4 Usiogope,+ kwa maana hutaaibishwa; wala usifedheheke,+ kwa maana hutakatishwa tamaa.+ Kwa maana utaisahau hata aibu ya wakati wa ujana wako,+ nawe hutaikumbuka tena shutuma ya ujane wako wenye kuendelea.”
14 “Na wana wa wale wanaokutesa watakuja kwako, wakiwa wanainama;+ na wale wote wanaokuvunjia heshima watainama penye nyayo za miguu yako,+ nao watakuita wewe jiji la Yehova, Sayuni+ wa Mtakatifu wa Israeli.
29 “ ‘ “Nami nitawainulia mmea ili kujifanyia jina,+ nao hawatakuwa tena wale walioondolewa na njaa katika nchi,+ nao hawatachukua fedheha tena kamwe kutoka kwa mataifa.+
19 Tazama, ninachukua hatua juu ya wote wanaokutesa, wakati huo;+ nami nitamwokoa yeye anayechechemea,+ na yeye ambaye ametawanywa nitamkusanya pamoja.+ Nami nitawaweka kuwa sifa na kuwa jina katika nchi yote ya aibu yao.