6 huyo Ezra alitoka Babiloni; naye alikuwa mwandikaji stadi+ katika sheria ya Musa,+ ambayo Yehova Mungu wa Israeli alikuwa ametoa, hata mfalme akampa maombi yake yote, kulingana na mkono wa Yehova Mungu wake juu yake.+
28 Naye amenipa fadhili zenye upendo+ mbele ya mfalme na washauri+ wake na kuhusu wakuu wote wa mfalme wenye nguvu. Mimi nami nikajitia nguvu kulingana na mkono+ wa Yehova Mungu wangu juu yangu, nami nikawakusanya wakuu kutoka katika Israeli ili waende pamoja nami.
22 Kwa maana niliona haya kumwomba mfalme jeshi+ na wapanda-farasi+ ili kutusaidia juu ya adui zetu njiani, kwa sababu tulikuwa tumemwambia mfalme: “Mkono+ wa Mungu wetu uko juu ya wote wanaomtafuta kwa wema,+ bali nguvu zake na hasira zake+ ziko juu ya wote wanaomwacha.”+