25 Kwa maana leo ameshuka ili atoe dhabihu+ ya ng’ombe na vinono na kondoo kwa wingi sana, na kuwaalika wana wote wa mfalme na wakuu wa jeshi na Abiathari kuhani;+ na tazama, wanakula na kunywa mbele yake na kusema, ‘Mfalme Adoniya na aishi!’+
39 Kisha Sadoki kuhani akachukua pembe ya mafuta+ kutoka katika hema,+ akamtia mafuta+ Sulemani; nao wakaanza kupiga baragumu, na watu wote wakaanza kusema kwa sauti: “Mfalme Sulemani na aishi!”+
12 Kisha akamtoa nje mwana+ wa mfalme, akamvika taji+ na ule Ushuhuda;+ na basi wakamfanya kuwa mfalme+ na kumtia mafuta.+ Nao wakaanza kupiga makofi+ na kusema: “Mfalme na aishi!”+
9 Na ule umati, wale waliokuwa wakienda mbele yake na wale waliokuwa wakifuata wakawa wakipaaza sauti: “Mwokoe Mwana wa Daudi, tunaomba!+ Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova!+ Mwokoe, tunaomba, katika vilele vilivyo juu!”+