2 Na itatukia katika siku za mwisho+ kwamba mlima wa nyumba+ ya Yehova utawekwa imara juu ya kilele cha milima,+ nao utainuliwa juu ya vilima;+ na mataifa yote yatamiminika huko.+
10 Na itakuwa katika siku hiyo+ kwamba patakuwa na mzizi wa Yese+ ambao utakuwa unasimama kuwa ishara kwa ajili ya vikundi vya watu.+ Mataifa yatamtafuta yeye ili kuuliza habari zake,+ na mahali pake pa kupumzikia patakuwa patukufu.+
10 “Na hesabu ya wana wa Israeli itakuwa kama chembe za mchanga wa bahari ambao hauwezi kupimwa wala kuhesabiwa.+ Na itakuwa kwamba mahali ambapo walikuwa wakiambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’+ wataambiwa, ‘Wana wa Mungu aliye hai.’+
11 Lakini ninawaambia ninyi kwamba wengi kutoka sehemu za mashariki na sehemu za magharibi+ watakuja na kuketi kwenye meza pamoja na Abrahamu na Isaka na Yakobo katika ufalme+ wa mbinguni;+