Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 34:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 usije ukafanya agano na wakaaji wa nchi hiyo, kwa maana hakika watafanya uasherati na miungu+ yao na kutolea miungu yao dhabihu,+ na mtu fulani hakika atakualika, nawe hakika utakula sehemu ya dhabihu yake.+

  • Waamuzi 2:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Nao hawakuwasikiliza hata waamuzi wao, lakini wakafanya uasherati+ na miungu mingine+ na kuiinamia. Waligeuka upesi kutoka katika njia ambayo mababu zao walikuwa wametembea kwa kutii amri za Yehova.+ Wao hawakufanya hivyo.

  • Zaburi 106:37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 Nao wakawa wakiwatoa dhabihu wana wao+

      Na binti zao kwa roho waovu.+

  • Zaburi 106:39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Nao wakawa wasio safi kwa sababu ya kazi zao+

      Na wakaendelea kufanya uasherati kwa matendo yao.+

  • Yeremia 3:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kuna msemo: “Mwanamume akimwacha mke wake na mke huyo aondoke kwake na kuwa wa mwanamume mwingine, je, mwanamume huyo anapaswa kurudi kwake tena?”+

      Je, nchi hiyo haikutiwa unajisi hakika?+

      “Nawe mwenyewe umefanya ukahaba pamoja na rafiki wengi;+ na je, unapaswa kurudi kwangu mimi?”+ asema Yehova.

  • Ezekieli 16:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 “‘Lakini ulianza kuutegemea urembo wako+ nawe ukawa kahaba kwa sababu ya jina lako+ na kumimina matendo yako ya ukahaba kwa kila mpita-njia;+ ukawa wake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki