2 Wafalme
19 Na ikawa kwamba mara tu Mfalme Hezekia+ aliposikia, mara moja akayararua mavazi yake,+ akavaa nguo za magunia,+ akaingia ndani ya nyumba ya Yehova.+ 2 Na zaidi ya hayo, akamtuma Eliakimu,+ aliyekuwa juu ya hiyo nyumba, na Shebna+ mwandishi na wanaume wazee wa makuhani wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa Isaya+ nabii, mwana wa Amozi.+ 3 Nao wakamwambia: “Hezekia amesema hivi, ‘Leo ni siku ya taabu+ na ya kemeo+ na ya dharau yenye dhihaka;+ kwa maana wana wamefika mpaka kwenye mlango wa tumbo la uzazi,+ na hakuna nguvu za kuzaa.+ 4 Pengine Yehova Mungu wako atayasikia+ maneno yote ya Rabshake, ambaye mfalme wa Ashuru bwana wake alimtuma ili kumdhihaki+ Mungu aliye hai, naye kwa kweli atamtoza hesabu kwa ajili ya maneno ambayo Yehova, Mungu wako, ameyasikia.+ Nawe uinue sala+ kwa ajili ya mabaki+ ambao wanapatikana.’”
5 Basi watumishi wa Mfalme Hezekia wakaingia kwa Isaya.+ 6 Ndipo Isaya akawaambia: “Mwambieni bwana wenu, ‘Yehova amesema hivi:+ “Usiogope+ kwa sababu ya maneno uliyosikia ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamesema vibaya kunihusu.+ 7 Tazama, ninatia roho+ ndani yake, naye atasikia habari+ na kurudi katika nchi yake mwenyewe; nami hakika nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.”’”+
8 Baada ya hapo Rabshake+ akarudi na kumkuta mfalme wa Ashuru akipigana na Libna;+ kwa maana alikuwa amesikia kwamba ameondoka Lakishi.+ 9 Alisikia ikisemwa hivi kumhusu Tirhaka mfalme wa Ethiopia: “Tazama, amekuja kupigana nawe.” Kwa hiyo akatuma wajumbe+ tena kwa Hezekia, na kusema: 10 “Mwambieni hivi Hezekia mfalme wa Yuda, ‘Usiache Mungu unayemtegemea akudanganye,+ na kusema: “Yerusalemu+ halitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 11 Tazama! Wewe mwenyewe umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru walizitendea nchi zote kwa kuziangamiza;+ na je, wewe mwenyewe utakombolewa?+ 12 Je, miungu+ ya mataifa ambayo mababu zangu waliharibu imeyakomboa, naam, Gozani+ na Harani+ na Resefu na wana wa Edeni+ waliokuwa katika Tel-asari?+ 13 Yuko wapi—mfalme wa Hamathi+ na mfalme wa Arpadi+ na mfalme wa majiji ya Sefarvaimu, Hena na Iva?’”+
14 Ndipo Hezekia akaichukua ile barua kutoka mkononi mwa wale wajumbe, akaisoma,+ kisha Hezekia akaenda katika nyumba ya Yehova, akaitandaza mbele za Yehova.+ 15 Na Hezekia akaanza kusali+ mbele za Yehova na kusema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli,+ unayeketi juu ya makerubi,+ wewe peke yako ndiye Mungu wa kweli wa falme+ zote za dunia.+ Wewe mwenyewe umezifanya mbingu+ na dunia.+ 16 Tega sikio lako, Ee Yehova, usikie.+ Fungua macho yako,+ Ee Yehova, uone, na uyasikie maneno ya Senakeribu ambayo ametuma ili kumdhihaki+ Mungu aliye hai. 17 Ee Yehova, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameharibu mataifa na nchi zao.+ 18 Nao wameiteketeza miungu yao kwa moto, kwa sababu hiyo haikuwa miungu,+ bali kazi ya mikono ya mwanadamu,+ miti na mawe; hivi kwamba wakaiharibu. 19 Na sasa, Ee Yehova Mungu wetu,+ tafadhali, utuokoe+ kutoka mkononi mwake, ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe, Ee Yehova, ndiye Mungu peke yako.”+
20 Na Isaya mwana wa Amozi akatuma habari kwa Hezekia, na kusema: “Yehova, Mungu wa Israeli amesema hivi,+ ‘Nimeisikia+ sala+ ambayo umenitolea kumhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru. 21 Yehova amesema neno hili juu yake:
“Bikira, binti Sayuni, amekudharau,+ amekudhihaki.+
Binti Yerusalemu+ ametikisa kichwa+
chake nyuma yako.
