54 Kwa hiyo, akamwita haraka mtumishi aliyechukua silaha zake na kumwambia: “Chomoa upanga wako, uniue,+ wasije wakasema juu yangu, ‘Mwanamke ndiye aliyemuua.’” Mara moja mtumishi wake akamchoma, naye akafa.+
4 Ndipo Sauli akamwambia mchukua-silaha wake: “Chomoa upanga wako,+ unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa+ wasije na kunichoma na kunitendea vibaya.” Naye mchukua-silaha wake hakutaka,+ kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga, akauangukia.+
23 Naye Ahithofeli akaona kwamba haikutendwa kulingana na shauri lake,+ naye akatandika punda, akaondoka na kwenda nyumbani kwake katika jiji lake.+ Kisha akawapa nyumba yake+ amri halafu akajinyonga,+ akafa.+ Basi akazikwa+ katika makaburi ya mababu zake.