Ayubu
40 Naye Yehova akaendelea kumjibu Ayubu, akasema:
2 “Je, inampasa mtu anayetafuta makosa kushindana na Mweza-Yote?+
Mwenye kumkaripia Mungu na ajibu hayo yeye mwenyewe.”+
3 Naye Ayubu akamjibu Yehova, akasema:
4 “Tazama! Nimekuwa kitu kisicho na maana.+
Nitakujibu nini?
Nimeuweka mkono wangu juu ya kinywa changu.+
5 Nimesema mara moja, nami sitajibu;
Na mara mbili, nami sitaongeza lolote.”
6 Na Yehova akaendelea kumjibu Ayubu kutoka katika ile dhoruba ya upepo,+ akasema:
7 “Tafadhali, jifunge viuno vyako, kama mwanamume;+
Nitakuuliza maswali, nawe unijulishe.+
8 Kwa kweli, je, utaifanya haki yangu kuwa bure?
Je, utanitangaza mimi kuwa mwovu ili wewe uwe upande wa haki?+
9 Au, je, una mkono kama ule wa Mungu wa kweli,+
Na, je, unaweza kutoa mngurumo kwa sauti kama yake?+
13 Wafiche pamoja katika mavumbi,+
Funga nyuso zao katika mahali palipofichika,
14 Nami, naam, mimi nitakupongeza,
Kwa sababu mkono wako wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Tazama, sasa, Behemothi* ambaye nimemfanya na wewe pia.
Yeye hula majani+ kama ng’ombe.
16 Tazama, basi, nguvu zake zimo katika viuno vyake,
Na nishati+ zake zimo katika kano za tumbo lake.
17 Yeye huinamisha mkia wake kama mwerezi;
Kano za mapaja yake zimeungamana pamoja.
18 Mifupa yake ni mianzi ya shaba;
Mifupa yake yenye nguvu ni kama fimbo za chuma iliyofuliwa.
21 Yeye hulala chini ya miyungiyungi yenye miiba,
Katika mahali palipofichika penye matete+ na mahali penye majimaji.+
22 Miyungiyungi yenye miiba humzuia kwa kivuli chake;
Mierebi ya bonde la mto humzunguka.
23 Mto ukitenda kwa jeuri, yeye hakimbii kwa wasiwasi.
Ana uhakika, hata Yordani+ ukifurika juu ya kinywa chake.
24 Je, yeyote anaweza kumshika akiwa anaona?
Je, yeyote anaweza kuitoboa pua yake kwa mitego?