22 Umemdhihaki+ nani na kusema vibaya+ juu
yake?
Nawe umepaaza sauti+
yako juu ya nani
Na kuinua macho+ yako juu?
Ni juu ya Mtakatifu wa Israeli!+
23 Umemdhihaki Yehova kupitia wajumbe+ wako, nawe unasema,+
‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita+ mimi mwenyewe—
Mimi hakika nitapanda vilele vya maeneo yenye milima,+
Sehemu za mbali zaidi za Lebanoni;+
Nami nitaikata mierezi+ yake iliyotukuka, miberoshi+ yake iliyo bora.
Nami nitaingia mahali pake pa mwisho pa kukaa, msitu wa shamba lake la matunda.+
24 Mimi hakika nitachimba na kunywa maji mageni,
Nami nitaikausha mifereji yote ya Nile ya Misri kwa nyayo za miguu yangu.’+
25 Je, hujasikia?+ Tangu nyakati za zamani za kale ndilo nitakalofanya.+
Tangu siku zilizopita nimelifanya.+
Sasa nitalitimiza.+
Nawe utafanya majiji yenye ngome yawe ukiwa kama marundo ya mabomoko.+
26 Na wakaaji wao watakuwa na mikono minyonge;+
Wataingiwa na hofu tupu na kuona aibu.+
Watakuwa kama majani ya shambani na majani mabichi yaliyo laini,+
Majani ya dari,+ kunapokuwa na kuunguzwa mbele ya upepo wa mashariki.+
27 Nami najua vema+ kuketi kwako kimya na kuondoka+ kwako na kuingia kwako,
Na kujichochea kwako juu yangu,+
28 Kwa sababu kujichochea kwako juu yangu+ na kunguruma kwako kumepanda mpaka ndani ya masikio yangu.+
Nami hakika nitatia kulabu yangu puani mwako na lijamu yangu katikati ya midomo yako,+
Nami hakika nitakurudisha kupitia njia ile uliyoijia.”+
29 “‘Na hii itakuwa ndiyo ishara kwa ajili yako:+ Mimea inayochipuka kutokana na mbegu zilizoanguka+ italiwa mwaka huu, na katika mwaka wa pili nafaka inayochipuka yenyewe; lakini katika mwaka wa tatu pandeni mbegu,+ na mvune na mpande mashamba ya mizabibu na kula mazao yake.+ 30 Na wale watakaoponyoka wa nyumba ya Yuda, wale wanaobaki,+ hakika watatia mizizi kwenda chini na kuzaa matunda kwenda juu.+ 31 Kwa maana mabaki watatoka katika Yerusalemu,+ na wale wanaoponyoka katika Mlima Sayuni.+ Bidii+ ya Yehova wa majeshi itatenda hayo.
32 “‘Ndiyo sababu Yehova amesema hivi kumhusu mfalme wa Ashuru:+ “Hataingia katika jiji+ hili wala hatapiga mshale+ humo wala kulikabili kwa ngao wala kujenga juu yake boma la kulizingira.+ 33 Atarudi kupitia ile njia aliyoijia, naye hataingia ndani ya jiji hili, asema Yehova.+ 34 Nami hakika nitalilinda+ jiji hili ili kuliokoa kwa ajili yangu mwenyewe+ na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”’”+
35 Na ikawa kwamba usiku huo malaika wa Yehova alitoka, akapiga na kuwaua watu 185,000 katika kambi+ ya Waashuru.+ Watu walipoamka asubuhi na mapema, tazama, wote walikuwa mizoga iliyokufa.+ 36 Kwa hiyo Senakeribu+ mfalme wa Ashuru akaondoka, akaenda, akarudi,+ akaanza kukaa katika Ninawi.+ 37 Na ikawa kwamba alipokuwa akiinama nyumbani mwa Nisroki+ mungu wake,+ Adrameleki na Shareza, wanawe yeye mwenyewe, wakampiga na kumuua kwa upanga,+ nao wakakimbia, wakaenda katika nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.