13 Kwa hiyo Musa akawaamuru wana wa Israeli, na kusema: “Hii ndiyo nchi mtakayojigawia kwa kura+ iwe miliki, kama vile ambavyo Yehova ameamuru ili kuyapa yale makabila tisa na nusu.+
4 Basi wakaja mbele ya Eleazari+ kuhani na Yoshua mwana wa Nuni na wakuu, wakisema: “Yehova ndiye aliyemwamuru Musa atupe sisi urithi katikati ya ndugu zetu.”+ Basi akawapa urithi katikati ya ndugu za baba yao kwa agizo la Yehova.+
6 Nanyi kwa upande wenu, mtaandika vipimo vya ramani vya nchi katika mafungu saba, nanyi mtayaleta kwangu hapa, nami nitapiga kura+ hapa kwa ajili yenu mbele za Yehova Mungu wetu.