Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 39:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Tazama! Umezifanya siku zangu kuwa chache tu;+

      Na urefu wa maisha yangu si kitu mbele zako.+

      Kwa kweli kila mtu wa udongo, ingawa anasimama imara, si kitu ila pumzi tu.+ Sela.

  • Mhubiri 2:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Na mimi, naam, mimi nikageuka kuelekea kazi zangu zote ambazo mikono yangu ilikuwa imefanya na kuelekea kazi ngumu niliyokuwa nimejitahidi kuitimiza,+ na, tazama! kila kitu kilikuwa ubatili na kufuatilia upepo,+ wala hapakuwa na lolote lenye faida chini ya jua.+

  • Mhubiri 2:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Kwa maana amempa mwanadamu aliye mwema mbele zake+ hekima na ujuzi na furaha,+ bali amempa mtenda-dhambi shughuli ya kukusanya na kuleta pamoja ili tu ampe mtu aliye mwema mbele za yule Mungu wa kweli.+ Hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.+

  • Mhubiri 6:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Ni afadhali kuona kwa macho kuliko kutembea huku na huku kwa nafsi.+ Hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.+

  • Luka 12:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ndipo akawaambia: “Endeleeni kufungua macho yenu na mjilinde na kila namna ya tamaa,+ kwa sababu hata wakati mtu ana vitu vingi uzima wake hautokani na vitu alivyo navyo.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki