Zaburi
Kwa kiongozi juu ya Paa wa Mapambazuko. Muziki wa Daudi.
22 Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+
Kwa nini uko mbali usiniokoe,+
Mbali na maneno ya mngurumo wangu?+
2 Ee Mungu wangu, mimi huendelea kuita wakati wa mchana, nawe huitiki;+
Na wakati wa usiku, wala sinyamazi.+
7 Wale wote wanaoniona mimi, hunidharau;+
Wanaendelea kufungua vinywa vyao wazi, wanaendelea kutikisa vichwa vyao:+
8 “Yeye alijitia mikononi mwa Yehova.+ Acha Yeye amwokoe!+
Na amkomboe, kwa kuwa yeye amependezwa naye!”+
9 Kwa maana Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+
Wewe ndiye unayenifanya niwe na tegemeo nilipokuwa kwenye maziwa ya mama yangu.+
10 Nimetupwa kwako kutoka tumbo la uzazi;+
Kutoka katika tumbo la mama yangu wewe umekuwa Mungu wangu.+
Na mifupa yangu yote imetenganishwa.+
Moyo wangu umekuwa kama nta;+
Umeyeyuka ndani katika sehemu zangu za ndani.+
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae cha udongo,+
Na ulimi wangu umefanywa ushikamane na ufizi wangu;+
Nawe unaniweka katika mavumbi ya kifo.+
16 Kwa maana mbwa wamenizingira;+
Kusanyiko la watenda-maovu limenizunguka.+
Wako kwenye mikono yangu na miguu yangu kama simba.+
21 Uniokoe kutokana na kinywa cha simba,+
Na unijibu na kuniokoa kutokana na pembe za ng’ombe-mwitu.+
23 Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni!+
Enyi nyote mlio uzao wa Yakobo, mtukuzeni!+
Na mwogopeni yeye, enyi nyote mlio uzao wa Israeli.+
Wala kuchoshwa na mateso ya mwenye kuteseka;+
Naye hakumficha uso wake,+
Naye alipomlilia amsaidie alisikia.+
25 Kutoka kwako sifa yangu itakuwa katika kutaniko kubwa;+
Nadhiri zangu nitazitimiza mbele ya wale wanaomwogopa.+
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kurudi kwa Yehova.+
Na familia zote za mataifa zitainama mbele zako.+