26 Ahazia alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye akatawala mwaka mmoja katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Athalia+ mjukuu wa Omri+ mfalme wa Israeli.
6 Naye akaendelea kutembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ kama walivyofanya wale wa nyumba ya Ahabu; kwa maana binti ya Ahabu alikuwa amekuwa mke wake,+ naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+