4 “Na haya ndiyo mavazi watakayoyafanya: kifuko cha kifuani,+ na efodi+ na koti lisilo na mikono+ na kanzu yenye mirabamiraba, kilemba+ na ukumbuu;+ nao watafanya mavazi matakatifu kwa ajili ya Haruni ndugu yako na wanawe, ili awe kuhani kwangu.
7 Baada ya hayo akamvika kanzu+ na kumfunga ukumbuu+ na kumvika lile koti lisilo na mikono+ na kumvika efodi+ na kumfunga kwa mshipi+ wa ile efodi na kuufunga imara kwa mshipi huo.
4 Anapaswa kuvaa ile kanzu takatifu ya kitani,+ nayo ile suruali+ ya kitani itakuwa mwilini mwake, naye atajifunga kwa ukumbuu+ wa kitani na kujivika kile kilemba+ cha kitani. Hayo ni mavazi matakatifu.+ Naye atauosha mwili wake katika maji+ na kuyavaa.