17 Na hakika mimi nitauweka uso wangu juu yenu, nanyi hakika mtashindwa mbele ya adui zenu;+ nao wale wanaowachukia ninyi watawakanyagia chini,+ nanyi kwa kweli mtakimbia wakati ambapo hakuna mtu yeyote anayewafuatilia.+
48 Nawe utalazimika kuwatumikia adui+ zako ambao Yehova atawatuma juu yako kwa njaa+ na kiu na uchi na uhitaji wa kila kitu; naye hakika ataweka nira ya chuma katika shingo yako mpaka atakapokuwa amekuangamiza wewe.+
14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ akawatia mikononi mwa waporaji, nao wakaanza kuwapora;+ naye akawauza mkononi mwa adui zao waliowazunguka pande zote,+ wala hawakuweza tena kusimama mbele ya adui zao.+