Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 6:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Usiifuate miungu mingine, miungu yoyote ya vikundi vya watu wanaowazunguka pande zote,+

  • Kumbukumbu la Torati 31:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Tazama! Unalala pamoja na mababu zako;+ na hakika watu hawa watainuka+ na kufanya uasherati na miungu migeni ya nchi wanayoiendea,+ kati yao, nao hakika wataniacha+ na kuvunja agano langu ambalo nimefanya pamoja nao.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 15:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Kwa hiyo akaenda mbele ya Asa na kumwambia: “Mnisikilize mimi, Ee Asa na Yuda wote na Benyamini! Yehova yuko pamoja nanyi ikiwa ninyi mko pamoja naye;+ nanyi mkimtafuta,+ atawaruhusu mumpate, lakini mkimwacha yeye atawaacha ninyi.+

  • Zaburi 73:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Kwa maana, tazama! Walewale wanaokaa mbali nawe wataangamia.+

      Hakika utamnyamazisha kila mtu ambaye kwa njia isiyo ya adili anakuacha.+

  • Isaya 1:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Na anguko la waasi na la wenye dhambi litakuwa kwa wakati uleule mmoja,+ na wale wanaomwacha Yehova watafikia mwisho wao.+

  • Yeremia 2:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Ubaya wako unapaswa kukurekebisha,+ na matendo yako mwenyewe ya kukosa uaminifu yanapaswa kukukaripia.+ Jua, basi, na kuona kwamba kumwacha Yehova Mungu wako ni jambo baya na lenye uchungu,+ nawe hujaingiwa na hofu yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki