Amosi
3 “Lisikieni neno hili ambalo Yehova amesema kuwahusu ninyi,+ enyi wana wa Israeli, kuhusu familia nzima niliyoitoa katika nchi ya Misri,+ nikisema, 2 ‘Mimi nimewajua ninyi peke yenu+ kati ya familia zote za nchi.+ Hiyo ndiyo sababu nitawatoza ninyi hesabu kwa sababu ya makosa yenu yote.+
3 “‘Je, watu wawili watatembea pamoja isipokuwa wawe wamekutana kwa mapatano?+ 4 Je, simba atanguruma mwituni wakati hana mawindo yoyote?+ Je, mwana-simba mwenye manyoya shingoni atatoa sauti mafichoni mwake ikiwa hakukamata chochote? 5 Je, ndege ataanguka ndani ya mtego chini ikiwa hakuna mnaso kwa ajili yake?+ Je, mtego huteguka udongoni ikiwa haujakamata chochote kamwe? 6 Je, baragumu ikipigwa katika jiji, watu wenyewe pia hawatetemeki?+ Je, msiba ukitokea katika jiji, Yehova siye pia aliyetenda? 7 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hatafanya lolote isipokuwa awe amewafunulia watumishi wake manabii jambo lake la siri.+ 8 Kuna simba ambaye amenguruma!+ Ni nani hataogopa? Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova mwenyewe amesema! Ni nani ambaye hatatoa unabii?’+
9 “ ‘Litangazeni kwenye minara ya makao katika Ashdodi na juu ya minara ya makao ya nchi ya Misri,+ na kusema: “Kusanyikeni pamoja juu ya milima ya Samaria,+ mwone machafuko mengi yaliyo katikati yake na visa vya upunjaji vilivyo ndani yake.+ 10 Nao hawajajua jinsi ya kufanya yaliyo manyoofu,”+ asema Yehova, “wale wanaoweka jeuri+ akiba na uporaji katika minara ya makao yao.” ’
11 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kuna adui kuzunguka nchi,+ naye atazishusha nguvu zako zikutoke, na minara ya makao yako itaporwa.’+
12 “Yehova amesema hivi, ‘Kama vile mchungaji anavyonyakua miguu miwili au kipande cha sikio kutoka katika kinywa cha simba,+ ndivyo wana wa Israeli watakavyonyakuliwa, wale wanaokaa katika Samaria kwenye kitanda cha utukufu+ na kwenye kitanda cha Damasko.’+
13 “ ‘Sikieni na kutoa ushahidi+ katika nyumba ya Yakobo,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Mungu wa majeshi. 14 ‘Maana, siku yangu ya kutoza hesabu+ kwa sababu ya maasi ya Israeli juu yake, mimi nitazitoza hesabu pia madhabahu za Betheli;+ na pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.+ 15 Nami nitaiangusha nyumba ya wakati wa majira ya baridi+ kali pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi.’+
“ ‘Na nyumba za pembe za tembo zitaangamia,+ na nyumba nyingi zitakwisha,’+ asema Yehova.”