9 Watumishi wangu watazishusha kutoka Lebanoni+ kwenda baharini; nami nitaziweka katika vyelezo vya magogo ili zisafirishwe baharini mpaka mahali ambapo utanijulisha;+ nami nitazifungua pale, nawe utazichukua; na kufanya mapendezi yangu kwa kutoa chakula kwa ajili ya nyumba yangu.”+
10 Na, tazama! kwa wakusanyaji wa mbao, wakataji wa miti, ninatoa chakula kwa watumishi wako, kori 20,000 za ngano,+ na kori 20,000 za shayiri, na bathi 20,000 za divai,+ na bathi 20,000 za mafuta.”
7 Nao wakawapa pesa+ wachongaji+ wa mawe na mafundi,+ na kuwapa Wasidoni+ na Watiro+ vyakula+ na vinywaji na mafuta,+ ili walete miti ya mierezi kutoka Lebanoni+ mpaka kwenye bahari iliyoko Yopa,+ kulingana na ruhusa waliyopewa na Koreshi+ mfalme wa Uajemi.
20 Sasa yeye alitaka kupigana na watu wa Tiro na wa Sidoni. Kwa hiyo wakamjia kwa umoja na, baada ya kumshawishi Blasto, aliyekuwa msimamizi wa chumba cha kulala cha mfalme, wakaanza kutoa ombi la kutaka amani, kwa sababu nchi yao iligawiwa chakula+ kutoka katika kile cha mfalme.