17 Na hakika mimi nitauweka uso wangu juu yenu, nanyi hakika mtashindwa mbele ya adui zenu;+ nao wale wanaowachukia ninyi watawakanyagia chini,+ nanyi kwa kweli mtakimbia wakati ambapo hakuna mtu yeyote anayewafuatilia.+
14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ akawatia mikononi mwa waporaji, nao wakaanza kuwapora;+ naye akawauza mkononi mwa adui zao waliowazunguka pande zote,+ wala hawakuweza tena kusimama mbele ya adui zao.+
9 Nao wakamsahau Yehova, Mungu wao,+ naye akawauza+ mkononi mwa Sisera+ mkuu wa jeshi la Hasori na mkononi mwa Wafilisti+ na mkononi mwa mfalme wa Moabu,+ nao wakaendelea kupiga vita juu yao.