34 Na katika jambo hilo kukawa na kisababishi cha dhambi kwa nyumba ya Yeroboamu+ nayo ikawa sababu ya kuwafutilia mbali na kuwaangamiza kutoka katika uso wa nchi.+
31 Na Yehu hakuwa mwangalifu ili atembee katika sheria ya Yehova, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote.+ Yeye hakugeuka kutoka katika dhambi za Yeroboamu alizosababisha Israeli kutenda dhambi.+
21 Kwa maana alirarua Israeli kutoka katika nyumba ya Daudi, nao wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme; na Yeroboamu+ akawatenga Israeli wasimfuate Yehova, naye akawasababisha watende dhambi kubwa.+