Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Nanyi mtazishika na kuzifanya, kwa sababu hiyo ni hekima+ kwenu na uelewaji+ kwenu mbele ya macho ya vikundi vya watu watakaosikia juu ya masharti yote haya, nao watasema, ‘Taifa hili kubwa bila shaka ni watu wenye hekima na wenye uelewaji.’+

  • Kumbukumbu la Torati 8:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Nawe umkumbuke Yehova Mungu wako, kwa sababu yeye ndiye anayekupa nguvu za kufanyiza mali;+ ili kutimiza agano lake ambalo aliwaapia mababu zako, kama ilivyo leo hii.+

  • Yoshua 1:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Ila tu uwe hodari na mwenye nguvu sana ili uangalie kufanya kulingana na sheria yote ambayo Musa mtumishi wangu alikuamuru.+ Usiiache, kwenda upande wa kuume wala wa kushoto,+ kusudi utende kwa hekima kila mahali unapoenda.+

  • 1 Wafalme 2:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Nawe lazima ushike wajibu wako kwa Yehova, Mungu wako, kwa kutembea katika njia+ zake, kwa kushika sheria zake, amri zake na maamuzi yake ya hukumu+ na shuhuda zake, kulingana na yaliyoandikwa katika sheria ya Musa,+ ili utende kwa busara katika kila jambo unalofanya na kila mahali unapoenda;

  • Zaburi 103:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini fadhili zenye upendo za Yehova ni za tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo+

      Kuwaelekea wale wanaomwogopa,+

      Na uadilifu wake kwa wana wa wana,+

  • Zaburi 103:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Kuwaelekea wale wanaolishika agano lake+

      Na kuwaelekea wale wanaoyakumbuka maagizo yake ili kuyafanya.+

  • Luka 11:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Lakini akasema: “Hapana, badala yake, Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki