao chake akiwa ametagaa dunia na bahari. Basi, huu usimulizi-taswira wa kidrama humaanisha nini kwa jamii ya Yohana leo?
Ile Hati-kunjo Ndogo Leo
18. Kwenye mwanzo wa siku ya Bwana, ni kupendezwa gani ambako jamii ya Yohana ilionyesha katika kitabu cha Ufunuo?
18 Anavyoona Yohana hutangulia kuwa kivuli chenye kutazamisha cha ono la jamii ya Yohana mwanzoni mwa siku ya Bwana. Kuelewa kwao makusudi ya Yehova, kutia na dokezo la zile ngurumo saba, kulikuwa si kamili wakati huo. Hata hivyo, walipendezwa kwa kina kirefu na Ufunuo, na Charles Taze Russell alikuwa ameeleza juu ya sehemu nyingi zao wakati wa maisha yake. Baada ya kifo chake katika 1916, mengi ya maandishi yake yalikusanywa na kuchapishwa katika kitabu kilichoitwa The Finished Mystery. Ingawa hivyo, baada ya wakati kupita, kitabu hicho kilithibitika kuwa kisichotosheleza kuwa ufafanuzi wa Ufunuo. Baki la ndugu za Kristo lililazimika kungojea kwa muda zaidi uelewevu sahihi wa rekodi hiyo iliyovuviwa.
19. (a) Jamii ya Yohana ilitumiwaje na Yehova hata kabla sauti za ngurumo saba hazijatangazwa kikamili? (b) Ni lini jamii ya Yohana ilipopewa hati-kunjo ndogo iliyofunguliwa, na hii ilimaanisha nini kwao?
19 Hata hivyo, kama Yohana, wao walitumiwa na Yehova hata kabla zile sauti za ngurumo saba hazijatangazwa kikamili. Walikuwa wamehubiri kwa bidii-endelevu kwa miaka 40 kabla ya 1914, na walikuwa wamejitahidi kubaki wakiwa watendaji katika wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu. Wao walikuwa wamethibitika kuwa ndio wale ambao, wakati bwana-mkubwa alipowasili, walipatikana kuwa wakiwapa watu wa nyumbani chakula kwa wakati ufaao. (Mathayo 24:45-47) Hivyo, katika 1919 walikuwa ndio wale ambao walipewa hati-kunjo ndogo—yaani, ujumbe ulio wazi wa kuhubiria aina ya binadamu. Kama Ezekieli wao walikuwa na ujumbe kwa ajili ya tengenezo lisilo jaminifu—Jumuiya ya Wakristo—lililodai kumtumikia Mungu lakini, kwa kweli, halikuwa likifanya hivyo. Kama Yohana wao walipaswa kuhubiria zaidi “vikundi vya watu na mataifa na ndimi na wafalme wengi.”
20. Kula kwa Yohana hati-kunjo ndogo kulikuwa picha ya nini?
20 Kula kwa Yohana hati-kunjo yote kulitoa picha ya kwamba ndugu za Yesu walikubali mgawo huu. Ukawa sehemu yao kwa kadiri ya kwamba wao walikuwa wamehusianishwa na sehemu hii ya Neno la Mungu lililovuviwa, wakipata ulishaji kutokana nayo. Lakini walichopaswa kuhubiri kilikuwa na semi za hukumu za Yehova ambazo zilikuwa si tamu kwa wengi wa aina ya binadamu. Kweli kweli, kilitia ndani tauni zilizotabiriwa katika Ufunuo sura ya 8. Hata hivyo, ilikuwa tamu kwa Wakristo hawa wenye mioyo myeupe kujua hukumu hizo na kung’amua kwamba wao walikuwa wakitumiwa tena na Yehova katika kupiga mbiu yazo.—Zaburi 19:9, 10.
21. (a) Ujumbe wa hati-kunjo ndogo umekuwaje mtamu kwa umati mkubwa pia? (b) Ni kwa nini habari njema ni habari mbaya kwa wapinzani?
21 Baada ya wakati, ujumbe wa hati-kunjo hii ukawa pia mtamu kwa “umati mkubwa . . . kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na ndimi” waliopatikana kuwa walikuwa wakitweta kwa ajili ya vitu vyenye kukirihika walivyoona vikifanywa katika Jumuiya ya Wakristo. (Ufunuo 7:9, NW; Ezekieli 9:4) Hawa, vilevile, hupiga kisulubu mbiu ya habari njema, wakitumia maneno matamu, yenye neema kueleza uandalizi mzuri ajabu wa Yehova kwa ajili ya Wakristo wenye mfano wa kondoo. (Zaburi 37:11, 29; Wakolosai 4:6) Lakini kwa wapinzani hii ni habari mbaya. Kwa nini? Humaanisha kwamba mfumo ambao katika huo wanaitibari—na ambao huenda hata umewaletea utoshelezo wa muda—lazima uende. Kwa wao, habari njema humaanisha maangamizi.—Wafilipi 1:27, 28; linga Kumbukumbu 28:15; 2 Wakorintho 2:15, 16.
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 25
Kuhuisha Mashahidi Wawili
1. Yule malaika kabambe aomba Yohana afanye nini?
KABLA mwishowe ole wa pili haujapita, “malaika kabambe aomba Yohana ashiriki sehemu katika toleo jingine la kiunabii, hili likiwa linahusiana na hekalu. (Ufunuo 9:12; 10:1, NW) Hapa pana anavyoripoti Yohana: “Na mwanzi kama ufito nikapewa mimi alipokuwa akisema: ‘Inuka na kupima patakatifu pa hekalu la Mungu na madhabahu na wale wanaoabudu ndani yalo.’”—Ufunuo 11:1, NW.
Patakatifu pa Hekalu
2. (a) Ni patakatifu pa hekalu gani ambapo pangedumu mpaka siku yetu? (b) Ni nani aliye Kuhani Mkuu wa patakatifu pa hekalu na ni nini Patakatifu Zaidi Sana palo?
2 Hekalu linalotajwa hapa haliwezi kuwa hekalu halisi lolote katika Yerusalemu, kwa kuwa la mwisho la hayo liliharibiwa na Waroma katika 70 W.K. Hata hivyo, mtume Paulo alionyesha kwamba hata kabla ya uharibifu huo, palikuwa pametokea patakatifu pa hekalu pengine ambapo pangedumu mpaka siku yetu. Hili lilikuwa hekalu kubwa la kiroho ambalo lilitimiza mifano ya kiunabii iliyoandaliwa na ile tabenakulo na baadaye na mahekalu yaliyojengwa katika Yerusalemu. Ndilo “hema la kweli, ambalo Yehova alijenga, na si mwanadamu,” na Kuhani Mkuu walo ni Yesu, ambaye Paulo anasema habari zake kuwa alikuwa tayari ‘ameketi chini kwenye mkono wa kulia wa kiti cha ufalme cha Fahari ya Ufalme katika mbingu.’ Patakatifu Zaidi Sana palo ndipo mahali pa kuwapo kwa Yehova katika mbingu yenyewe.— Waebrania 8:1, 2; 9:11, 24, NW.
3. Kwenye tabenakulo, ni nini kilichokuwa picha ya (a) pazia lililotenganisha Patakatifu Zaidi Sana na Patakatifu? (b) dhabihu za wanyama? (c) madhabahu ya dhabihu?
3 Mtume Paulo anaeleza kwamba pazia la tabenakulo, lenye kutenganisha chumba cha Patakatifu Zaidi Sana na Patakatifu, ni picha ya mnofu wa Yesu. Wakati Yesu alipodhabihu uhai wake, pazia hili liliraruliwa sehemu mbili, katika maana ya kwamba mnofu wa Yesu haukuwa tena kizuizi cha kuingia kwake ndani ya kuwapo kwa Yehova katika mbingu. Kwa msingi wa dhabihu ya Yesu, makuhani wa chini wake wapakwa-mafuta ambao wangekufa wakiwa waaminifu, uwadiapo wakati, wangepita pia na kuingia katika zile mbingu. (Mathayo 27:50, 51; Waebrania 9:3; 10:19, 20, NW) Paulo anataja, vilevile, kwamba dhabihu za wanyama zilizoendelea kutolewa katika tabenakulo zilielekeza mbele kwenye dhabihu moja ya Yesu ya uhai wake mkamilifu wa kibinadamu. Madhabahu ya dhabihu katika ua iliwakilisha uandalizi wa Yehova, kulingana na mapenzi yake, kwa ajili ya kukubali dhabihu ya Yesu kwa niaba ya “wengi”—wa watakatifu na, baadaye, wa kondoo wengine ambao wangekuwa ‘wakimtafuta kwa hamu nyingi kwa ajili ya wokovu wao.’—Waebrania 9:28; 10:9, 10; Yohana 10:16, NW.
4. Ni nini kilichofananishwa na (a) Mahali Patakatifu (b) ule ua wa ndani?
4 Kutokana na habari hii iliyovuviwa kimungu, sisi tunaweza kukata maneno kwamba Mahali Patakatifu katika tabenakulo hufananisha hali takatifu inayofurahiwa kwanza na Kristo na kisha na washiriki wapakwa-mafuta wa ukuhani wa kifalme wa 144,000 wakati wao wangali duniani, kabla ya kuingia kupitia “pazia.” (1 Petro 2:9, NW) Inawakilisha vizuri kulelewa kwao kuwa wana wa kiroho wa Mungu, hata kama vile Mungu alivyomkiri Yesu kuwa Mwana wake kufuatia ubatizo wa Yesu katika Yordani katika 29 W.K. (Luka 3:22; Warumi 8:15) Namna gani ua wa ndani, sehemu pekee ya tabenakulo iliyoonekana kwa Waisraeli wasio wa kikuhani na mahali ambapo dhabihu zilitolewa? Hiyo ni picha ya msimamo mkamilifu wa binadamu Yesu uliomstahilisha yeye kutoa uhai wake kwa ajili ya aina ya binadamu. Inawakilisha pia msimamo wa uadilifu, unaohesabiwa kwa msingi wa dhabihu ya Yesu, ambao wafuasi wake wapakwa-mafuta wanafurahia wakati wanapotumikia hapa duniani.a—Warumi 1:7; 5:1.
Kupima Patakatifu pa Hekalu
5. Katika unabii wa Maandiko ya Kiebrania, ni nini kilichodokezwa na (a) kupimwa kwa Yerusalemu? (b) kupimwa kwa hekalu la njozi ya Ezekieli?
5 Yohana anaambiwa “kupima patakatifu pa hekalu la Mungu na madhabahu na wale wanaoabudu ndani yalo.” Hiyo inadokeza nini? Katika unabii wa Maandiko ya Kiebrania, kuhesabu kama huko kuliandaa dhamana ya kwamba haki ingetolewa kwa msingi wa viwango vikamilifu vya Yehova. Katika siku za Mfalme Manase mwovu, kule kupimwa kwa Yerusalemu kwa kiunabii kulishuhudia hukumu isiyobadilishika ya uharibifu wa jiji hilo. (2 Wafalme 21:13; Maombolezo 2:8) Hata hivyo, badaye wakati Yeremia alipoona Yerusalemu likipimwa, hiyo ilithibitisha kwamba jiji hilo lingejengwa tena. (Yeremia 31:39; ona pia Zekaria 2:2-8.) Hali kadhalika, ule upimaji mwingi na wenye mambo mengi wa hekalu la kinjozi lililoshuhudiwa na Ezekieli ulikuwa dhamana kwa Wayahudi wahamishwa katika Babuloni kwamba ibaada ya kweli ingerudishwa katika bara la nyumbani kwao. Pia kilikuwa kikumbusha kwamba, kwa sababu ya makosa yao, tangu hapo na kuendelea ilibidi Waisraeli wajipimishe kwa viwango vitakatifu vya Mungu.—Ezekieli 40:3, 4; 43:10.
