Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 3:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Kisha Mungu akamwambia Musa tena:

      “Hivi ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli, ‘Yehova Mungu wa mababu zenu, Mungu wa Abrahamu,+ Mungu wa Isaka+ na Mungu wa Yakobo,+ amenituma kwenu.’ Hilo ndilo jina langu mpaka wakati usio na kipimo,+ na huo ndio ukumbusho wangu kwa kizazi baada ya kizazi.+

  • Kutoka 6:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Nami nilikuwa nikimtokea Abrahamu,+ Isaka+ na Yakobo+ kama Mungu Mweza-Yote,+ lakini kuhusu jina langu Yehova+ sikujifanya nijulikane+ kwao.

  • Kutoka 20:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Mimi ni Yehova Mungu wako,+ ambaye nimekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya watumwa.+

  • Zaburi 83:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Ili watu wajue+ kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+

      Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi,+ juu ya dunia yote.+

  • Zaburi 113:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Kutoka mapambazuko ya jua mpaka kutua kwake+

      Jina la Yehova ni la kusifiwa.+

  • Isaya 42:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu;+ nami sitampa mwingine yeyote utukufu wangu mwenyewe,+ wala sitazipa+ sanamu za kuchongwa sifa yangu.+

  • Malaki 2:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Ikiwa hamtasikiliza,+ na ikiwa hamtaiweka moyoni+ ili kulipa jina langu utukufu,”+ Yehova wa majeshi amesema, “mimi pia nitaleta juu yenu laana,+ nami nitazilaani baraka zenu.+ Ndiyo, hata nimeilaani baraka, kwa sababu hamwitii moyoni.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki