24 na moto ukatoka mbele za Yehova+ nao ukaanza kuteketeza lile toleo la kuteketezwa na vile vipande vyenye mafuta juu ya madhabahu. Watu wote walipoona hilo, wakaanza kupaaza sauti+ zao nao wakaanguka kifudifudi.
20 Basi ikawa kwamba, mwali wa moto ulipokuwa ukipaa kutoka katika madhabahu kuelekea mbinguni, malaika wa Yehova akapaa katika ule mwali wa madhabahu huku Manoa na mke wake wakitazama.+ Wakaanguka kifudifudi mara moja.+
26 Ndipo Daudi akamjengea Yehova madhabahu+ hapo na kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, naye akamwitia Yehova,+ambaye sasa alimjibu kwa moto+ kutoka mbinguni juu ya madhabahu ya toleo la kuteketezwa.
7Basi mara tu Sulemani alipomaliza kusali,+ moto ukashuka kutoka mbinguni,+ ukateketeza lile toleo la kuteketezwa+ na zile dhabihu, na utukufu+ wa Yehova ukaijaza nyumba ile.