6. Ni nini ishara ya Yohana kuambiwa apime patakatifu pa hekalu na makuhani wanaoabudu humo? Fafanua.
6 Kwa hiyo, wakati Yohana anapoamriwa apime patakatifu pa hekalu na wale makuhani wanaoabudu ndani yalo, hiyo ni ishara ya kwamba hakuna kitu kinachoweza kuzuia utimizo wa makusudi ya Yehova kwa habari ya mipango ya hekalu hilo na wale wanaoshirikishwa nalo, na kwamba makusudi hayo yanakaribia upeo wayo. Sasa kwa kuwa vitu vyote vimewekwa chini ya nyayo za malaika kabambe wa Yehova, ndio wakati kwa “ule mlima wa nyumba ya Yehova” kuwa “umewekwa kiimara juu ya kilele cha milima.” (Isaya 2:2-4, NW) Ibada safi ya Yehova lazima ikwezwe, baada ya karne nyingi za uasi-imani wa Jumuiya ya Wakristo. Pia ni wakati wa kufufuliwa kwa wale wa ndugu za Yesu waaminifu waliokufa waingie ndani ya “Patakatifu pa Patakatifu Pote.” (Danieli 9:24; 1 Wathesalonike 4:14-16; Ufunuo 6:11; 14:4, NW) Na wale wa mwisho walio duniani wa “watumwa wa Mungu wetu” lazima wapimwe kulingana na vile viwango vya kimungu ili wastahili kwa ajili ya mahali pao pa kudumu katika mpango wa hekalu wakiwa wana wa Mungu wazaliwa kwa roho. Jamii ya Yohana leo inajua kabisa viwango hivyo vitakatifu nayo imeazimia kujipatanisha navyo.—Ufunuo 7:1-3, NW; Mathayo 13:41, 42; Waefeso 1:13, 14; linga Warumi 11:20.
Kukanyagwa kwa Ua
7. (a) Ni kwa nini Yohana anaambiwa asipime ua? (b) Ni wakati gani jiji takatifu lilipokanyagwa chini ya nyayo kwa miezi 42? (c) Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walishindwaje kutegemeza viwango vya uadilifu vya Yehova kwa miezi 42?
7 Ni kwa nini Yohana alikatazwa kupima ua? Yeye anatuambia kwa maneno haya: “Lakini kwa habari ya ua ambao uko nje ya patakatifu pa hekalu, utupe nje kabisa na usiupime, kwa sababu umepewa kwa mataifa, na wao watakanyaga jiji takatifu kwa miezi arobaini na miwili.” (Ufunuo 11:2, NW) Tumeona kwamba ua wa ndani ni picha ya msimamo wa uadilifu duniani wa Wakristo waliozaliwa kwa roho. Kama tutakavyoona, rejezo hapa ni kwa miezi 42 halisi iliyoendelea kuanzia Desemba 1914 mpaka Juni 1918, wakati wote wadaio kuwa Wakristo walitiwa katika mtihani mkali. Je! wao wangeshikilia viwango vya uadilifu vya Yehova katika pindi ya hiyo miaka ya vita? Walio wengi hawakufanya hivyo. Kwa ujumla, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo waliweka utukuzo wa taifa mbele ya kutii sheria ya kimungu. Katika pande zote mbili za vita hiyo, ambayo ilipiganwa hasa katika Jumuiya ya Wakristo, viongozi wa kidini waliwahubiri vijana waingie katika mahandaki ya vita. Mamilioni kadhaa walichinjwa. Kufikia wakati hukumu ilianza na nyumba ya Mungu katika 1918, United States ilikuwa pia imeingia katika umwagaji-damu huo, na viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo yote walikuwa wamejitia katika hatia ya damu ambayo ingali inapiga kilio kwa ajili ya kisasi cha kimungu. (1 Petro 4:17) Kutupwa nje kwao kumekuwa kwa kudumu, kusikobadilika.—Isaya 59:1-3, 7, 8; Yeremia 19:3, 4.
8. Wakati wa Vita ya Ulimwengu 1, wengi wa Wanafunzi wa Biblia walikuja kung’amua nini, lakini ni jambo gani ambalo hawakuthamini kikamili?
8 Ingawa hivyo, vipi kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia? Je! wangepimwa mara hiyo katika 1914 kwa kushikamana kwao na viwango vya kimungu? La. Kama vile wale wanaodai kuwa Wakristo katika Jumuiya ya Wakristo, wao vilevile lazima watahiniwe. ‘Walitupwa nje kabisa, wakapewa kwa mataifa’ wajaribiwe vikali na kunyanyaswa. Wengi wao waling’amua kwamba hawapaswi kwenda nje wakaue binadamu mwenzao, lakini bado hawakuwa wamethamini kikamili kutokuwamo kwa Kikristo. (Mika 4:3; Yohana 17:14, 16; 1 Yohana 3:15) Chini ya mkazo kutoka mataifa, baadhi yao waliacha msimamo wao.
9. Ni jiji takatifu gani ambalo lilikanyagwa chini ya nyayo na mataifa, na duniani, ni nani waliowakilisha jiji hilo?
9 Ingawa hivyo, ni jinsi gani jiji takatifu lilikanyagwa na mataifa hayo? Kwa wazi, hii hairejezei Yerusalemu lililoharibiwa zaidi ya miaka 25 kabla Ufunuo haujaandikwa. Badala ya hivyo, hilo jiji takatifu ni Yerusalemu Jipya, linaloelezwa baadaye katika Ufunuo, ambalo linawakilishwa duniani sasa na mabaki ya Wakristo wapakwa-mafuta walio katika ua wa ndani wa hekalu. Baada ya wakati kupita, hawa pia watakuwa sehemu ya hilo jiji takatifu. Kwa hiyo kuwakanyaga ni sawasawa na kukanyaga hilo jiji takatifu lenyewe.—Ufunuo 21:2, 9-21.
