17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo,+ ambaye aliwaua vijana wao kwa upanga+ katika nyumba ya patakatifu pao,+ wala hakumhurumia kijana wala bikira, mzee wala mkongwe.+ Kila kitu Yeye alikitia mkononi mwake.
17 Na Mfalme Sedekia akatuma watu kumchukua, na mfalme akaanza kumuuliza maswali katika nyumba yake mahali pa maficho.+ Naye akaendelea kusema: “Je, liko neno lolote kutoka kwa Yehova?” Yeremia akasema: “Liko!” Naye akaendelea kusema: “Utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babiloni!”+
5 Na jeshi la Wakaldayo likawafuatilia,+ nao wakamfikia Sedekia katika nchi tambarare ya jangwa la Yeriko.+ Kisha wakamchukua na kumleta kwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi+ ili atangaze hukumu juu yake.+
20 Nami nitautandaza wavu wangu juu yake, naye hakika atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia;+ nami nitamleta Babiloni na kujiweka katika hukumu pamoja naye huko kuhusiana na ukosefu wake wa uaminifu alionitendea.+