2 Mambo ya Nyakati
7 Basi mara tu Sulemani alipomaliza kusali,+ moto ukashuka kutoka mbinguni,+ ukateketeza lile toleo la kuteketezwa+ na zile dhabihu, na utukufu+ wa Yehova ukaijaza nyumba ile. 2 Na makuhani hawakuweza kuingia ndani ya nyumba ya Yehova+ kwa sababu utukufu wa Yehova ulikuwa umeijaza nyumba ya Yehova. 3 Na wana wote wa Israeli walikuwa wakitazama wakati moto uliposhuka na utukufu wa Yehova ulipokuwa juu ya nyumba ile, kisha wakainama+ kifudifudi mara moja, juu ya sakafu ya mawe, wakasujudu+ na kumshukuru Yehova, “kwa maana yeye ni mwema,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
4 Na mfalme na watu wote walikuwa wakitoa dhabihu mbele za Yehova.+ 5 Na Mfalme Sulemani akatoa dhabihu ya ng’ombe 22,000 na kondoo 120,000.+ Hivyo ndivyo mfalme na watu wote walivyoizindua+ nyumba ya Mungu wa kweli. 6 Na makuhani+ walikuwa wamesimama katika vituo vyao vya kazi, na Walawi+ wakiwa na vyombo vya nyimbo+ kwa Yehova ambavyo Daudi+ mfalme alikuwa amevitengeneza ili kumshukuru Yehova, “kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo,” wakati Daudi alipokuwa akitoa sifa kwa mkono wao; na makuhani walikuwa wakipiga kwa sauti kubwa zile tarumbeta+ mbele zao, huku Israeli wote wakiwa wamesimama.
7 Kisha Sulemani akatakasa+ sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya nyumba ya Yehova, kwa sababu alitolea hapo yale matoleo ya kuteketezwa+ na vile vipande vya mafuta vya dhabihu za ushirika, kwa maana madhabahu ya shaba+ ambayo Sulemani alikuwa ametengeneza haikuweza kutoshea toleo la kuteketezwa na toleo la nafaka+ na vipande vya mafuta.+ 8 Na Sulemani akaifanya sherehe+ hiyo wakati huo kwa siku saba, na Israeli wote pamoja naye,+ kutaniko kubwa sana+ kuanzia maingilio ya Hamathi+ kushuka mpaka kwenye bonde la mto la Misri.+ 9 Lakini katika siku ya nane wakafanya kusanyiko kuu,+ kwa sababu kule kuzinduliwa kwa madhabahu walikuwa wamekufanya kwa siku saba na ile sherehe kwa siku saba. 10 Na katika siku ya 23 ya mwezi wa 7 akawaruhusu watu waende zao nyumbani kwao, wakiwa na shangwe+ na kuchangamka moyoni kutokana na wema+ ambao Yehova alikuwa amemtendea Daudi na Sulemani na Israeli watu wake.+
11 Hivyo Sulemani akaimaliza nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme;+ na kila jambo ambalo lilikuwa limeingia moyoni mwa Sulemani kufanya kuhusiana na nyumba ya Yehova na nyumba yake mwenyewe yeye alifanikiwa. 12 Sasa Yehova akamtokea+ Sulemani wakati wa usiku na kumwambia: “Nimeisikia sala yako,+ nami nimechagua+ mahali hapa kwa ajili yangu mwenyewe ili pawe nyumba ya dhabihu.+ 13 Ninapofunga mbingu ili mvua isinyeshe+ nami ninapoamuru panzi waile nchi+ nami nikileta tauni katikati ya watu wangu,+ 14 na watu wangu+ ambao jina langu limeitwa+ juu yao wajinyenyekeze+ na kusali+ na kuutafuta uso wangu+ na wageuke kutoka katika njia zao mbaya,+ basi mimi nitasikia nikiwa mbinguni+ na kusamehe dhambi yao,+ nami nitaiponya nchi yao.+ 15 Sasa macho+ yangu yatakuwa wazi na masikio+ yangu yatasikiliza sala katika mahali hapa. 16 Na sasa naichagua+ na kuitakasa nyumba hii ili jina langu+ liwe hapo mpaka wakati usio na kipimo,+ na macho yangu na moyo wangu vitakuwa hapo sikuzote.+
17 “Na wewe ukitembea mbele zangu, kama Daudi+ baba yako alivyotembea, kwa kutenda kulingana na yote ambayo nimekuamuru,+ nawe uyashike masharti+ yangu na maamuzi yangu ya hukumu+ 18 mimi pia nitakifanya imara kiti cha ufalme wako,+ kama nilivyofanya agano pamoja na Daudi baba yako,+ nikisema, ‘Hakuna mwanamume wa kwako atakayekatiliwa mbali asitawale juu ya Israeli.’+ 19 Lakini mkigeuka+ nyuma na kwa kweli mziache kanuni zangu+ na amri zangu+ ambazo nimeweka mbele yenu, nanyi kwa kweli mwende kuitumikia miungu mingine+ na kuiinamia,+ 20 mimi pia nitawang’oa kutoka katika nchi yangu ambayo nimewapa;+ na nyumba hii ambayo nimeitakasa+ kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali kutoka mbele za uso wangu,+ nami nitaifanya kuwa neno la kimethali+ na shutuma kati ya vikundi vyote vya watu.+ 21 Na nyumba hii iliyokuwa marundo ya mabomoko,+ kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao+ na kwa hakika aseme, ‘Kwa sababu gani Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+ 22 Nao watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova+ Mungu wa mababu zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri,+ nao wakashikamana na miungu mingine+ na kuiinamia na kuitumikia.+ Ndiyo sababu alileta juu yao msiba huu wote.’”+