Wale Mashahidi Wawili
10. Mashahidi waaminifu wa Yehova watafanya nini wanapokuwa wakikanyagwa?
10 Hata wanapokuwa wakikanyagwa washikamanifu hawa hawaachi kuwa mashahidi waaminifu wa Yehova. Kwa sababu hiyo, unabii huendelea: “‘Na mimi nitafanya mashahidi wangu wawili watoe unabii siku elfu moja mia mbili na sitini wakiwa wamevalia nguo za magunia.’ Hao wanafananishwa na mizeituni miwili na vinara vya taa viwili nao wanasimama mbele za Bwana wa dunia.”—Ufunuo 11:3, 4, NW.
11. Ilimaanisha nini kwa Wakristo wapakwa-mafuta waaminifu kutoa unabii “wakiwa wamevalia nguo za magunia”?
11 Wakristo hawa wapakwa-mafuta waaminifu walihitaji sifa ya uvumilivu, kwa kuwa walipaswa kutoa unabii “wakiwa wamevalia nguo za magunia.” Hiyo ilimaanisha nini? Katika nyakati za Biblia mara nyingi nguo ya gunia ilifananisha maombolezo. Kuivaa kulikuwa ishara ya kwamba mtu alikuwa ameshushwa katika huzuni au dhiki. (Mwanzo 37:34; Ayubu 16:15, 16; Ezekieli 27:31, NW) Nguo ya gunia ilishirikishwa na jumbe za maombolezo za maangamizi au huzuni ambazo manabii wa Mungu walipaswa kupigia mbiu. (Isaya 3:8, 24-26; Yeremia 48:37; 49:3) Kuvaa nguo ya gunia kungeweza kuonyesha unyenyekevu au toba kwa sababu ya onyo la kimungu. (Yona 3:5) Nguo za Magunia zenye kuvaliwa na mashahidi wawili huonekana kuwa zinaonyesha uvumilivu wa unyenyekevu katika kutangaza hukumu za Yehova. Wao walikuwa mashahidi wakipiga mbiu ya siku yake ya kisasi ambayo ingeleta pia maombolezo kwa mataifa hayo.—Kumbukumbu 32:41-43.
12. Ni kwa nini kipindi cha wakati ambacho jiji takatifu lingekanyagwa chini ya nyayo huonekana kuwa halisi?
12 Jamii ya Yohana ilipaswa ihubiri ujumbe huu kwa wakati dhahiri uliotajwa: siku 1,260, au miezi 42, urefu ule ule wa wakati ambao jiji takatifu lingekanyagwa chini ya nyayo. Kipindi hiki kinaonekana kuwa halisi, kwa maana kinasemwa kwa njia mbili tofauti, kwanza kwa miezi na kisha kwa siku. Kwa kuongezea, mwanzoni mwa siku ya Bwana, kulikuwako wakati uliotiwa alama wa miaka mitatu na nusu ambao magumu yaliyowapata watu wa Mungu yalilingana na matukio yaliyotolewa unabii hapa—kuanzia Desemba 1914 na kuendelea mpaka Juni 1918. (Ufunuo 1:10) Wao walihubiri ujumbe wa “nguo za magunia” kuhusu hukumu za Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo na ulimwengu.
13. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba Wakristo wapakwa-mafuta walifananishwa na mashahidi wawili? (b) Ni unabii gani wa Zekaria ambao tunakumbushwa na Yohana kuwaita mashahidi wawili “mizeituni miwili na vinara vya taa viwili”?
13 Uhakika wa kwamba wao walifananishwa na mashahidi wawili unatuthibitishia kwamba ujumbe wao ni sahihi na una msingi mzuri. (Linga Kumbukumbu 17:6; Yohana 8:17, 18.) Yohana anawaita “mizeituni miwili na vinara vya taa viwili,” akisema kwamba wao “wanasimama mbele za Bwana wa dunia.” Hili ni rejezo la wazi kwenye unabii wa Zekaria, ambaye aliona kinara cha taa chenye matawi saba na mizeituni miwili. Hiyo mizeituni ilisemekana kuwa ni picha ya “wapakwa-mafuta wawili,” yaani, Gavana Zerubabeli na Kuhani Mkuu Yoshua, “wanasimama kando ya Bwana wa dunia kwa ujumla.”—Zekaria 4:1-3, 14, NW.
14. (a) Ni nini kilichoonyeshwa na njozi ya Zekaria ya mizeituni miwili? na kinara cha taa? (b) Wakristo wapakwa-mafuta wangepatwa na nini wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu?
14 Zekaria aliishi wakati wa kujenga upya, na njozi yake ya mizeituni miwili ilimaanisha kwamba Zerubabeli na Yoshua wangebarikiwa kwa roho ya Yehova katika kuimarisha watu kwa ajili ya kazi. Njozi ya vinara vya taa ilikumbusha Zekaria ‘asidharau siku ya vitu vidogo’ kwa sababu makusudi ya Yehova yangetimizwa—“‘si kwa kani ya kijeshi, wala kwa nguvu, bali kwa roho yangu,’ Yehova wa majeshi amesema.” (Zekaria 4:6, 10; 8:9, NW) Kile kikosi kidogo cha Wakristo kilichodumu katika kupelekea aina ya binadamu nuru ya ukweli wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu kingetumiwa jinsi iyo hiyo katika kazi ya kujenga upya. Wao pia wangekuwa chanzo cha kitia-moyo na, wajapokuwa wachache, wangejifunza kutegemea imara ya Yehova, wasidharau siku ya mianzo midogo.
