18Ndipo kusanyiko lote la wana wa Israeli likakutanika Shilo,+ nao wakaweka huko lile hema la mkutano,+ kwa maana sasa nchi ilikuwa imetiishwa mbele yao.+
19 Mwishowe wakasema: “Tazama! Kuna sherehe ya Yehova kutoka mwaka mpaka mwaka katika Shilo,+ ambalo liko upande wa kaskazini wa Betheli, kuelekea upande wa mashariki wa njia kuu inayopanda kutoka Betheli kwenda Shekemu+ na kuelekea upande wa kusini wa Lebona.”
3 Na mtu huyo akawa akipanda kutoka jiji lake mwaka baada ya mwaka ili kusujudu+ na kutoa dhabihu kwa Yehova wa majeshi huko Shilo.+ Na hapo ndipo wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi,+ walikuwa makuhani kwa Yehova.+
12 “‘Hata hivyo, nendeni, sasa, mahali pangu palipokuwa katika Shilo,+ ambapo nilifanya jina langu likae hapo pale mwanzoni,+ na kuona nilivyopafanya kwa sababu ya ubaya wa watu wangu Israeli.+