5 Na sasa ikiwa mtaitii+ sauti yangu kabisa na kulishika kwa kweli agano+ langu, ndipo hakika mtakapokuwa mali yangu ya pekee kutoka kati ya vikundi vingine vyote vya watu,+ kwa sababu dunia nzima ni yangu.+
6 Kwa maana ninyi ni watu watakatifu kwa Yehova Mungu wenu.+ Ni ninyi ambao Yehova Mungu amewachagua ninyi muwe watu wake, mali ya pekee, kutoka kati ya vikundi vyote vya watu vilivyo kwenye uso wa nchi.+
15 Ila Yehova alishikamana na mababu zako na kuwapenda, hivi kwamba akachagua uzao wao baada yao,+ naam, ninyi, kutoka kati ya vikundi vyote vya watu, kama ilivyo leo hii.
17 “Nao watakuwa wangu,”+ Yehova wa majeshi amesema, “siku ile nitakapotokeza mali ya pekee.+ Nami nitawaonyesha huruma, kama vile mwanamume anavyomwonyesha huruma mwana wake ambaye anamtumikia.+