15 Na Yehova Mungu wa mababu zao akaendelea kutuma juu yao kupitia kwa wajumbe wake,+ akatuma tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake+ na makao yake.+
13 Na sasa kwa sababu mliendelea kufanya kazi hizi zote,’ asema Yehova, ‘nami nikaendelea kusema nanyi, nikiamka mapema na kusema,+ lakini hamkusikiliza,+ nami nikaendelea kuwaita, lakini hamkujibu,+
7 Kwa maana niliwaonya mababu zenu siku ile niliyowatoa katika nchi ya Misri+ na mpaka leo hii, nikiamka mapema na kuwaonya, nikisema: “Tiini sauti yangu.”+
10 Watu hawa wabaya wanaokataa kuyatii maneno yangu,+ wanaotembea katika ukaidi wa moyo+ wao na wanaoendelea kufuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiinamia,+ pia watakuwa kama mshipi huu ambao haufai kwa jambo lolote.’
12 Na ninyi katika matendo yenu mmetenda vibaya zaidi kuliko baba zenu,+ na, tazama, kila mmoja wenu anaufuata ukaidi+ wa moyo wake mbaya kwa kutonitii mimi.+