15. (a) Uhakika wa kwamba Wakristo wapakwa-mafuta walielezwa kuwa mashahidi wawili hutukumbusha nini pia? Fafanua. (b) Ni ishara za aina gani ambazo mashahidi wawili wamepewa mamlaka kufanya?
15 Uhakika wa kwamba wao walielezwa kuwa mashahidi wawili unakumbusha sisi pia juu ya kugeuka sura. Katika njozi hiyo, watatu wa mitume wa Yesu walimwona katika utukufu wa Ufalme, akiandamanwa na Musa na Eliya. Hilo lilitoa kimbele kivuli cha kuketi kwa Yesu juu ya kiti cha ufalme chake chenye utukufu katika 1914 atimize kazi iliyotangulia kutolewa kimbele kielezi na hao manabii wawili. (Mathayo 17:1-3) Kwa kufaa, hao mashahidi wawili wanaonwa sasa wakifanya ishara zinazokumbusha zile za Musa na Eliya. Mathalani, Yohana anasema hivi kwa habari yao: “Na ikiwa yeyote anataka kudhuru wao, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao; na ikiwa yeyote angepaswa kutaka kudhuru wao, kwa jinsi hii yeye lazima auawe. Hawa wana mamlaka kufunga mbingu ili kwamba mvua isianguke wakati wa kutoa kwao unabii.”—Ufunuo 11:5, 6a, NW.
16. (a) Ishara inayohusu moto inatukumbushaje wakati ambao mamlaka ya Musa ilipokaidiwa katika Israeli? (b) Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walikaidije Wanafunzi wa Biblia na wakachochea matata kwa ajili yao wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu, na hao walijipiganiaje?
16 Hii inatukumbusha wakati ambao mamlaka ya Musa ilipingwa katika Israeli. Nabii huyo alitamka maneno ya hukumu yenye moto, na Yehova aliwaharibu waasi hao, akila 250 kwa moto halisi kutoka mbinguni. (Hesabu 16:1-7, 28-35) Hali kadhalika, viongozi wa Jumuiya ya Wakristo walikaidi Wanafunzi wa Biblia, wakisema kwamba hao hawakuwa wamehitimu kamwe katika makoleji ya kitheolojia. Lakini mashahidi wa Mungu walikuwa na vitambulisho vya juu zaidi vya kuwa wahudumu: wale watu wasikivu waliotii ujumbe wao wa Kimaandiko. (2 Wakorintho 3:2, 3) Katika 1917 Wanafunzi wa Biblia walitangaza The Finished Mystery, elezo lenye nguvu juu ya Ufunuo na Ezekieli. Hicho kilifuatwa na mgawanyo wa nakala 10,000,000 za trakti ya kurasa nne The Bible Students Monthly ikiwa na makala kuu yenye kichwa “Anguko la Babuloni—Sababu Lazima Jumuiya ya Wakristo Iteseke Sasa—Tokeo la Mwisho.” Katika United States, wale viongozi wa kidini waliokasirika walitumia kichaa cha vita kuwa udhuru wa kufanya kitabu hicho kipigwe marufuku. Katika nchi nyinginezo kitabu hicho kilikaguliwa kabla ya kuruhusiwa. Hata hivyo, watumishi wa Mungu walifuliza kupiga vita kwa matoleo yenye moto ya trakti yenye kurasa nne iliyokuwa na kichwa Kingdom News. Kadiri siku ya Bwana ilivyoendelea, vichapo vingine vilionyesha wazi hali ya kufa kiroho ya Jumuiya ya Wakristo.—Linga Yeremia 5:14.
17. (a) Ni matukio gani katika siku za Eliya yaliyohusu ukame na moto? (b) Moto ulitokaje katika vinywa vya mashahidi wawili, na ni ukame gani uliohusika?
17 Vipi Eliya? Katika siku za wafalme wa Israeli, nabii huyu alipiga mbiu ya ukame kuwa wonyesho wa ghadhabu ya Yehova juu ya Waisraeli waabudu-Baali. Uliendelea kwa miaka mitatu na nusu. (1 Wafalme 17:1; 18:41-45; Luka 4:25; Yakobo 5:17) Baadaye, wakati Mfalme Ahazi alipotuma askari-jeshi wamlazimishe Eliya aje ndani ya kuwapo kwake kwa kifalme, nabii huyo aliita moto kutoka mbinguni uteketeze askari-jeshi hao. Ni wakati tu kamanda wa kivita alipoonyesha heshima inayofaa cheo chake akiwa nabii ndipo Eliya alikubali kuandamana naye kwenda kwa mfalme. (2 Wafalme 1:5-16) Hali kadhalika, kati ya 1914 na 1918, baki la wapakwa-mafuta lilivuta uangalifu kwa ujasiri kwenye hali ya ukame wa kiroho katika Jumuiya ya Wakristo na likaonya juu ya hukumu yenye moto kwenye “ile siku kubwa na yenye kuvuvia hofu ya Yehova inayokuja.”—Malaki 4:1, 5; Amosi 8:11, NW.
18. (a) Ni mamlaka gani waliyopewa mashahidi wawili, na ni jinsi gani ni kama ile aliyopewa Musa? (b) Mashahidi wawili walifichuaje Jumuiya ya Wakristo?
18 Yohana anazidi kusema hivi juu ya wale mashahidi wawili: “Na wao wana mamlaka juu ya maji kuyageuza kuwa damu na kupiga dunia kwa kila aina ya tauni mara nyingi kadiri watakavyo.” (Ufunuo 11:6b, NW) Ili kumsadikisha Farao aruhusu Israeli waende wakiwa huru, Yehova alitumia Musa apige Misri yenye uonevu kwa tauni kutia na kugeuza maji kuwa damu. Karne nyingi baadaye, Wafilisti adui za Israeli walikumbuka vizuri matendo ya Yehova dhidi ya Misri, hiyo ikiwafanya walie: “Ni nani ataokoa sisi kutoka mkono wa Mungu huyu mwenye fahari ya kifalme? Huyu ndiye yule Mungu ambaye alikuwa mpigaji wa Misri kwa kila aina ya uchinjaji [“mapigo,” Union Version] katika nyika.” (1 Samueli 4:8 NW; Zaburi 105:29) Musa alifananisha Yesu, ambaye alikuwa na mamlaka kutamka hukumu za Mungu juu ya viongozi wa kidini wa siku yake. (Mathayo 23:13; 28:18; Matendo 3:22) Na wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu ndugu za Kristo, wale mashahidi wawili, walifichua ile hali ya “maji” yenye kuleta kifo ambayo Jumuiya ya Wakristo ilikuwa ikiwapa makundi yayo.
Mashahidi Wawili Wauawa
19. Kulingana na simulizi la Ufunuo, kunatukia nini wakati mashahidi wawili wanapomaliza kushuhudu kwao?
19 Tauni hii ilikuwa kali sana hivi kwamba baada ya mashahidi wawili kuwa wametoa unabii kwa miezi 42 katika nguo za magunia, Jumuiya ya Wakristo ilitumia uvutano wayo wa kilimwengu kusababisha ‘wauawe.’ Yohana anaandika: “Na wakati wao wamekwisha kumaliza kushuhudu kwao, hayawani-mwitu ambaye hupanda kutoka katika abiso atafanya vita na wao na kushinda wao na kuua wao. Na maiti zao zitakuwa katika njia pana ya jiji kubwa ambalo kwa maana ya kiroho huitwa Sodoma na Misri, ambako pia Bwana yao alitundikwa kwenye nguzo. Na wale wa vikundi vya watu na makabila na ndimi na mataifa watatazama maiti zao kwa siku tatu na nusu, na wao hawaruhusu maiti zao zilazwe katika kaburi. Na wale wanaokaa juu ya dunia hushangilia juu yao na kujifurahisha wenyewe, na wao watapelekeana zawadi, kwa sababu manabii wawili hawa walitesa wale wanaokaa juu ya dunia.”—Ufunuo 11:7-10, NW.
20. Ni nini “hayawani-mwitu ambaye hupanda kutoka katika abiso”?
20 Hili ndilo la kwanza la marejezo 37 katika Ufunuo kwa hayawani-mwitu. Wakati uwadiapo tutachunguza huyu na hayawani wengine kwa ukamili. Kwa sasa yatosha kusema kwamba “hayawani-mwitu ambaye hupanda kutoka katika abiso” ni ubuni wa Shetani, mfumo wa mambo wa kisiasa ulio hai.b—Linga Ufunuo 13:1; Danieli 7:2, 3, 17.
21. (a) Wale maadui wa kidini wa mashahidi wawili walitumiaje kwa faida yao hali ya vita? (b) Uhakika wa kwamba zile maiti za mashahidi wawili ziliachwa bila kuzikwa ulionyesha nini? (c) Kipindi cha wakati cha siku tatu na nusu chapasa kionweje? (Ona kielezi cha chini.)
21 Kutoka 1914 kufika 1918 mataifa yalikuwa yakishughulika na vita ya kwanza ya ulimwengu. Hisi za utukuzaji wa taifa zilipanda juu, na katika masika ya 1918, maadui wa kidini wa mashahidi wawili walijifaidi na hali hiyo. Walitumia kwa hila chombo cha Serikali cha kisheria hivi kwamba wahudumu wenye madaraka miongoni mwa Wanafunzi wa Biblia walitiwa gerezani kwa mashtaka bandia ya kufitini serikali. Wafanya kazi wenzi waaminifu waliduwaa. Utendaji wa Ufalme karibu ulikoma. Ilikuwa kana kwamba ile kazi ya kuhubiri ilikuwa imekufa. Katika nyakati za Biblia ulikuwa utovu wa heshima mbaya sana kutolazwa katika kaburi la ukumbusho. (Zaburi 79:1-3; 1 Wafalme 13:21, 22) Kwa hiyo, suto kubwa lingeshikamana na kuacha mashahidi wawili bila kuzikwa. Katika hewa yenye joto ya Palestina, maiti ikiwa peupe katika barabara wazi ingeanza kuvunda kikweli baada ya siku tatu na nusu halisi.c (Linga Yohana 11:39.) Elezo hili lenye mambo mengi katika unabii huonyesha aibu ambayo hao mashahidi wawili walilazimika kuvumilia. Hao ambao wametajwa hapo juu ambao walitiwa gerezani hata walikatazwa dhamana wakati kesi zao zilipokuwa kwenye rufani. Walifichuliwa peupe muda mrefu kutosha kuwa uvundo kwa wakazi wa “jiji kubwa.” Lakini hili “jiji kubwa” lilikuwa nini?
22. (a) Ni nini jiji kubwa? (b) Vichapo vya umma vilijiungaje na viongozi wa kidini katika kushangilia juu ya kunyamazishwa kwa mashahidi wawili? (Ona kisanduku.)
22 Yohana anatupa sisi madokezo fulani. Yeye anasema kwamba Yesu alitundikwa kwenye nguzo huko. Hivyo mara moja sisi tunafikiria Yerusalemu. Lakini yeye anasema pia kwamba hilo jiji kubwa linaitwa Sodoma na Misri. Basi, Yerusalemu halisi liliitwa Sodoma wakati mmoja kwa sababu ya mazoea yalo machafu. (Isaya 1:8-10; linga Ezekieli 16:49, 53-58.) Na Misri, ile serikali ya ulimwengu kubwa ya kwanza, nyakati nyingine huonekana ikiwa picha ya huu mfumo wa mambo wa ulimwengu. (Isaya 19:1, 19; Yoeli 3:19) Kwa sababu hiyo, jiji hili kubwa ni picha ya “Yerusalemu” lililochafuliwa ambalo hudai kuabudu Mungu lakini ambalo limekuwa chafu na lenye dhambi, kama Sodoma, na sehemu ya huu mfumo wa wambo wa ulimwengu wa kishetani, kama Misri. Ni picha ya Jumuiya ya Wakristo, ambayo ni kisawe cha Yerusalemu lisilo jaminifu, tengenezo ambalo washiriki walo walikuwa na sababu kubwa sana ya kushangilia wakati waliponyamazisha ile kazi sumbufu ya mashahidi wawili ya kuhubiri.
