29 Na Wakaldayo wanaopiga vita juu ya jiji hili wataingia ndani na kuliwasha jiji hili na kuliteketeza kwa moto+ na nyumba ambazo juu ya paa zake wamemfukizia Baali moshi wa dhabihu na kuimiminia miungu mingine matoleo ya kinywaji kwa kusudi la kunitia uchungu.’+
22 “‘Tazama, mimi ninaamuru,’ asema Yehova, ‘na hakika mimi nitawarudisha katika jiji hili,+ nao watapiga vita juu yake na kuliteka na kuliteketeza kwa moto;+ na majiji ya Yuda nitayafanya kuwa mahame yenye ukiwa bila mkaaji.’”+
23 Nao wanawatoa nje wake zako wote na wana wako wote na kuwapeleka kwa Wakaldayo, nawe mwenyewe hutaponyoka mkononi mwao,+ lakini utakamatwa kwa mkono wa mfalme wa Babiloni, na kwa sababu yako jiji hili litateketezwa kwa moto.”+