12 Yehova atakufungulia ghala lake zuri, mbingu, ili kunyesha mvua juu ya nchi yako katika majira+ yake na kubariki kila tendo la mkono wako;+ nawe hakika utakopesha mataifa mengi, hali wewe mwenyewe hutakopa.+
13 Na itakuwa kwamba kama vile mlivyokuwa laana katikati ya mataifa,+ enyi nyumba ya Yuda na nyumba ya Israeli,+ ndivyo nitakavyowaokoa, nanyi mtakuwa baraka.+ Msiogope.+ Mikono yenu na iwe na nguvu.’+
10 Leteni ghalani sehemu zote za kumi,+ ili kuwe na chakula nyumbani mwangu;+ nanyi, tafadhali, mnijaribu kwa njia hii,”+ Yehova wa majeshi amesema, “kama sitawafungulia ninyi malango ya mbinguni+ na kuwamwagia baraka hata kusiwe na uhitaji tena.”+