Wainuliwa Tena!
23. (a) Inakuwaje kwa mashahidi wawili baada ya siku tatu na nusu, na tokeo ni nini kwa maadui wao? (b) Ni lini Ufunuo 11:11, 12 na unabii wa Ezekieli kuhusu Yehova akipulizia bonde la mifupa mikavu ulipopata utimizo wa ki-siku-hizi?
23 Vichapo vya umma vilijiunga na viongozi wa kidini katika kuharibu sifa ya watu wa Mungu, nyusipepa moja ikisema: “Tamati ya The Finished Mystery imetolewa.” Ingawa hivyo, hilo lilikuwa mbali sana na ukweli! Wale mashahidi wawili hawakubaki wakiwa wafu. Tunasoma: “Na baada ya siku tatu na nusu roho ya uhai kutoka kwa Mungu iliingia ndani yao, na wao wakasimama kwa nyayo zao, na hofu kubwa ikaanguka juu ya wale waliokuwa wakiona wao. Na wao wakasikia sauti kubwa kutoka mbingu ikisema kwao: ‘Njooni juu huku.’ Na wao wakaenda juu ndani ya mbingu kwa wingu na maadui wao wakaona wao.” (Ufunuo 11:11, 12, NW) Hivyo, wao walikuwa na ono kama lile la mifupa mikavu katika bonde ambalo Ezekieli alitembelea katika njozi. Yehova alipuliza juu ya hiyo mifupa mikavu, nayo ikawa hai, ikiandaa picha ya uzawa mpya wa taifa la Israeli baada ya miaka 70 ya utekwa katika Babuloni. (Ezekieli 37:1-14) Unabii huo muwili, katika Ezekieli na katika Ufunuo, ulikuwa na utimizo wao wa ki-siku-hizi wenye kutazamisha katika 1919, wakati Yehova aliporudisha mashahidi wake ‘waliokufa’ kwenye uhai wenye kusisimua.
24. Mashahidi wawili walipokuja kwenye uhai tokeo lilikuwa nini kwa wanyanyasi wao wa kidini?
24 Ulikuwa mshtuko kama nini kwa wanyanyasi hao! Ghafula maiti za mashahidi wawili zikawa hai tena na zenye kutenda. Viongozi wa kidini hao waliona uchungu sana, na zaidi hivyo kwa kuwa wahudumu hao Wakristo ambao walikuwa wametungia hila wawaweke katika gereza walikuwa huru tena, na baadaye wakaondolewa mashtaka kabisa. Mshtuko huo lazima uwe ulikuwa mkubwa hata zaidi wakati, katika Septemba 1919, hao Wanafunzi wa Biblia walipofanya mkusanyiko katika Sida Pointi Ohaiyo, U.S.A. Huko J. F. Rutherford, aliyeachiliwa karibuni, alichochea wakusanyikaji kwa hotuba yake “Kutangaza Ufalme,” iliyotegemea Ufunuo 15:2 na Isaya 52:7. Wale wa jamii ya Yohana wakaanza tena ‘kutoa unabii,’ au kuhubiri peupe. Walizidi kupata imara tena na tena, wakifichua kwa ujasiri unafiki wa Jumuiya ya Wakristo.
25. (a) Ni lini mashahidi wawili walipoambiwa, “Njooni juu huku,” na hilo lilitukiaje? (b) Urudisho wa mashahidi wawili ulikuwa na tokeo gani lenye kushtua jiji kubwa?
25 Jumuiya ya Wakristo ilijaribu tena na tena kurudia ushindi wayo wenye shangwe wa 1918. Ilianza kutumia watu wenye ghasia, kutunga hila kisheria, vifungo vya gereza, hata kunyongwa—lakini wapi! Baada ya 1919 ilikuwa haiwezi kufikia milki ya kiroho ya mashahidi wawili. Katika mwaka huo Yehova alikuwa amesema kwao: “Njooni juu huku,” nao walikuwa wamepanda kwenye hali ya kiroho iliyoinuliwa ambayo maadui wao wangeweza kuwaona lakini hawangeweza kuwagusa. Yohana anaeleza habari ya vile jiji kubwa liliathiriwa na tokeo lenye kushtua la kurudishwa kwao: “Na katika saa hiyo likatukia tetemeko la dunia kubwa, na asilikumi ya jiji ikaanguka; na watu elfu saba wakauawa na hilo tetemeko la dunia, na wanaobaki wakashikwa na kikuli na wakampa Mungu wa mbingu utukufu.” (Ufunuo 11:13, NW) Kulikuwako vurugu kubwa kikweli katika milki ya dini. Ardhi ilionekana inajongeza chini ya viongozi wa makanisa yaliyoimarishwa wakati hiki kikundi cha Wakristo kilichohuishwa kilipoanza kufanya kazi. Asilikumi moja ya jiji lao, kitamathali watu 7,000, waliathiriwa sana sana hivi kwamba wanasemekana kuwa waliuawa.
