Waroma
9 Ninasema kweli katika Kristo; sisemi uwongo, kwa kuwa dhamiri yangu yatoa ushahidi pamoja nami katika roho takatifu, 2 kwamba nina kihoro kikubwa na umivu lisilokoma moyoni mwangu. 3 Kwa maana ningeweza kutaka mimi mwenyewe niwe nimetenganishwa na Kristo kama mlaaniwa kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kulingana na mwili, 4 ambao, wakiwa hivyo, ni Waisraeli, ambao tendo la kufanywa kuwa wana ni lao na utukufu na maagano na upaji wa Sheria na utumishi mtakatifu na zile ahadi; 5 ambao akina baba wa zamani ni wao na ambao yule Kristo alizuka kutoka kwao kulingana na mwili: Mungu, aliye juu ya wote, awe mbarikiwa milele. Ameni.
6 Hata hivyo, si kama kwamba neno la Mungu lilikuwa limeshindwa. Kwa maana si wote ambao ni wa kuchipuka kutoka Israeli walio “Israeli” kikweli. 7 Wala si wote walio watoto kwa sababu wao ni mbegu ya Abrahamu, bali: “Ile itakayoitwa ‘mbegu yako’ itakuwa kupitia Isaka.” 8 Yaani, watoto wa mwili sio watoto wa Mungu kikweli, bali watoto kwa njia ya ahadi huhesabiwa kuwa ndiyo mbegu. 9 Kwa maana neno la ahadi lilikuwa kama ifuatavyo: “Kwenye wakati huu hakika nitakuja na Sara atakuwa na mwana.” 10 Lakini si kisa hicho tu, bali pia Rebeka alipochukua mimba kupata mapacha kwa mwanamume mmoja, Isaka baba yetu wa zamani: 11 kwa maana walipokuwa bado hawajazaliwa wala kuzoea kufanya jambo jema au ovu, ili kusudi la Mungu kwa habari ya kule kuchagua lipate kuendelea kutegemea, si kazi, bali Yeye aitaye, 12 Rebeka aliambiwa: “Mwenye umri mkubwa zaidi atakuwa mtumwa wa mwenye umri mdogo zaidi.” 13 Kama vile imeandikwa: “Nilimpenda Yakobo, lakini Esau nilimchukia.”
14 Basi, tutasema nini? Je, kwa Mungu kuna ukosefu wa haki? Hilo lisipate kuwa hivyo kamwe! 15 Kwa maana yeye amwambia Musa: “Hakika nitakuwa na rehema juu ya yeyote yule niwaye na rehema juu yake, nami hakika nitaonyesha huruma kwa yeyote yule nimwonyeshaye huruma.” 16 Hivyo basi, hilo lategemea, si yeye anayetaka wala yeye anayekimbia, bali Mungu, aliye na rehema. 17 Kwa maana Andiko lamwambia Farao: “Kwa sababu hiihii nimekuacha wewe ubaki, ili kwamba kuhusiana na wewe nipate kuonyesha nguvu yangu, na ili kwamba jina langu lipate kutangazwa katika dunia yote.” 18 Hivyo basi, yeye ana rehema juu ya yeye ambaye ataka, lakini juu ya yeye ambaye ataka humwacha awe mwenye shingo ngumu.
19 Kwa hiyo utaniambia: “Kwa nini bado yeye atafuta kosa? Kwa maana ni nani ambaye amekinza mapenzi yake yaliyo dhahiri?” 20 Basi, Ewe mtu, kwa kweli wewe ni nani hata uwe ukimjibu Mungu? Hakika je, kitu kilichofinyangwa kitamwambia yeye aliyekifinyanga, “Kwa nini ulinifanya mimi kwa njia hii?” 21 Ama je, mfinyanzi hana mamlaka juu ya udongo wa mfinyanzi kufanya kutokana na donge lilelile chombo kimoja kwa utumizi wenye kuheshimika, kingine kwa utumizi usio wenye kuheshimika? 22 Basi, ikiwa Mungu, ingawa anayo nia ya kuonyesha hasira ya kisasi yake na kujulisha nguvu yake, alivumilia kwa ustahimilivu mwingi vyombo vya hasira ya kisasi vilivyofanywa kufaa kwa ajili ya uharibifu, 23 ili apate kujulisha utajiri wa utukufu wake juu ya vyombo vya rehema, alivyotayarisha kimbele kwa ajili ya utukufu, 24 yaani, sisi, alioita si kutoka miongoni mwa Wayahudi tu bali pia kutoka miongoni mwa mataifa, kuna ubaya gani? 25 Ni kama asemavyo pia katika Hosea: “Wale ambao si watu wangu hakika nitawaita ‘watu wangu,’ na mwanamke ambaye hakuwa mpendwa nitamwita ‘mpendwa’; 26 na katika mahali walipoambiwa, ‘Nyinyi si watu wangu,’ hapo wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’”
27 Zaidi ya hayo, Isaya hupaaza kilio kuhusu Israeli: “Ijapokuwa idadi ya wana wa Israeli huenda ikawa kama mchanga wa bahari, ni mabaki watakaookolewa. 28 Kwa maana Yehova atafanyiza kutoa hesabu duniani, akikumaliza na kukukata kuwe kufupi.” 29 Pia, kama vile Isaya alivyokuwa amesema wakati wa mbele: “Isingekuwa Yehova wa majeshi alikuwa ametuachia sisi mbegu, tungalikuwa kama Sodoma, nasi tungalifanywa kama vile Gomora.”
30 Basi, tutasema nini? Kwamba watu wa mataifa, ijapokuwa kutokufuatia uadilifu, waliufikia uadilifu, uadilifu utokanao na imani; 31 lakini Israeli, ijapokuwa kufuatia sheria ya uadilifu, hakuifikia sheria. 32 Kwa sababu gani? Kwa sababu aliifuatia, si kwa imani, bali kama kwa kazi. Wao walijikwaa kwenye “jiwe la kukwaza”; 33 kama vile imeandikwa: “Tazama! Ninaweka katika Zayoni jiwe la kukwaza na tungamo-mwamba la udhia, lakini yeye awekaye imani yake juu yalo hatakuja kukata tamaa.”