Mhubiri
Mhubiri
1 Maneno ya mkutanishaji,+ mwana wa Daudi, mfalme katika Yerusalemu.+ 2 “Ubatili mkubwa zaidi!”+ mkutanishaji amesema, “ubatili mkubwa zaidi! Kila kitu ni ubatili!”+ 3 Mwanadamu anapata faida gani katika kazi yake yote iliyo ngumu anayoifanya+ kwa bidii chini ya jua?+ 4 Kizazi kinaenda,+ kizazi kinakuja;+ lakini dunia inasimama mpaka wakati usio na kipimo.+ 5 Pia jua limechomoza, na kushuka,+ nalo linajitahidi kwa nguvu kwenda mahali pake ambapo litachomoza tena.+
6 Upepo unaenda kusini, nao unazunguka kuelekea kaskazini.+ Unaendelea kuzungukazunguka sikuzote,+ nao unairudia mizunguko+ yake.
7 Mito yote ya wakati wa majira ya baridi kali+ inaenda baharini,+ hata hivyo bahari haijai.+ Mahali inapoenda mito hiyo ya majira ya baridi kali, hapo ndipo inarudi ili iende tena.+ 8 Mambo yote yanachosha;+ hakuna mtu anayeweza kuzungumza juu yake. Jicho halitosheki kuona,+ wala sikio halijai kwa sababu ya kusikia.+ 9 Lile ambalo limetokea, ndilo litakalotokea;+ na lile ambalo limefanywa, ndilo litakalofanywa; na kwa hiyo, hakuna jambo jipya chini ya jua.+ 10 Je, kuna lolote ambalo mtu anaweza kusema juu yake: “Ona hili; ni jipya”? Tayari limekuwako tangu wakati usio na kipimo.+ Jambo ambalo limetokea lilikuwako kabla ya wakati wetu.+ 11 Watu wa nyakati zilizopita hawakumbukwi, wala wale watakaokuja baadaye hawatakumbukwa.+ Nao pia hawatakumbukwa kati ya wale watakaokuja baadaye.+
12 Mimi, mkutanishaji, nilikuwa mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.+ 13 Nami nikakusudia moyoni mwangu kutafuta na kuchunguza jinsi hekima+ inavyohusiana na kila jambo ambalo limefanywa chini ya mbingu—shughuli yenye msiba ambayo Mungu amewapa wana wa binadamu wajishughulishe nayo.+ 14 Niliona kazi zote zilizofanywa chini ya jua,+ na, tazama! mambo yote yalikuwa ubatili na kufuatilia upepo.+
15 Lililopotoshwa haliwezi kunyooshwa,+ nalo linalokosekana haliwezi kuhesabiwa. 16 Mimi, naam, mimi mwenyewe nilisema moyoni mwangu:+ “Tazama! Mimi mwenyewe nimepata hekima nyingi kuliko yeyote aliyenitangulia katika Yerusalemu,+ nao moyo wangu mwenyewe umeona kwa wingi sana hekima na ujuzi.”+ 17 Nami nikauruhusu moyo wangu ujue hekima na wazimu,+ nami nimejua upumbavu,+ kwamba hayo pia ni kufuatilia upepo.+ 18 Kwa maana katika wingi wa hekima mna mambo mengi yenye kuudhi,+ hivi kwamba anayeongeza ujuzi anaongeza maumivu.+