26. Ni nani wanaowakilishwa na “asilikumi ya jiji” na “elfu saba” wa Ufunuo 11:13? Fafanua.
26 Usemi “asilikumi ya jiji” hukumbusha sisi kwamba Isaya alitoa unabii kwa habari ya Yerusalemu la kale kwamba asilikumi ingeokoka uharibifu wa jiji hilo ikiwa mbegu takatifu. (Isaya 6:13) Hali kadhalika, nambari 7,000 hutukumbusha kwamba wakati Eliya alipohisi kwamba ni yeye pekee aliyebaki akiwa mwaminifu katika Israeli, Yehova alimwambia kwamba kwa uhakika kungali kulikuwako 7,000 ambao hawakuwa wameinamia Baali. (1 Wafalme 19:14, 18) Katika karne ya kwanza, mtume Paulo alisema kwamba hao 7,000 walikuwa ni picha ya baki la Wayahudi ambalo lilikuwa limeitikia habari njema juu ya Kristo. (Warumi 11:1-5) Maandiko haya hutusaidia sisi kuelewa kwamba “elfu saba” na “asilikumi ya jiji” katika Ufunuo 11:13 ni wale ambao huitikia mashahidi wawili waliorudishwa na ambao wanaacha jiji kubwa lenye dhambi. Wao ni kana kwamba wanakufa kwa Jumuiya ya Wakristo. Majina yao huondolewa kutoka katika orodha za umemba. Kwa kadiri inavyohusika wao hawaishi tena.d
27, 28. (a) ‘Wanaobaki walimpaje Mungu wa mbingu utukufu?’ (b) Viongozi wa kidini walilazimika kukubali nini?
27 Lakini ‘wanaobaki [wa Jumuiya ya Wakristo] walimpaje Mungu wa mbingu utukufu’? Hakika si kwa kuachana na dini zao zilizoasi imani na kuwa watumishi wa Mungu. Badala ya hivyo, ni kama vile imeelezwa katika Word Studies in the New Testament cha Vincent, katika kuzungumzia ule usemi “wakampa Mungu wa mbingu utukufu.” Humo imetaarifiwa hivi: “Fungu hilo huashiria si wongofu, wala toba, wala kutoa shukrani, bali utambuzi, ambao ndiyo maana yalo ya kawaida katika maandiko. Linga Yosh. vii. 19 (Sept.). Yohana ix. 24; Matendo xii 23; Rom. iv. 20.” Kwa udhiko layo, Jumuiya ya Wakristo ililazimika kukiri kwamba Mungu wa Wanafunzi wa Biblia alikuwa amefanya tendo kubwa kwa kuwarudisha kwenye utendaji wa Kikristo.
28 Huenda ikawa kwamba hao viongozi wa kidini walifanya ukiri huu kiakili tu, au kwa wao wenyewe. Bila shaka, hakuna wowote wao waliorekodiwa wakikiri peupe Mungu wa mashahidi wawili. Lakini unabii wa Yehova kupitia Yohana unatusaidia kutambua kilichokuwa mioyoni mwao na kung’amua mshtuko wenye kudhilisha uliowapata katika 1919. Toka mwaka huo na kuendelea, kadiri “elfu saba” walivyoacha Jumuiya ya Wakristo zijapokuwa jitihada za kuazimu kushikilia kondoo zayo, viongozi wa kidini walilazimishwa kutambua kwamba Mungu wa jamii ya Yohana alikuwa mwenye nguvu zaidi ya mungu wao. Katika miaka ya baadaye wao wangeng’amua hivyo hata kwa uwazi zaidi, kwa kuwa wengi zaidi wa kundi lao wangeondoka, wakirudisha mwangwi wa maneno ya watu wakati Eliya alipopata ushindi wenye shangwe juu ya wanadini wa Baali kwenye Mlima Karmeli: “Yehova ndiye Mungu wa kweli! Yehova ndiye Mungu wa kweli!”—1 Wafalme 18:39, NW.
29. Ni kitu gani ambacho Yohana anasema kinakuja upesi, na ni kutikiswa gani zaidi kunakongojea Jumuiya ya Wakristo?
29 Lakini sikiliza! Yohana anatuambia: “Ole wa pili umepita. Tazama! Ole wa tatu unakuja upesi.” (Ufunuo 11:14, NW) Ikiwa Jumuiya ya Wakristo imetikiswa na yale ambayo yametukia kufikia hapa, itafanya nini wakati ole wa tatu unapotangazwa, malaika wa saba anapopuliza tarumbeta yake, na mwishowe ile siri takatifu ya Mungu inaletwa kwenye tamati hatimaye kabisa?—Ufunuo 10:7.
[Maelezo ya Chini]
a Kupata mazungumzo kamili ya hili hekalu la kiroho, ona makala “Hekalu Kubwa la Kiroho la Yehova” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 1996 na “Hekalu la Kweli Moja Mahali pa Kuabudu” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Juni 1, 1972.
b “Abiso” (Kigiriki, aʹbys·sos; Kiebrania, tehohmʹ) hurejezea kimfano mahali pa kutotenda. (Ona Ufunuo 9:2.) Hata hivyo, katika maana halisi, inaweza pia kurejezea bahari kubwa mno. Mara nyingi neno la Kiebrania hutafsiriwa “kilindi cha maji.” (Zaburi 71:20; 106:9; Yona 2:5, NW) Hivyo, “hayawani-mwitu ambaye hupanda kutoka katika abiso” anaweza kutambulishwa na ‘hayawani-mwitu anayepanda kutoka katika bahari.’—Ufunuo 11:7; 13:1, NW.
c Angalia kwamba katika kuchunguza yanayopata maono ya watu wa Mungu wakati huu, inaonekana kwamba ingawa miezi 42 huwakilisha miaka mitatu na nusu halisi, siku tatu na nusu haziwakilishi kipindi halisi chenye saa 84. Inaelekea kwamba, kipindi mahususi cha siku tatu na nusu kimetajwa mara mbili (katika mstari wa 9 na 11) kukazia kwamba kingekuwa kipindi kifupi tu kikilinganishwa na miaka mitatu na nusu ya utendaji inayokitangulia.
d Linga utumizi wa maneno “-fia,” “-fu,” na “-ishi” katika maandiko kama Warumi 6:2, 10, 11; 7:4, 6, 9; Wagalatia 2:19; Wakolosai 2:20; 3:3.
-