Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nehemia 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Hata hivyo, wakakosa kutii,+ wakakuasi+ na kuzidi kutupa sheria yako nyuma ya migongo yao,+ wakawaua manabii wako mwenyewe,+ waliotoa ushahidi juu yao ili kuwarudisha kwako;+ nao wakaendelea kutenda matendo ya ukosefu mkubwa wa heshima.+

  • Isaya 1:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Lakini mkikataa+ na kwa kweli muwe waasi, mtaliwa na upanga; kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hayo.”+

  • Isaya 30:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Kwa maana wao ni watu waasi,+ wana wasiosema kweli,+ wana ambao hawataki kuisikia sheria ya Yehova;+

  • Isaya 63:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Lakini wao wenyewe waliasi+ na kuihuzunisha roho yake takatifu.+ Sasa alibadilika akawa adui+ yao; yeye mwenyewe alipiga vita juu yao.+

  • Ezekieli 2:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, ninakutuma kwa wana wa Israeli,+ kwa mataifa yenye kuasi ambayo yameniasi.+ Hao wenyewe na mababu zao wamenitendea makosa mpaka siku hii ya leo.+

  • Ezekieli 20:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 “ ‘ “Na hao wana wakaanza kuniasi.+ Hawakutembea katika sheria zangu, nayo maamuzi yangu ya hukumu hawakuendelea kuyashika kwa kuyafanya, ambayo, kama mtu akiendelea kuyafanya, ataendelea pia kuishi kwa hayo.+ Sabato zangu walizitia unajisi.+ Kwa hiyo nikaahidi kumwaga ghadhabu yangu juu yao, ili kuitimiliza hasira yangu juu yao nyikani.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki