16 ndipo mimi nitawafanyia yanayofuata, na katika kutoa adhabu hakika nitaleta juu yenu usumbufu kwa kifua kikuu+ na homa kali, kufanya macho yafifie+ na kuifanya nafsi idhoofike.+ Nanyi mtapanda mbegu yenu bure, kwa maana adui zenu hakika wataila.+
51 Nao hakika watakula uzao wa wanyama wako wa kufugwa na mazao ya udongo wako mpaka utakapokuwa umeangamizwa,+ nao hawatakuachia nafaka yoyote, divai mpya au mafuta, mtoto wa ng’ombe wako au uzao wa kundi lako, mpaka watakapokuwa wamekuangamiza.+
37 na mazao yake yamejaa+ kwa ajili ya wafalme+ ambao umeweka juu yetu kwa sababu ya dhambi zetu,+ nao wanatawala juu ya miili yetu na juu ya wanyama wetu wa kufugwa, kulingana na mapenzi yao, nasi tumo katika taabu kubwa.+
7 Nchi yenu ni ukiwa,+ majiji yenu yameteketezwa kwa moto;+ udongo wenu—mbele ya macho yenu wageni+ wanaula,+ na ukiwa huo ni kama maangamizi yaliyofanywa na wageni.+
17 Hakika wao pia watakula mavuno yako na mkate wako.+ Watu hao watakula wana wako na binti zako. Watakula makundi yako na mifugo yako. Watakula mzabibu wako na mtini wako.+ Watavunja-vunja kwa upanga majiji yako yenye ngome unayoyategemea.”