Mhubiri
2 Nilisema, naam mimi, moyoni mwangu:+ “Njoo basi, nikujaribu kwa kushangilia.+ Pia, uone mema.”+ Na tazama! hilo pia lilikuwa ubatili. 2 Nikasema juu ya kicheko: “Ni wazimu!”+ na juu ya shangwe:+ “Hii inafanya nini?”
3 Nikachunguza kwa moyo wangu kwa kuuchangamsha mwili wangu kwa divai,+ huku nikiuongoza moyo wangu kwa hekima,+ hata nipate kushika upumbavu mpaka nione kuna faida gani kwa wana wa binadamu katika mambo waliyofanya chini ya mbingu siku za maisha yao.+ 4 Nikafanya kazi kubwa zaidi.+ Nikajijengea nyumba;+ nikajipandia mashamba ya mizabibu.+ 5 Nikajifanyia mashamba na bustani,+ nikapanda humo aina zote za miti ya matunda. 6 Nikajifanyia vidimbwi vya maji+ ili kumwagilia maji msitu wenye miti.+ 7 Nikapata watumishi wa kiume na wajakazi,+ nikawa na wana waliozaliwa nyumbani mwangu.+ Pia, nikawa na mifugo, ng’ombe na kondoo kwa wingi kuliko wote walionitangulia katika Yerusalemu.+ 8 Pia nikajikusanyia fedha na dhahabu,+ na mali iliyo ya pekee kwa wafalme na wilaya za utawala.+ Nikajifanyia waimbaji wa kiume na wa kike+ na wale walio furaha tele+ ya wana wa binadamu, bibi, naam mabibi.+ 9 Nikawa mkuu zaidi na kuongezeka kuliko mtu yeyote aliyenitangulia katika Yerusalemu.+ Tena, nikaendelea kukaa na hekima yangu.+
10 Wala sikuyanyima macho yangu chochote ambacho yaliomba.+ Sikuunyima moyo wangu shangwe ya aina yoyote, kwa maana moyo wangu ulifurahia kazi yangu yote iliyo ngumu,+ nalo hilo likawa fungu langu katika kazi yangu yote iliyo ngumu.+ 11 Na mimi, naam, mimi nikageuka kuelekea kazi zangu zote ambazo mikono yangu ilikuwa imefanya na kuelekea kazi ngumu niliyokuwa nimejitahidi kuitimiza,+ na, tazama! kila kitu kilikuwa ubatili na kufuatilia upepo,+ wala hapakuwa na lolote lenye faida chini ya jua.+
12 Nami, naam mimi, nikageuka nione hekima+ na wazimu na upumbavu;+ kwa maana mtu wa udongo anayekuja baada ya mfalme anaweza kufanya nini? Jambo ambalo watu tayari wamefanya. 13 Nami, naam mimi, nikaona kwamba hekima ina faida kuliko upumbavu,+ kama vile nuru ilivyo na faida kuliko giza.+
14 Mtu yeyote mwenye hekima, macho yake yamo katika kichwa chake;+ lakini mjinga anaendelea kutembea katika giza tupu.+ Nami nimepata kujua, mimi pia, kwamba kuna mwisho mmoja ambao huwapata hao wote.+ 15 Nami mwenyewe nikasema moyoni mwangu:+ “Mwisho uleule unaompata mjinga+ utanipata mimi, naam mimi.”+ Kwa nini mimi basi, nikawa na hekima, hekima yenye kuzidi sana+ hivyo wakati huo? Kisha nikasema moyoni mwangu: “Hilo pia ni ubatili.” 16 Kwa maana mtu mwenye hekima hakumbukwi zaidi ya yule mjinga mpaka wakati usio na kipimo.+ Siku ambazo tayari zinakuja, kila mtu husahauliwa; naye mwenye hekima atakufa jinsi gani? Pamoja na mjinga.+
17 Nami nikauchukia uzima,+ kwa sababu ninavyoona ni kwamba kazi ambayo imefanywa chini ya jua ni yenye msiba,+ kwa maana kila jambo lilikuwa ni ubatili na kufuatilia upepo.+ 18 Nami, naam mimi, nikachukia kazi yangu yote iliyo ngumu ambayo niliifanya kwa bidii chini ya jua,+ ambayo ningemwachia mtu ambaye angekuja baada yangu.+ 19 Na ni nani anayejua kama atakuwa mwenye hekima au mpumbavu?+ Hata hivyo, atachukua usimamizi wa kazi yangu yote iliyo ngumu niliyoifanya kwa bidii ambayo ndani yake nilitumia hekima chini ya jua.+ Hilo pia ni ubatili. 20 Na mimi mwenyewe nikageuka niufanye moyo wangu ukate tamaa+ kuelekea kazi ngumu yote niliyokuwa nimefanya kwa bidii chini ya jua. 21 Kwa maana kuna mwanadamu ambaye amefanya kazi yake ngumu kwa hekima na kwa ujuzi na kwa ustadi,+ lakini mwanadamu ambaye hakufanyia kazi ngumu kitu hicho atapewa fungu lake huyo.+ Hilo pia ni ubatili na msiba mkubwa.+
22 Kwa maana mwanadamu hupata nini kwa ajili ya kazi yake yote iliyo ngumu na kwa ajili ya jitihada za moyo wake katika kufanya kazi ngumu chini ya jua?+ 23 Kwa maana siku zake zote, shughuli zake huleta maumivu na masumbuko,+ pia usiku moyo wake haulali kamwe.+ Hilo pia ni ubatili mtupu.
24 Kwa mwanadamu hakuna jambo bora kuliko kwamba ale, naam, anywe na kuifanya nafsi yake ione mema kwa sababu ya kazi yake ngumu.+ Hilo pia mimi nimeliona, naam mimi, ya kwamba linatoka kwenye mkono wa Mungu wa kweli.+ 25 Kwa maana ni nani ambaye hula+ na ni nani ambaye hunywa vizuri kuliko mimi?+
26 Kwa maana amempa mwanadamu aliye mwema mbele zake+ hekima na ujuzi na furaha,+ bali amempa mtenda-dhambi shughuli ya kukusanya na kuleta pamoja ili tu ampe mtu aliye mwema mbele za yule Mungu wa kweli.+ Hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.+