11 Vitawi vyake vitakapokuwa vimekauka, wanawake wanaoingia watavivunja, na kuviwasha.+ Kwa maana wao ni kundi la watu lisilo na hamu ya uelewaji.+ Ndiyo sababu Mtengenezaji wake hatalionyesha rehema, na Mfanyizaji wake hatalionyesha kibali.+
7 Hata korongo juu mbinguni—anajua vema nyakati zake zilizowekwa;+ na njiwa-tetere+ na barawai na teleka—huangalia vema wakati wa kila mmoja wao kuingia. Lakini watu wangu hawajaijua hukumu ya Yehova.”’+
6 Hakika watu wangu watanyamazishwa, kwa sababu hakuna ujuzi.+ Kwa kuwa wewe mwenyewe umeukataa ujuzi,+ mimi pia nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu;+ na kwa sababu unaendelea kuisahau sheria ya Mungu wako,+ hata mimi nitawasahau wana wako.+
44 nao watakuangusha chini wewe na watoto wako walio ndani yako,+ nao hawataacha jiwe juu ya jiwe+ ndani yako, kwa sababu hukufahamu wakati wa kukaguliwa kwako.”+