9 “Ila jiangalie na kuitunza vema nafsi yako,+ ili usisahau mambo ambayo macho yako yameona,+ nayo yasiondoke moyoni mwako siku zote za maisha yako;+ nawe utawajulisha mambo hayo wana wako na wajukuu wako,+
11 Na ikawa kwamba walipokuwa wanakimbia kutoka mbele ya Israeli, wakiwa kwenye mteremko wa Beth-horoni, Yehova akawatupia mawe+ makubwa kutoka mbinguni mpaka Azeka, nao wakafa. Wale waliokufa kutokana na hayo mawe ya mvua walikuwa wengi kuliko wale ambao wana wa Israeli waliwaua kwa upanga.
13 Basi jua likasimama tuli, mwezi nao ukasimama, mpaka taifa hilo lilipokuwa limelipiza kisasi juu ya adui zake.+ Je, habari hizo hazikuandikwa katika kitabu cha Yashari?+ Na jua likaendelea kusimama katikati ya mbingu nalo halikuharakisha kwenda kutua kwa karibu siku nzima.+
40 Na Yoshua akaanza kuipiga nchi yote ya eneo lenye milima+ na Negebu+ na Shefela+ na miteremko+ na wafalme wao wote. Hakuacha mtu yeyote aokoke,+ akaangamiza+ kila kitu kilichopumua, kama vile Yehova Mungu wa Israeli alivyokuwa ameamuru.+
17 kutoka Mlima Halaki,+ unaopanda mpaka Seiri,+ na mpaka Baal-gadi+ katika nchi tambarare ya bondeni ya Lebanoni, pale chini ya Mlima Hermoni,+ naye akawakamata wafalme wao wote, akawapiga na kuwaua.+