4 Kwa hiyo, kwa kweli nitauacha moyo wa Farao uwe mkaidi,+ naye hakika atawafuatilia wao nami nitajipatia utukufu kupitia kwa Farao na majeshi yake yote;+ nao Wamisri watajua hakika kwamba mimi ni Yehova.”+ Basi wakafanya vivyo hivyo.
19 Na sasa, Ee Yehova Mungu wetu,+ tafadhali, utuokoe+ kutoka mkononi mwake, ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe, Ee Yehova, ndiye Mungu peke yako.”+
23 ‘Nami hakika nitalitakasa jina langu kuu,+ ambalo lilikuwa likitiwa unajisi katikati ya mataifa, ambalo ninyi mlilitia unajisi katikati yao; nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘wakati nitakapotakaswa katikati yenu mbele ya macho yao.+
21 “ ‘Nami nitaweka utukufu wangu kati ya mataifa; na mataifa yote yatalazimika kuiona hukumu yangu ambayo nimeitenda+ na mkono wangu ambao nimeuweka katikati yao.+