31 na katika nyika,+ mahali ambapo uliona jinsi Yehova Mungu wako alivyokuchukua+ kama vile mtu anavyomchukua mwana wake, katika njia yote mliyoitembea mpaka mlipokuja hapa.’+
11 Atalichunga kundi lake mwenyewe kama mchungaji.+ Atawakusanya pamoja wana-kondoo kwa mkono wake;+ naye atawabeba katika kifua chake.+ Wale wanaonyonya atawaongoza kwa uangalifu.+
3 “Nisikilize mimi, Ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote mnaobaki wa nyumba ya Israeli,+ ninyi niliowachukua tangu tumboni, ambao mmechukuliwa toka tumbo la uzazi.+
9 Wakati wa taabu zao zote hilo lilimtaabisha.+ Na mjumbe wake binafsi akawaokoa.+ Katika upendo wake na katika huruma yake yeye mwenyewe aliwakomboa,+ naye akawainua na kuwachukua siku zote za zamani za kale.+