21 Na hapo wakaaji wa maeneo yasiyo na maji hakika watalala, na nyumba zao zitajaa bundi-tai.+ Na hapo mbuni watakaa, na roho waovu wenye umbo la mbuzi watarukaruka hapo.+
39 Kwa hiyo wakaaji wa maeneo yasiyo na maji watakaa pamoja na wanyama wenye kupiga mayowe, na mbuni watakaa ndani yake;+ na ndani yake yeye hatakaliwa tena kamwe, wala yeye hatakaa mahali popote kwa kizazi baada ya kizazi.”+
25 “Tazama, mimi niko dhidi yako,+ Ee mlima wenye kuharibu,”+ asema Yehova, “wewe mwenye kuiharibu dunia yote;+ nami nitaunyoosha mkono wangu juu yako na kukuviringisha kutoka katika miamba na kukufanya kuwa mlima ulioteketezwa.”+
62 Nawe useme, ‘Ee Yehova, wewe mwenyewe umesema juu ya mahali hapa, kupakatilia mbali ili kwamba mkaaji+ yeyote asiwe ndani yake, mwanadamu wala mnyama wa kufugwa, bali pawe mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.’
2 Naye akapaaza kilio kwa sauti yenye nguvu,+ akisema: “Ameanguka! Babiloni Mkubwa ameanguka,+ naye amekuwa makao ya roho waovu na mahali pa kuvizia pa kila pumzi+ chafu na mahali pa kuvizia pa kila ndege mchafu na mwenye kuchukiwa!+